Phd Hewa
JF-Expert Member
- Oct 3, 2016
- 572
- 466
kituo kikubwa cha habari Kenya cha Citizen kimeripoti kupotea kwa Rais wa Malawi, Peter Mutharika ambae hajarudi nchini kwake tangu alivyoondoka kuelekea New York Marekani kwenye mkutani mkubwa wa Umoja wa Mataifa kwa mujibu wa rekodi imetajwa kuwa aliondoka nchini New york, September 15 2016 na mpaka sasahivi hajawasili nchini kwake Malawi.
Rais Mutharika amepotea kwa muda wa wiki 3 tangu sasa aondoke nchini kwake na imepelekea raia wa nchi hiyo kuweka hashtags kwenye mitandao ya kijamii zikisema [HASHTAG]#bringbackMutharika[/HASHTAG] haswa kwenye twitter kama unavyoona hapo chini.
