Taazia: Sheikh Saud Bin Ahmed al Busaidi hakukata tamaa na rehma za Allah

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,917
30,259
TAAZIA: SHEIKH SAUD BIN AHMED AL BUSAIDI
HAKUKATA TAMAA NA REHMA ZA ALLAH



Sheikh Saud bin Ahmed Al Busaid
(Picha kutoka katika kitabu chake)


Nimepata taaarifa ya msiba wa Sheikh Saud bin Ahmed Al Busaidi jana usiku kutoka Abu Dhabi kwa rafiki yangu Abdul Aleem Attas. Mara ya mwisho tulionana Dar es Salaam yapata zaidi ya miaka 20 iliyopita na tukapoteana hadi siku tatu zilizopita bada ya mmoja wa jamaa zake kuniunganisha na yeye baada ya kusoma historia fupi niliyoandika ya harakati za kudai uhuru wa Tanganyika na nikamtajaa baba yake mdogo Shariff Abdallah Attas, mtu maarufu katika Dar es Salaam ya 1950. Akijua mapenzi yangu ya vitabu Abdul Aleem akaniambia kuwa kaninunulia kitabu cha marehemu mzee wetu, ‘’Memoirs of an Oman Gentlemn from Zanzibar.’’ Nilimfahamisha kuwa kitabu ninacho toka kilipotoka na alinipa mwandishi mwenyewe na kina sahihi yake.

Nawapa pole wafiwa wote khasa Dr. Rawya Saud Al Busaidi. Allah awape subra wafiwa wote na Allah amweke baba yetu mahali pema peponi.

Hakika ni vigumu sana kuandika taazia ya mtu ambae hukupata kumjua kwa karibu. Lakini juu ya ukweli huu naamini nina dhima ya kusema kitu kidogo kuhusu msomi huyu wa Chuo Kikuu Cha Oxford kutoka Zanzibar ingawa lazima nikiri kuwa nimemjua Sheikh Saud kwa kusoma kitabu chake, ambacho kwa ukamilifu si tu ni histori ya maisha yake binafsi bali pia ni historia ya Zanzibar inayorudi nyuma kiasi cha karne moja hivi sasa. Kitabu hiki ninacho na namshukuru Allah kuwa alinipa mwenyewe kupitia rafiki yangu Dr. Harith Ghassany na kama nilivyokwisa kusema kina sahihi yake. Kitabu hiki kipo katika Maktaba yangu. Nina furaha ya kusema pia kuwa kitabu hiki nilikifanyia pito (book review) ili wasomaji wafahamu umuhimu wa kukisoma.



Kama ilivyo kawaida ya kumbukumbu zilizoandikwa na wa wale ambao walishuhudia mainduzi na kisha walikimbia Zanzibar baada ya mapinduzi, historia ya Sheikh Saud bin Ahmed Al Busaidi inafuata mkondo ule ule wa kuanza kuelezea Zanzibar iliyokuwa imetulia na mahali pazuri pa kuishi kisha ikafuatia maisha ya shida, wasiwasi, vifungo na mauaji na mwisho kwa wale waliiobahatika kukimbia nchi wakiwa hai, maisha ya uhamishoni na mwisho kuishia takriban wengi wao, katika faraja na ustawi katika nchi mpya walizohamia, iwe ni UAE au Oman. Haya nimeyasoma katika kitabu cha Sheikh Ali Muhsin, ‘’Conflict and Harmony in Zanzibar,’’ na katika kitabu cha Muhammad Al - Marhuby kuhusu maisha ya baba yake Sheikh Amor Ali Ameir Al Marhubi, ‘’Amor Ali Ameir His Life and Legacy My Father.’’ HIstoria hii kwa wengi ni faraja.

Kumbukumbu hizi zimatuachia elimu ya kutosha ya kuweza kuijua kwa undani historia ya kweli ya Zanzibar. Historia ya maisha ya Sheikh Saud bin Ahmed Al Busaidi unaweza ukaipa jina, ‘’A Tale of Two Revolutions.’’ Aliondoka Zanzibar baada ya mapinduzi ya mwaka wa 1964 kisha akaondoka Libya baada ya mapinduzi ya 1969 yaliyomuingiza Muammar Gadafi madarakani. Kati ya mapinduzi haya Sheikh Saud hakukata tamaa katika maisha yake alifanya kazi kwa juhudi kubwa na hakutaka kuangalia nyuma na kujisikitikia. Kila siku yake ilikuwa siku mpya iliyompa nafasi ya kuangalia mbele na kushinda changamoto mpya zilizojitokeza ama akiwa Kenya baada ya kukimbia Zanzibar, Misri, Libya au Oman.

Mwaka wa 1970 Sultan Qaboos alichukua uongozi wa Oman na akafungua milango kwa Waomani waliokuwa nje warejee kwenye nchi yao ya asili, Oman na watapokelewa kwa mikono miwili. Sheikh Saud bin Ahmed Al Busaidi alifunga mizigo na kwenda Oman mwaka wa 1971 na huu ukawa mwanzo wa maisha mapya ya furaha na umafanikio makubwa akiwa Oman akishiriki katika kutumikia nchi yake mpya kwa juhudi na mapenzi makubwa.

Mzee wetu katika kitabu chake kwa furaha amehitimisha kwa nukuu kutoka kwa William Shakespeare, ‘’All’s well that ends well.’’ Ameandika maneno haya akirudi nyuma kuiangalia nchi yake Zanzibar aliyoikimbia miaka 50 iliyopita lakini kwa rehma zake Allah amejikuta yuko tena Zanzibar kwa mapumziko akitokea Oman akiwa visiwani na wanae na wajukuu zake. Hii ilikuwa kwa hakika moja ya ndoto zake kuwa ifike siku arudi nchini kwake na aweze kukanyaga ardhi ambayo aliikanyaga akiwa mtoto mdogo akicheza katika vichochoro vya Mji Mkongwe.

Napenda kuhitimisha k kusem kuwa Sheikh Saud ameishi maisha yaliyokamilika akipanda milima na kushuka mabonde akiwa na ustahamilivu na mategemeo mema. Katika maisha yake ukisoma kitabu chake kunzia maisha yake Zanzibar hadi kuishia Oman yapo mazingatio mengi sana.

Allah ampanulie kaburi lake alijaze nuru na amweke mahali pema peponi.
Amin.
 
TAAZIA: SHEIKH SAUD BIN AHMED AL BUSAIDI
HAKUKATA TAMAA NA REHMA ZA ALLAH



Sheikh Saud bin Ahmed Al Busaid
(Picha kutoka katika kitabu chake)


Nimepata taaarifa ya msiba wa Sheikh Saud bin Ahmed Al Busaidi jana usiku kutoka Abu Dhabi kwa rafiki yangu Abdul Aleem Attas. Mara ya mwisho tulionana Dar es Salaam yapata zaidi ya miaka 20 iliyopita na tukapoteana hadi siku tatu zilizopita bada ya mmoja wa jamaa zake kuniunganisha na yeye baada ya kusoma historia fupi niliyoandika ya harakati za kudai uhuru wa Tanganyika na nikamtajaa baba yake mdogo Shariff Abdallah Attas, mtu maarufu katika Dar es Salaam ya 1950. Akijua mapenzi yangu ya vitabu Abdul Aleem akaniambia kuwa kaninunulia kitabu cha marehemu mzee wetu, ‘’Memoirs of an Oman Gentlemn from Zanzibar.’’ Nilimfahamisha kuwa kitabu ninacho toka kilipotoka na alinipa mwandishi mwenyewe na kina sahihi yake.

Nawapa pole wafiwa wote khasa Dr. Rawya Saud Al Busaidi. Allah awape subra wafiwa wote na Allah amweke baba yetu mahali pema peponi.

Hakika ni vigumu sana kuandika taazia ya mtu ambae hukupata kumjua kwa karibu. Lakini juu ya ukweli huu naamini nina dhima ya kusema kitu kidogo kuhusu msomi huyu wa Chuo Kikuu Cha Oxford kutoka Zanzibar ingawa lazima nikiri kuwa nimemjua Sheikh Saud kwa kusoma kitabu chake, ambacho kwa ukamilifu si tu ni histori ya maisha yake binafsi bali pia ni historia ya Zanzibar inayorudi nyuma kiasi cha karne moja hivi sasa. Kitabu hiki ninacho na namshukuru Allah kuwa alinipa mwenyewe kupitia rafiki yangu Dr. Harith Ghassany na kama nilivyokwisa kusema kina sahihi yake. Kitabu hiki kipo katika Maktaba yangu. Nina furaha ya kusema pia kuwa kitabu hiki nilikifanyia pito (book review) ili wasomaji wafahamu umuhimu wa kukisoma.



Kama ilivyo kawaida ya kumbukumbu zilizoandikwa na wa wale ambao walishuhudia mainduzi na kisha walikimbia Zanzibar baada ya mapinduzi, historia ya Sheikh Saud bin Ahmed Al Busaidi inafuata mkondo ule ule wa kuanza kuelezea Zanzibar iliyokuwa imetulia na mahali pazuri pa kuishi kisha ikafuatia maisha ya shida, wasiwasi, vifungo na mauaji na mwisho kwa wale waliiobahatika kukimbia nchi wakiwa hai, maisha ya uhamishoni na mwisho kuishia takriban wengi wao, katika faraja na ustawi katika nchi mpya walizohamia, iwe ni UAE au Oman. Haya nimeyasoma katika kitabu cha Sheikh Ali Muhsin, ‘’Conflict and Harmony in Zanzibar,’’ na katika kitabu cha Muhammad Al - Marhuby kuhusu maisha ya baba yake Sheikh Amor Ali Ameir Al Marhubi, ‘’Amor Ali Ameir His Life and Legacy My Father.’’ HIstoria hii kwa wengi ni faraja.

Kumbukumbu hizi zimatuachia elimu ya kutosha ya kuweza kuijua kwa undani historia ya kweli ya Zanzibar. Historia ya maisha ya Sheikh Saud bin Ahmed Al Busaidi unaweza ukaipa jina, ‘’A Tale of Two Revolutions.’’ Aliondoka Zanzibar baada ya mapinduzi ya mwaka wa 1964 kisha akaondoka Libya baada ya mapinduzi ya 1969 yaliyomuingiza Muammar Gadafi madarakani. Kati ya mapinduzi haya Sheikh Saud hakukata tamaa katika maisha yake alifanya kazi kwa juhudi kubwa na hakutaka kuangalia nyuma na kujisikitikia. Kila siku yake ilikuwa siku mpya iliyompa nafasi ya kuangalia mbele na kushinda changamoto mpya zilizojitokeza ama akiwa Kenya baada ya kukimbia Zanzibar, Misri, Libya au Oman.

Mwaka wa 1970 Sultan Qaboos alichukua uongozi wa Oman na akafungua milango kwa Waomani waliokuwa nje warejee kwenye nchi yao ya asili, Oman na watapokelewa kwa mikono miwili. Sheikh Saud bin Ahmed Al Busaidi alifunga mizigo na kwenda Oman mwaka wa 1971 na huu ukawa mwanzo wa maisha mapya ya furaha na umafanikio makubwa akiwa Oman akishiriki katika kutumikia nchi yake mpya kwa juhudi na mapenzi makubwa.

Mzee wetu katika kitabu chake kwa furaha amehitimisha kwa nukuu kutoka kwa William Shakespeare, ‘’All’s well that ends well.’’ Ameandika maneno haya akirudi nyuma kuiangalia nchi yake Zanzibar aliyoikimbia miaka 50 iliyopita lakini kwa rehma zake Allah amejikuta yuko tena Zanzibar kwa mapumziko akitokea Oman akiwa visiwani na wanae na wajukuu zake. Hii ilikuwa kwa hakika moja ya ndoto zake kuwa ifike siku arudi nchini kwake na aweze kukanyaga ardhi ambayo aliikanyaga akiwa mtoto mdogo akicheza katika vichochoro vya Mji Mkongwe.

Napenda kuhitimisha k kusem kuwa Sheikh Saud ameishi maisha yaliyokamilika akipanda milima na kushuka mabonde akiwa na ustahamilivu na mategemeo mema. Katika maisha yake ukisoma kitabu chake kunzia maisha yake Zanzibar hadi kuishia Oman yapo mazingatio mengi sana.

Allah ampanulie kaburi lake alijaze nuru na amweke mahali pema peponi.
Amin.

Unajua Bwana Mohamed Said kutokana na mapenzi yako makubwa ya kila kitu Kiislamu na Uarabu basi kwako yo yote wa upande huo kwako mzuri na muungwana. Mimi sio adui wala mpinzani wako huwa napenda sana haswa unapotoa historia ya Jiji letu la Dar es Salaam (ingawa nimekuwa nasubiri siku utakayosema turudishe jina asili la Jiji hili Mzizima badala hii ya Kiarabu lakini naona hapo sijafanikiwa). Sio siri Mzee au sijui niseme Kakangu we ni hazina, lakini wanasema penye uzuri ndio penye ubaya. Ndugu yangu wewe kasumba ya Kiarabu imekuteka kiasi hujijui kuwa unaukana au hata unaonea sana Uafrika wetu. Kama Muumba ndio huyu aliyetuumba na sisi sioni tatizo kwako kuukubali na kuutukuza Uafrika pia. Huyu Sheikh (RIP) sio namsema vibaya na kusema kweli simjui wala sijawahi kumsikia lakini kwa ushahidi wa kimazingira naweza sema lazima alikuwa mfaidika wa mfumo wa biashara halamu ya utumwa leo naona juu hapo eti Zanzibar ilikuwa na maisha ya utulivu kipindi hicho. Unikalia mabegani we ulie juu kweli una haki ya kusema kila kitu ni shwari na Amani ila mie niliebeba mzigo sijui kama nitaona hali sawa na wewe. Ndugu yangu Mohamed Said hatujui kinachokuja baada ya maisha haya hatujui huko tuendako kama Muumba atakuwa pia anaangalia mambo kama unafiki na udhaifu wa kujikomba komba na kulimbuka na kama atatumia hayo kuuliza mchango wetu basi hebu tuzingatie nini tunafanya hapa kabla ya kuondoka, kwanini tuwe kivuli wakati mwenyezi Mungu katuumba tukiwa kamili. Huyu Sheikh most likely alikuwa slave owner au muhusika wa hali hiyo dhalimu.
 
Unajua Bwana Mohamed Said kutokana na mapenzi yako makubwa ya kila kitu Kiislamu na Uarabu basi kwako yo yote wa upande huo kwako mzuri na muungwana. Mimi sio adui wala mpinzani wako huwa napenda sana haswa unapotoa historia ya Jiji letu la Dar es Salaam (ingawa nimekuwa nasubiri siku utakayosema turudishe jina asili la Jiji hili Mzizima badala hii ya Kiarabu lakini naona hapo sijafanikiwa). Sio siri Mzee au sijui niseme Kakangu we ni hazina, lakini wanasema penye uzuri ndio penye ubaya. Ndugu yangu wewe kasumba ya Kiarabu imekuteka kiasi hujijui kuwa unaukana au hata unaonea sana Uafrika wetu. Kama Muumba ndio huyu aliyetuumba na sisi sioni tatizo kwako kuukubali na kuutukuza Uafrika pia. Huyu Sheikh (RIP) sio namsema vibaya na kusema kweli simjui wala sijawahi kumsikia lakini kwa ushahidi wa kimazingira naweza sema lazima alikuwa mfaidika wa mfumo wa biashara halamu ya utumwa leo naona juu hapo eti Zanzibar ilikuwa na maisha ya utulivu kipindi hicho. Unikalia mabegani we ulie juu kweli una haki ya kusema kila kitu ni shwari na Amani ila mie niliebeba mzigo sijui kama nitaona hali sawa na wewe. Ndugu yangu Mohamed Said hatujui kinachokuja baada ya maisha haya hatujui huko tuendako kama Muumba atakuwa pia anaangalia mambo kama unafiki na udhaifu wa kujikomba komba na kulimbuka na kama atatumia hayo kuuliza mchango wetu basi hebu tuzingatie nini tunafanya hapa kabla ya kuondoka, kwanini tuwe kivuli wakati mwenyezi Mungu katuumba tukiwa kamili. Huyu Sheikh most likely alikuwa slave owner au muhusika wa hali hiyo dhalimu.
Whats your point exactly?
 
Unajua Bwana Mohamed Said kutokana na mapenzi yako makubwa ya kila kitu Kiislamu na Uarabu basi kwako yo yote wa upande huo kwako mzuri na muungwana. Mimi sio adui wala mpinzani wako huwa napenda sana haswa unapotoa historia ya Jiji letu la Dar es Salaam (ingawa nimekuwa nasubiri siku utakayosema turudishe jina asili la Jiji hili Mzizima badala hii ya Kiarabu lakini naona hapo sijafanikiwa). Sio siri Mzee au sijui niseme Kakangu we ni hazina, lakini wanasema penye uzuri ndio penye ubaya. Ndugu yangu wewe kasumba ya Kiarabu imekuteka kiasi hujijui kuwa unaukana au hata unaonea sana Uafrika wetu. Kama Muumba ndio huyu aliyetuumba na sisi sioni tatizo kwako kuukubali na kuutukuza Uafrika pia. Huyu Sheikh (RIP) sio namsema vibaya na kusema kweli simjui wala sijawahi kumsikia lakini kwa ushahidi wa kimazingira naweza sema lazima alikuwa mfaidika wa mfumo wa biashara halamu ya utumwa leo naona juu hapo eti Zanzibar ilikuwa na maisha ya utulivu kipindi hicho. Unikalia mabegani we ulie juu kweli una haki ya kusema kila kitu ni shwari na Amani ila mie niliebeba mzigo sijui kama nitaona hali sawa na wewe. Ndugu yangu Mohamed Said hatujui kinachokuja baada ya maisha haya hatujui huko tuendako kama Muumba atakuwa pia anaangalia mambo kama unafiki na udhaifu wa kujikomba komba na kulimbuka na kama atatumia hayo kuuliza mchango wetu basi hebu tuzingatie nini tunafanya hapa kabla ya kuondoka, kwanini tuwe kivuli wakati mwenyezi Mungu katuumba tukiwa kamili. Huyu Sheikh most likely alikuwa slave owner au muhusika wa hali hiyo dhalimu.

Dunyua,
Kuwa mimi naupenda Uislam wala hujakosea, hakika namshukuru Allah kwa
mimi kuzaliwa Muislam.

Kuwa napenda Uarabu au Waarabu sina sababu ya kuchukia Uarabu wala
kuwachukia Waarabu kama vile siwachukii watu wa makabila mengine.

Sasa tuje katika utulivu wa Zanzibar.

Zanzibar kwa kipindi chote cha Usultani hakuuliwa mtu kwa uonevu wala
hapakuwa na jela za mateso na watu kuuliwa dani ya jela hizo.

Masultani wameondka katika utawala mikono yao haivuji damu.

Inaelekea huijui historia vyema ndiyo ukasema huyu marehemu alikuwa na
watumwa.

Fanya utafiti kidogo upate kujifunza lini utumwa ulipigwa marufuku Zanzibar.
Tubaki katika utumwa na wewe kujifunza historia.

Fanya utafiti lau kidogo ujue utumwa wa Transatlantic Slave Trade na ule
wa Wabelgiji Congo.

Bila ya wewe kuwa na elimu hii hutoweza kijadili haya unayotaka kujadili.
Kuhusu mimi kuukana Uafrika wangu sijui kipi kimekufanya uhisi hivyo.

Huenda hujui lakini mimi nimeandika historia ya wazee wangu vipi walipigania
uhuru wa Tanganyika kuwaondoa Wazungu katika ardhi ya Tanganyika.

Najivunia sana historia hii.
 
Unajua Bwana Mohamed Said kutokana na mapenzi yako makubwa ya kila kitu Kiislamu na Uarabu basi kwako yo yote wa upande huo kwako mzuri na muungwana. Mimi sio adui wala mpinzani wako huwa napenda sana haswa unapotoa historia ya Jiji letu la Dar es Salaam (ingawa nimekuwa nasubiri siku utakayosema turudishe jina asili la Jiji hili Mzizima badala hii ya Kiarabu lakini naona hapo sijafanikiwa). Sio siri Mzee au sijui niseme Kakangu we ni hazina, lakini wanasema penye uzuri ndio penye ubaya. Ndugu yangu wewe kasumba ya Kiarabu imekuteka kiasi hujijui kuwa unaukana au hata unaonea sana Uafrika wetu. Kama Muumba ndio huyu aliyetuumba na sisi sioni tatizo kwako kuukubali na kuutukuza Uafrika pia. Huyu Sheikh (RIP) sio namsema vibaya na kusema kweli simjui wala sijawahi kumsikia lakini kwa ushahidi wa kimazingira naweza sema lazima alikuwa mfaidika wa mfumo wa biashara halamu ya utumwa leo naona juu hapo eti Zanzibar ilikuwa na maisha ya utulivu kipindi hicho. Unikalia mabegani we ulie juu kweli una haki ya kusema kila kitu ni shwari na Amani ila mie niliebeba mzigo sijui kama nitaona hali sawa na wewe. Ndugu yangu Mohamed Said hatujui kinachokuja baada ya maisha haya hatujui huko tuendako kama Muumba atakuwa pia anaangalia mambo kama unafiki na udhaifu wa kujikomba komba na kulimbuka na kama atatumia hayo kuuliza mchango wetu basi hebu tuzingatie nini tunafanya hapa kabla ya kuondoka, kwanini tuwe kivuli wakati mwenyezi Mungu katuumba tukiwa kamili. Huyu Sheikh most likely alikuwa slave owner au muhusika wa hali hiyo dhalimu.
Kabla ya Mapinduzi 1964,Baba yangu alikua na umri wa miaka kama 30 hivi ila hakupata kushuhudia biashara ya utumwa.
 
Back
Top Bottom