Tabasamu la JK na utingo aliyeachwa na dereva

Tabasamu la JK na utingo aliyeachwa na dereva

Unapoiona semi inayoyoma barabarani, sifa sio kwa dereva pekee.

Unapoona gari la abiria limefika salama safari yake sifa na shukrani sio kwa dereva pekee.

Unapoona hesabu ya tajiri imetimia tambua nyuma ya dereva kuna msaidizi muhimu almaarufu kama konda ama kwa Kiswahel sanifu, utingo.

Makonda (sio mabarcity) ni watu muhimu sana kwenye tasnia nzima ya usafiri. Kwenye magari ya mizigo ndio wasimamizi wa kupakia na kuhakikisha mzigo umefungwa vema.

Ndio wanaosimamia service ya gari, ndio wanaojua shida zote za gari hata inapopata pancha n.k n.k, na hata dereva anapochoka ama kwenda kuosha rungu kwa mpango wa kando utingo ndio hubaki na gari.

Mabus ya mikoani tunajua dhima kubwa ya makonda kuanzia kupakia abiria mpaka ku-overtake barabarani na matangazo yote safarini na dharura.

Kwenye daladala zetu ndio unaweza kuona nguvu halisi ya makonda. Yeye ndio wa kuamrisha gari isimame ama itembee ni mshika pesa ni mpanga matumizi nk nk.

Chini ya makonda ndio kuna wasaidizi wengine wote inapotokea kutoelewana kati ya konda na dereva mambo huenda kombo. Ni wakati wa uchaguzi, kila chama kimeshapata dereva wake, na kila dereva atakuwa na utingo wake na kila utingo atakuwa na wasaidizi wake.

Wakati vyama vingine vikionekana kujipanga vema kitimu na kuwa wamoja, chama tawala kina makunyanzi mengi. Makonda na wasaidizi muhinu wanaonesha wazi hawana furaha ama hawako pamoja na dereva wa jahazi, makada wote muhimu wako kimya kabisa!

Ninini kitatokea? CCM watachezeshwa segere mwanzo mwisho, watakuwa kama YANGA na SIMBA ama SAULI na NEW FORCE
Viwanjani ni SIMBA, SIMBA, SIMBAA.

Barabarani ni SAULI, SAULI, SAULI.

Nyuma ya tabasabu la JK kuna BM anacheka!

It seems watu wengi mnaipenda ccm kimya kimya,is like mnadhani bila ccm hakuna Tanzania? Acheeni ccm ijifie yenyewe,imetutesa sana watanzania,watoto wa watanzania hawana their future is uncertain sababu ya ccm then bado watu mnahangaika kuandika matatizo yao.Badala ya kuhamasisha watu tujipanga kuiong'oa ccm madarakani ama kwa kura au kwa nguvu ninyi mnahangaika na matatizo yao, IAM sorry for you guys
 
Hii sio kama ile ya PICHA KTK ULIMWENGU WA KIROHO!
20200805_143704.jpg
 
kuna nyakati maisha yanahtaji unafiki kidogo hivo kikwete atakua konda japo kinafiki zaidi.
 
Unapoiona semi inayoyoma barabarani, sifa sio kwa dereva pekee.

Unapoona gari la abiria limefika salama safari yake sifa na shukrani sio kwa dereva pekee.

Unapoona hesabu ya tajiri imetimia tambua nyuma ya dereva kuna msaidizi muhimu almaarufu kama konda ama kwa Kiswahel sanifu, utingo.

Makonda (sio mabarcity) ni watu muhimu sana kwenye tasnia nzima ya usafiri. Kwenye magari ya mizigo ndio wasimamizi wa kupakia na kuhakikisha mzigo umefungwa vema.

Ndio wanaosimamia service ya gari, ndio wanaojua shida zote za gari hata inapopata pancha n.k n.k, na hata dereva anapochoka ama kwenda kuosha rungu kwa mpango wa kando utingo ndio hubaki na gari.

Mabus ya mikoani tunajua dhima kubwa ya makonda kuanzia kupakia abiria mpaka ku-overtake barabarani na matangazo yote safarini na dharura.

Kwenye daladala zetu ndio unaweza kuona nguvu halisi ya makonda. Yeye ndio wa kuamrisha gari isimame ama itembee ni mshika pesa ni mpanga matumizi nk nk.

Chini ya makonda ndio kuna wasaidizi wengine wote inapotokea kutoelewana kati ya konda na dereva mambo huenda kombo. Ni wakati wa uchaguzi, kila chama kimeshapata dereva wake, na kila dereva atakuwa na utingo wake na kila utingo atakuwa na wasaidizi wake.

Wakati vyama vingine vikionekana kujipanga vema kitimu na kuwa wamoja, chama tawala kina makunyanzi mengi. Makonda na wasaidizi muhinu wanaonesha wazi hawana furaha ama hawako pamoja na dereva wa jahazi, makada wote muhimu wako kimya kabisa!

Ninini kitatokea? CCM watachezeshwa segere mwanzo mwisho, watakuwa kama YANGA na SIMBA ama SAULI na NEW FORCE
Viwanjani ni SIMBA, SIMBA, SIMBAA.

Barabarani ni SAULI, SAULI, SAULI.

Nyuma ya tabasabu la JK kuna BM anacheka!

mwaka huu kuna mgombea atapiga nyeto jukwaani
 
kuna nyakati maisha yanahtaji unafiki kidogo hivo kikwete atakua konda japo kinafiki zaidi.
Facial expression itasema...moyo mfu hauwezi kuzaa neno chanya

Jr[emoji769]
 
Shida kuna wimbi la watu bado wana utopolo kichwani, sifa sifa za kiongozi kilaza wanazifulahia kinoma.
 
Hii tushaizoea hujirudia kila Mara kipindi cha uchanguzi
Pia kumbuka kuna wale watakaopigwa panga na kamati kuu Kwa kile alichoita polepole "waliopitishwa na wajumbe Kwa njia ya rushwa"
Mara nyingi watu hawa wakishakatwa huwa wanarudi upande wa pili na wapambe wao yaani Kwa kifupi tutegemee mvurugano zaidi.
 
Shida kuna wimbi la watu bado wana utopolo kichwani, sifa sifa za kiongozi kilaza wanazifulahia kinoma.
Mwaka huu sidhani...ujinga utakuwa. Umewatoka wengi

Jr[emoji769]
 
Kikwete atawezaje kwenda kwenye kampeni kwa furaha bila ya
Kinana aliyekuwa katibu mkuu wa chama enzi zake? Ya Kinana yanajulikana wazi...
Bila ya Mzee Mangula...anayeumwa kwa tuhuma za kupewa sumu?
Bila Bernard Membe waziri wa mambo ya nje enzi zake?

Waliobaki ni vijana wake ambao nao wana ya kwao mioyoni mwao...
Makamba January
Nchemba Lameck
Nape Nnauye

Hata kama ataenda..ataenda kama mwana mkiwa anayeficha maumivu yake kwa tabasamu la lazima
Perezida-mushya-wa-Tanzania-Dr-John-Pombe-Magufuli-ahoberana-na-Jakaya-Kikwete-ucyuye-igihe-ny...jpg
 
Kikwete atawezaje kwenda kwenye kampeni kwa furaha bila ya
Kinana aliyekuwa katibu mkuu wa chama enzi zake? Ya Kinana yanajulikana wazi...
Bila ya Mzee Mangula...anayeumwa kwa tuhuma za kupewa sumu?
Bila Bernard Membe waziri wa mambo ya nje enzi zake?

Waliobaki ni vijana wake ambao nao wana ya kwao mioyoni mwao...
Makamba January
Nchemba Lameck
Nape Nnauye

Hata kama ataenda..ataenda kama mwana mkiwa anayeficha maumivu yake kwa tabasamu la lazimaView attachment 1529523

Adjustments.jpg

[emoji1787][emoji1787][emoji1787]ana wa zoom tu
 
Ilikuwa hivi hivi 2015. Sound kibao Ccm kuna mpasuko Lowassa kahama na kijiji ila mwisho wa siku sio wewe wala wenzio mnaamini kilichotokea. We kama mtaalam wa mambo ya giza nilitegemea hili uwe ushaliona na umeijua tafsiri yake. Vita zingine hua unayaficha majeshi yako mlimani na kwenye mahandaki wakati wote wa mchana then wakati adui anaamini kauteka mji usiku unamshukia kwa nguvu zote. Matokeo hua ni maangamizi.. So endeleeni na mitazamo yenu isiyo na uhalisia.. Hamjifunzi
 
Ilikuwa hivi hivi 2015. Sound kibao Ccm kuna mpasuko Lowasa kahama na kijiji ila mwisho wa siku sio wewe wala wenzio mnaamini kilichotokea. We kama mtaalam wa mambo ya giza nilitegemea hili uwe ushaliona na umeijua tafsiri yake. Vita zingine hua unayaficha majeshi yako mlimani na kwenye mahandaki wakati wote wa mchana then wakati adui anaamini kauteka mji usiku unamshukia kwa nguvu zote. Matokeo hua ni maangamizi.. So endeleeni na mitazamo yenu isiyo na uhalisia.. Hamjifunzi
giphy.gif


Jr[emoji769]
 
Hata mimi sipendi CCM washinde uchaguzi. Nadhani wanahitaji kupewa some time out! Hata hivyo, kutopenda kwangu CCM kushinda uchaguzi hakuwezi kuifanya ishindwe uchaguzi. Lazima tuwe realistic katika assessments zetu. Vinginevyo, tutakuwa watu wa kutafuta visingizio kila baada ya matokeo ya uchaguzi kutangazwa!

Kwa hali ya kisiasa ilivyo sasa, hakuna chama chenye nguvu ya kuiangusha CCM. Sababu zilizopelekea wapinzani kushindwa 2015 bado ni zile zile na ndizo zitakazopelekea wapinzani washindwe tena (pengine vibaya zaidi) mwaka huu.

Kama hufanyi hili kwa ushabiki wa kisiasa au for the sake of it, basi jenga utamaduni wa kupitia assessments zako za election cycles zilizotangulia ili kuepuka kurudia makosa uliyoyafanya siku za nyuma na hivyo kuboresha current assessment yako.
 
Hivi vyama vya upinzani havipo kimkakati kwasababu vilitakiwa kuwa na Malengo kwa mfano miaka 10 au mhula wa Jk wote wao walipaswa Kua wanamuuanda mtu ambaye sasa angesimama kama mpinzani sio hii yakusubiri mtu anatoka ccm eti wao ndio wanamuweka mgombea hii haitakaa ifanikiwe
Laxima wamuandee mtu miaka hata 15 theni aje asimame ndio wataingusha ccm
 
Hao makada muhimu, walio kimya ni kina nani? Toka lini CCM inategemea individuals ambao hawana lolote la kuongeza? Unavyoona uchaguzi huu, mbona hujasema sijamuona Manji na wafadhili wenzake wa chama enzi zile wakichangia chama?

Mambo yanabadilika sana. Siasa za 2020 ni tofauti sana na 2015 au 2010. Pengine kuna namna tulizoea sasa tunachokiona tunafikiri ni ishara ya kushindwa.

Trust me, waswahili wana usemi kwamba debe tupu haliachi kutika. Debe limejaa maji ndani, kelele zinatoka wapi?
 
Hivi vyama vya upinzani havipo kimkakati kwasababu vilitakiwa kuwa na Malengo kwa mfano miaka 10 au mhula wa Jk wote wao walipaswa Kua wanamuuanda mtu ambaye sasa angesimama kama mpinzani sio hii yakusubiri mtu anatoka ccm eti wao ndio wanamuweka mgombea hii haitakaa ifanikiwe
Laxima wamuandee mtu miaka hata 15 theni aje asimame ndio wataingusha ccm
Mmh mgombea wa mwaka huu ni mpinzani pure lakini

Jr[emoji769]
 
Hao makada muhimu, walio kimya ni kina nani? Toka lini CCM inategemea individuals ambao hawana lolote la kuongeza? Unavyoona uchaguzi huu, mbona hujasema sijamuona Manji na wafadhili wenzake wa chama enzi zile wakichangia chama?

Mambo yanabadilika sana. Siasa za 2020 ni tofauti sana na 2015 au 2010. Pengine kuna namna tulizoea sasa tunachokiona tunafikiri ni ishara ya kushindwa.

Trust me, waswahili wana usemi kwamba debe tupu haliachi kutika. Debe limejaa maji ndani, kelele zinatoka wapi?
Mmoja wetu kati yetu anaweza kuwa sahihi hebu tuupe wakati muda...tutarudi hapa kukumbushana

Jr[emoji769]
 
Mmoja wetu kati yetu anaweza kuwa sahihi hebu tuupe wakati muda...tutarudi hapa kukumbushana

Jr[emoji769]

Kwa hilo sababu umeiweka hekima mbele, yes, muda utaongea.
Kila zama na nabii wake. I suspect pia kila zama na vigogo wake. Shida ni kuwa kuna watanzania walishajipa titles ambazo hazipo popote kisheria. Ndio wanaopata tabu
 
Kwa hilo sababu umeiweka hekima mbele, yes, muda utaongea.
Kila zama na nabii wake. I suspect pia kila zama na vigogo wake. Shida ni kuwa kuna watanzania walishajipa titles ambazo hazipo popote kisheria. Ndio wanaopata tabu
Asante ...muda ni hakimu mzuri ....huongea kwa sauti isiyo na kigugumizi....tujipe muda...tutaisikia....na mwangwi wake pia
 
Back
Top Bottom