1000 digits
JF-Expert Member
- Oct 16, 2012
- 7,802
- 10,304
Kwa kweli haipendezi kuona taifa hili likijengwa kwa kodi za wote lakini wanaofaidi ni kakundi kadogo ka viongozi ndani ya CCM na marafiki zao tu.
Sio sawa kuwakataza wapinzani wasihiloji wala kuwaambia watanzania juu ya matumizi na mwenendo wa kodi za watu mil. 6 waliowapigia kura. CCM ina haki ya kuwapa taarifa wapiga kura wao mil. 8 juu ya maendeleo yanayotokana na kodi zao halikadhalika wapinzani nao wanahaki ya kukosoa juu ya matumizi ya kodi zao
Pamoja na kwamba sera zinazotekelezwa ni za CCM lakini kodi hawatoi wao wenyewe na kwa uzoefu maCCM wengi ndio wakwepa kodi na wala kodi inayotoka kwa asilimia kubwa kutikana na kushika ajira zote nono serikalini.
Haki ni vizuri ikawa sawa kwa vyama vyote sio kwa CCM wenyewe.
Nadhani ingekuwa vyema jeshi la polisi likaachana na mambo ya wanasiasa wanaokosoana kwa hoja.Kwa sababu hapakua na haja ya kutafuta taarifa za kiintelijensia kwa ajili kujua kuwa kuna vyama vitakwenda Dodoma kuzuia mkutano wa CCM kwani CDM walitangaza hadharani bila kificho na mimi nikategemea kuwa mkutano huo utaahirishwa kutokana na taarifa hizo zinazoweza kusababisha uvunjifu wa amani. Nadala yake Polisi wameimarisha ulizi ,jambo ambalo ni sahihi na ndilo lilokuwa linatakiwa kufanyika hata kwenye mikutano ya uponzani.
Kinachotakiwa ni kuimarisha ulinzi na sio kupiga marufuku mikutano ya kisiasa.
Sio sawa kuwakataza wapinzani wasihiloji wala kuwaambia watanzania juu ya matumizi na mwenendo wa kodi za watu mil. 6 waliowapigia kura. CCM ina haki ya kuwapa taarifa wapiga kura wao mil. 8 juu ya maendeleo yanayotokana na kodi zao halikadhalika wapinzani nao wanahaki ya kukosoa juu ya matumizi ya kodi zao
Pamoja na kwamba sera zinazotekelezwa ni za CCM lakini kodi hawatoi wao wenyewe na kwa uzoefu maCCM wengi ndio wakwepa kodi na wala kodi inayotoka kwa asilimia kubwa kutikana na kushika ajira zote nono serikalini.
Haki ni vizuri ikawa sawa kwa vyama vyote sio kwa CCM wenyewe.
Nadhani ingekuwa vyema jeshi la polisi likaachana na mambo ya wanasiasa wanaokosoana kwa hoja.Kwa sababu hapakua na haja ya kutafuta taarifa za kiintelijensia kwa ajili kujua kuwa kuna vyama vitakwenda Dodoma kuzuia mkutano wa CCM kwani CDM walitangaza hadharani bila kificho na mimi nikategemea kuwa mkutano huo utaahirishwa kutokana na taarifa hizo zinazoweza kusababisha uvunjifu wa amani. Nadala yake Polisi wameimarisha ulizi ,jambo ambalo ni sahihi na ndilo lilokuwa linatakiwa kufanyika hata kwenye mikutano ya uponzani.
Kinachotakiwa ni kuimarisha ulinzi na sio kupiga marufuku mikutano ya kisiasa.