Tabia hii ya AirTel ikome.

sekulu

JF-Expert Member
Jan 17, 2011
988
157
Ndugu wana JF,
Nawasalimu.

Naomba kutoa yangu ya Moyoni kuhusu huu mtandao wa sim wa AIRTEL kwa wateja wao waotumia huduma ya ONE NETWORK.

Hivi ninavoongea tangu jana mida kama ya saa saba mchana wateja wa Zain Tanzania wanaotumia Huduma ya One Network Wakiwa Nchi ya Uganda Simu Zao Hazina Network Mpaka muda huu. Hii sio haki ya Mteja hata kidogo. Ukiwoana kwenye Matangazo yao wanatangaza one network kumbe wizi Mtupu kwa sababu zifuatazo:

Ukitoka Tanzania Ukienda Uganda, kenya na ukaendelea kutumia namba yako ya kitanzania utakatwa TSHS 45 kwa kupokea simu,wakati unaunganishwa na kampuni moja. siielewi hii!

Ukiwa na voda na ukiwa nchi ya UGANDA AN KEnya, Utapokea simu bure bila kukatwa hata cent!

Airtel hayo mambo mumeanza lini????????????
 
Hii ni kweli kabisa,nimexperience wakati nimekwenda mombasa nchini kenya kila unapopokea simu wanakukata sh.45 na watu wako wanakupata kwa shida sana kama sio kutopatikana kabisa.

Baada ya kufuatilia Airtel wenyewe walisema wanakata hiyo pesa ili kufinance exchange deficity inayojitokeza katika nchi zenye mtandao wa Airtel.

Kwa kweli hata mimi sioni logic ya kukata pesa kwani huu ni upuzi na wizi na recently wameingia mkataba na IBM kumanage connection zao zote.

Mbona wakati wa zain haya mambo hayakuwepo? Ilikuwa ukimpigia mtu ambae yuko nje ya Tanzania unampata bila ya shida yoyote na hakatwi hata sh.1?

Wana JF wanaofanyakazi Airtel naomba watufafanulie zaidi je huu ni uhuru wa mawasiliano kama wanavyojitangaza au ndio wamekuwa dictator wa mawasiliano kiuhalisia??
 
Yani vurugu tupu, I wish irudi ZAIN na Sio AIRTEL

Very hopeless, Na kwa hapa Uganda ndo Hovyo kupita maelezo, Hapa Uganda unatuma Sms kwa 86 na unapopiga simu hela yako ya KiTZ wanaifanya kama ya Kiganda and therefore kuweza kupiga simu ni lazima uwe na kwanzia Mia 5 ndo unaweza kupiga simu.

Bora Kenya Sms unatuma Kwa sh 45 za kitanzania (kama sijakosea)

Voda Kila kitu ni bure na unaweza kumbeep mtu hata ukiwa na sh 4 ya kitanzania
 
Naelekea Kampaka kesho bandugu. Naombeni ushauri nende na line ipi ya huku Tz ambayo nitaweza kuitumia kuwasikiana na watu wangu wa huku bika makato yoyote? ..

Naomba pia kujua je vocha nitaweza kutumia za Uganda au ni mpaka ni recharge kwa kutumia vocha za huku Tz?

Je nitaweza kuunga vifurushi vya Tz? Au nitatumia vya huko Uganda?

Natanguliza shukrani

Hate me at your own risk
 
Naelekea Kampaka kesho bandugu. Naombeni ushauri nende na line ipi ya huku Tz ambayo nitaweza kuitumia kuwasikiana na watu wangu wa huku bika makato yoyote? ..

Naomba pia kujua je vocha nitaweza kutumia za Uganda au ni mpaka ni recharge kwa kutumia vocha za huku Tz?

Je nitaweza kuunga vifurushi vya Tz? Au nitatumia vya huko Uganda?

Natanguliza shukrani

Hate me at your own risk
Nenda na VODA
 
Back
Top Bottom