Taasisi za Kiislamu zaisafisha CHADEMA

EasyFit

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2011
Posts
1,269
Reaction score
1,082
TAASISI ya Kiislamu ya Islamic Peace Foundation (IPF) kwa kushirikiana na Baraza la Mikutano ya Kiislamu (BATAMIKI), zimesema Chadema si chama cha kidini.

Tamko hilo walilitoa jana kwa vyombo vya habari na kudai kuwa wamefikia uamuzi huo kutokana na dhana waliodai imeenezwa katika jamii ya Watanzania na Waislamu nchini kuwa Chadema ni chama cha kidini.

“Tunatoa mwito kwa Waislamu na Watanzania wote kwa ujumla kuipuuza dhana hii na kuwapuuza wale wanaoieneza ili tuwaunge mkono watu wote wanaotetea maslahi ya wanyonge na rasilimali za taifa letu,” ilieleza sehemu ya taarifa hiyo iliyosainiwa na Mkurugenzi wa IPF, Shehe Sadik Godigodi.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, viongozi wa taasisi hizo baada ya kutafakari dhana hiyo na hatima ya Taifa, wamebaini kuwa hakuna ukweli wowote wa jambo hilo bali ni propaganda.

Taarifa hiyo pia imewataka Watanzania kupuuza propaganda hiyo kwa kile ilichodai kuwa haikuanzia Chadema, bali katika Chama cha Wananchi (CUF).

Shehe Godigodi alidai kuwa CUF ilidaiwa ni ya kikabila na kidini (Uislamu) na kuleta athari kubwa katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2000.

“Hali kama hiyo sasa tunaiona inajitokeza ndani ya Chadema ambacho mwanzo kiliitwa cha kikabila kwa maana ya chama cha Wachaga.

“Lakini baada ya chama hicho kuimarika katika uchaguzi wa mwaka 2010 kama ilivyokuwa kwa CUF, kikabadilishiwa wimbo na kuwa chama cha udini yaani Ukristo,” ilieleza taarifa hiyo.

Viongozi wa taasisi hizo katika taarifa yao hiyo wamedai kuwa udini ndani ya Chadema haupo kwa kuwa chama hicho kama vilivyo vyama vingine kina Waislamu, Wakristo na wasio na dini.

Waliwataka Waislamu kutowabagua wenzao walio katika chama hicho kwa kuwa kufanya hivyo ni kinyume cha matakwa ya dini ya Kiislamu.

HabariLeo:

Inaonekana kuna U turn kwa hawa wenzetu hebu someni tamko lao la mwezi uliopita
 
Ahsante Sheikh GodiGodi, umefunguka baba sasa tusonge mbele daima hadi pale utu wwetu waafrika utakaporudi mikononi mwetu. Propaganda za kidini, kikabila hazina nafasi kwenye nchi zilizoendelea, zinatumiwa kwenye nchi zisizoendelea ili hizi nchi ziendelee kuwa makoloni ya nchi zilizoendelea.

Ni maneno machache lakini ya maana kubwa katika jamii yetu!!
 
Hongerani sana IPF na BATAMIKI sisi tulio pembeni tulikuwa tunawaona mnatumiwa na wasioitakia mema nchi yetu, lakini sasa kwa tamki hili mmeonyesha uwezo wenu wa kutafakari jambo japo mmechelewa sana...

Sitaki nirudie matamko yenu ya nyuma maana nitakuwa natonesha kidonda, leo naomba niakikishiwe tu kama BATAMIKI walikuwa hawatumiwi kisiasa.

Vipi mbona hawakuyasema haya wakati wa uchaguzi mwaka jana na hata wakati wa uchaguzi wa Igunga!!?? Najua mmekaa chini na kuona kwamba siasa za kidini hazitaijenga nchi zaidi ya kuibomoa... Wakristo na Waislamu tuishi kama tulivyokuwa mwanzo.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki CHADEMA.
 
Nafikiri tuwapongeze kwa kufunguka akili si muda mwafaka wa kuanza kuulizana kwanini hawakusema mwaka jana au juzi, ni sawa na mtu aliyeokoka kumuuliza kwanini hakuokoka mwaka jana.
 
Kwa kifupi inapendeza kuyasikia haya maneno kutoka kwa ndugu zetu waislamu, na walaaniwe wale wote wanaoeneza habari za udini wawe wakristo au waislamu kwa maana kamwe udini hautakaa usimame katika taifa hili zaidi ya kutufarakanisha na kutupotezea muda katika kuleta maendeleo na ustawi wa taifa letu sote, njaa haichagui mkristo au muislam, na Mungu aendelee kutuongoza na kutusimamia.
 
Reactions: PhD
Angalau hawa wameliona hili na kujua ukweli upo wapi!
 
kifo cha nyani miti yote huteleza! Tunakaribisha singo mpya kutoka ccm! Tutaipa promo ya kutosha kufunua upumbavu wao!!
 
Ngoja nione Bakwata watasemaje na wao..kwa maana kila mtu akiamka kule atokako na yeye anatoa tamko..
 
Hawa wamenunuliwa kwa pesa ndogo sana ili wafanye propaganda ya kuwadanganya waislam.jana kulikuwa na thred inayosema wamehongwa laki 8 si mmeona?hatudanganyiki ht siku moja.cdm na ukristo na uchaga dam dam
 
Bakwata ni jumuiya ndani ya CCM sii ya waislam!

Cha muhimu waislam tuungane kupambana kuitoa CCM ktk vyama vya siasa nchini kutokana na maovu wayafanyayo.

Jamani ndugu yangu juzi kafariki kwa ajali ya ndege arusha kisha hakuna umeme uwanja wa ndege! Wakasubiri angani mpaka mafuta yakaisha. Mpaka leo sijasikia aliyesababisha uzembe huo kuhojiwa wala kuchukuliwa hatua. Yaani raia kupoteza uhai nchi hii kwa uzembe sio tatizo.
 
hawa wamenunuliwa kwa pesa ndogo sana ili wafanye propaganda ya kuwadanganya waislam.jana kulikuwa na thred inayosema wamehongwa laki 8 si mmeona?hatudanganyiki ht siku moja.cdm na ukristo na uchaga dam dam

itakusaidia au kukuongezea nini ukisema hivyo!chuki unayoipandikiza itaanza kuku cost ktk familia yako!
 
Wanaisafisha au wao ndo wanajisafisha coz wao ndo waliochafuka na udini na kuipendelea CCM, CDM ni wasafi wala hawana udini wala ukabila. Lakin ni vema kama wameona na kujisafisha tunawapa hongera wamejivua gamba na BAKWATA nao watafuata mkondo.
 
Poleni sana ndungu zangu. U are always late like fire brigade!? Moto ukishaanza kuunguza nyumba ndio wanapewa taarifa na hadi wafike, nyumba imeteketea! Ndivyo mlivyotumika Igunga, waliowatumia wameshafanikiwa, nyie ndio mnashtuka.
Ninachoweza kuwaambia kwa sasa ni kuwakaribisha tena kwenye mapambano ya kuikomboa nchi huku mkiangalia mbele kwa makini ili msitumike tena kijingajinga na kuturudisha nyuma.

Mungu ibariki Tanzania na watu wake (waislamu, wakristo, wapagani, makabila yote na wa kanda zote)!
 
itakusaidia au kukuongezea nini ukisema hivyo!chuki unayoipandikiza itaanza kuku cost ktk familia yako!
hiyo ile thread ya hongo ya laki nane nayo ni propaganda. Tusubiri tutaona ukweli , lisemwalo lipo na kama halipo laja. Acha Mbowe mwenyewe akanushe au wewe ndo msemaji wa CDM?
 
Hawa wamenunuliwa kwa pesa ndogo sana ili wafanye propaganda ya kuwadanganya waislam.jana kulikuwa na thred inayosema wamehongwa laki 8 si mmeona?hatudanganyiki ht siku moja.cdm na ukristo na uchaga dam dam
Kwani nyie huwa mnatoa ngapi kwa Bakwata.
 
Who is GODIGODI? ama kweli njaa noma. Fafanua sasa kuhusu Mkuu wa Wilaya ya Igunga alidhalilishwa au la! Waislamu watakusaka uwaeleze mlikubaliana na nani kutoa tamko kama hilo?
 
Hawa wamenunuliwa kwa pesa ndogo sana ili wafanye propaganda ya kuwadanganya waislam.jana kulikuwa na thred inayosema wamehongwa laki 8 si mmeona?hatudanganyiki ht siku moja.cdm na ukristo na uchaga dam dam
Hata kwenye kundi la wajinga, kuna mjinga kuliko wenzake! Wenye akili hatuwezi kukushangaa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…