Tabata hatuna maji wiki nzima

Tabata hatuna maji wiki nzima

inchaji

JF-Expert Member
Joined
Jul 5, 2019
Posts
2,628
Reaction score
5,427
Tunaomba mamlaka husika zichukue hatua au zichukuliwe hatua. Tabata na vitongoji vyake na pengine tabata nzima maji ya dawasco hayatoki na hakuna taarifa yoyote.

Tangu mzee Magufuli aende kupumzika kwao tumekatiwa maji. mambo mengi napishanaga nae huyu mzee na chama chake ila suala la kupiga spana watumishi mizigo niko nae mia kwa mia.
 
We INCHAJI wa TABATA achaneni na maji sio issue. Kwa sasa mtanunua maji ya dukani UHAI, MASAFI, KISIMA n.k ... yanapatika kwa wingi

Pia maofisa wetu kwa kushirikiana na Serekali za Mitaa wamedhibiti bei hivyo yanapatika kwa gharama nafuu sana kwa wanyonge

Anyways kwa sasa tupo busy kuandaa mradi kuwaletea gesi majumbani

Mitano Tena !!!
 
tunaomba mamlaka husika zichukue hatua au zichukuliwe hatua. tabata na vitongoji vyake na pengine tabata nzima maji ya dawasco hayatoki na hakuna taarifa yoyote....
Tatizo watanzania tulizoea kuishi kiujanja ujanja Ndio maana tunaumia.

Tii sheria bila shuruti.

Lipa Ankara za maji upate huduma.

Tabata nyie ni wadeni sugu mnafikiri huduma ni bure kama zamani?

Awamu hii ya Rais mwema mwenye Moyo wa huruma na upendo kwa RAIA wake Ukitaka kufaidi acha ujanja janja.

La sivyo utaumia sana maana mianya ya wapiga dili imeziba kabisa
 
Walianza miaka mitano ya kwanza kabla ya kutaja jina wakawa wanaanza hivi , Raisi Wetu Mpendwa Daktari John Joseph Pombe Magufuli, Hii Awamu Ya Pili Wanasema Raisi Joseph John Pombe Magufuli, Akishastaafu watakua wanamwita Mzee Magufuli.
 
Vumilieni ndiyo mambo ya uchumi wa kati wa chini hayo
 
Taarifa ya Dharura,Mtambo wa Kuzalisha maji Ruvu Juu umesimama kutokana na hitilafu ya umeme iliyosababishwa na kuanguka kwa Nguzo 9 za umeme kutoka Chalinze hadi Mlandizi. Mafundi wa TANESCO na DAWASA wanaendelea na jitihada za kutatua tatizo.Huduma inatarajiwa kurejea baada ya saa 24,hivyo Tunakusihi kuhifadhi na kuzingatia matumizi bora ya maji..

Taarifa ya Dharura,Mtambo wa Kuzalisha maji Ruvu Juu umezima tangu saa 7:46 mchana wa leo 23/1/2021 baada ya kutokea hitilafu ya umeme.Mafundi wa TANESCO wanafuatilia kubaini chanzo ili kuweza kulishughulikia kwa haraka.DAWASA itatoa taarifa mara uzalishaji maji utakaporejea,hivyo Tunakusihi kuhifadhi na kuzingatia matumizi bora ya maji..
 
Nunueni maji ya chupa! uhai,afya,ishi,hill

Mitano tena
 
Tatizo watanzania tulizoea kuishi kiujanja ujanja Ndio maana tunaumia...
Mkuu kwan kakwambia hajlipa bili ?, mambo mengine bana , acha ujinga mkuu, kwamba Maji hayatoki sehem zote , kwa hiyo unataka kusema , watu wote tabata nzima hawajalipa bill
 
Back
Top Bottom