Taarifa ya kukosekana umeme


Na mwisho wa mwezi wanakata service charge ingawa umeme wenyewe haupo
 

Baadhi ya maeneo yataendelea kukosa umeme hadi lini? Toeni basi angalau taarifa inayojitosheleza, hii mbona imekaa kimtego mno? Maana hatujui lini sasa hili tatizo litaisha... nawachukia sana Tanesco na serikali yenu ya ccm. Mabadiliko ni Oct 25.
 
Ni ili ikifika 25 oktoba usione muujiza kukosa umeme. Sijui mnaotaka kulinda kura mtazionaje?
 
Nahisi kuna hujuma hapa!
Hii wizara aliyekuwa anaimudu ni Muhongo!
Angalau kukatika katika kwa umeme kulipungua ukilinganisha na kipindi hiki na hata ukilinganisha na kabla ya yeye kuwa waziri!!
 

Ndo hicho ccm mmezoea kuwaaminisha watu kwamba hakuna kinachowezekana kufanyika na tatizo lake likawa historia....angalia maji ni tatizo, huduma za afya ni kero, madawati shuleni ni tatizo, barabara mbovu, shilingi imeshuka thamani....yaani kwa ujumla hivyo ndivyo ccm wametufikisha hapo kwamba hakuna kinachoweza fanyika au kufanywa na tatizo lake likawa hostoria...lakini mnaweza kufanya vitu vya anasa kama kununua mashangingi, rais kuishi nnje ya inchi kwa miaka mitano, rushwa, ufisadi, mikataba mibovu, kununua vitu feki/chakavu kama mabehewa ya treni.....
 
Asante.......
Jioni wapi tupate hata kinywaji baridi tuondoe hili joto........

Kinywaji baridi kinapatikana wapi wakati umeme hakuna? kwetu ulikatika tangu usiku wa manane,asubuhi ulirudi kidogo ambao hata kuwasha bulbu haitoi mwanga baada ya muda ukakata tena.Inaboa sana.
 
Pelekeni huko umeme ul ikatwa tangia jana Oct 2.
 
Kinywaji baridi kinapatikana wapi wakati umeme hakuna? kwetu ulikatika tangu usiku wa manane,asubuhi ulirudi kidogo ambao hata kuwasha bulbu haitoi mwanga baada ya muda ukakata tena.Inaboa sana.

Njoo hapa Calabash uone kama vinywaji havijapoa.............
 
It is indirectly a matter of who is in power......
 
nahisi kuna hujuma hapa!
Hii wizara aliyekuwa anaimudu ni muhongo!
Angalau kukatika katika kwa umeme kulipungua ukilinganisha na kipindi hiki na hata ukilinganisha na kabla ya yeye kuwa waziri!!

we inaonekana bado umeme ulikuwa haujafika huko kwenu kipindi hicho! Shirika la tanesco linawadai serikali hela, tanesco hawana hela ya kujiendesha
 
Kama sisi ni wateja kama mnavyotuita kwanini tunaponunua umeme wa luku mnatukata asilimia tatu mnapeleka ewura na asilimia moja rea? Kwanini mnatuuzia nguzo na vifaa vingine kisha mnavitumia kuunganishia wateja wengine na kuongeza kipato kwa shirika lenu,huu sio wizi,fanyeni mtoe fidia kwa mliowafanyia hivyo
 
Tanesco ni ile ile, stori ni zile zile
 
Hiyo ni leo....
Lakini pia baada ya kushughulikiwa kwa hitilafu........umeme hakuna.......hata jana kabla ya hitilafu.....juzi.....juzi ile.......umeme haukuwepo pia............

...una maswali magumu sana,hebu tafuta mengine.?!
 
Tanesco wamesahau kuwa uongo wao una mwisho. Waseme tu kuwa uzalishaji ni mdogo umeme ni kidogo haukidhi tena mahitaji ya nchi nzima .Tanesco haina hata uwezo wa ku cover operation cost kwa kupitia mapato yao. Ndio maana unit ya umeme itapanda siku hadi siku.
 
eti mitambo inawashwa,wapi bana,,,,hiyo mitambo ya aina gani wanawasha mwezi mzima?,mbona hata mitambo ya nyuklia haichukui mda wote huop kuwaka?

Sasa mbona bado unaendelea kuishabikia ccm ilhali unaona kero kama hizi za umeme zimetuchosha na hawajaweza kufanya kitu mpaka sasa!
 

...hii taarifa ya kinafiki tu kutoka Tanesco.Kwa nini.?
..Mnasema umeme ulikatika leo alfajiri sababu ya hitilafu iliyotokea hayo maeneo mliyotaja,fine.
At the same time mnasema tena;
...Hata hivyo umeme utaendelea kukosekana sababu ya upungufu wa uzalishaji umeme kwenye vyanzo vya maji...
Sasa tuwaelewe vipi.?!
Kwamba;hata kama pasingekuwepo na hiyo hitilafu,ni wazi bado umeme ungekatika tu.Kwanini nyie watu msikubali wazi kuna mgao wa umeme kuliko kuendelea kuchengana kama watoto.?!
Hii taarifa yenu ni fake,yaani inabembea bembea tu,ni heri mngekaa kimya mtuache tufikirie sababu zetu wenyewe,mlichofanya ni kutuongezea maswali vichwani yasiyo na maana.
#tired!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…