Taarifa: Polisi wakamata bunduki aina ya SMG na jumla ya risasi 59

eyetyna

Senior Member
Jun 24, 2011
148
17
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linawashikilia watu saba kwa tuhuma za kujihusisha na matukio ya uhalifu ikiwa ni pamoja na unyang'anyi wa kutumia silaha. Watuhumiwa wamekamakwa katika matukio tofauti jijini Dar es Salaam kufuatia oparesheni kali inayoendelea ya kuwasaka wahalifu wa makosa mbalimbali.

Katika tukio la kwanza mnamo tarehe 03/06/2015 majira saa 08:00HRS maeneo ya Tabata Kinyerezi mtaa wa Kibaga askari wa kikosi kazi (TASK FORCE) walimkamata mtuhumiwa HEMED S/O HASSAN MRISHO @ BUDA, Miaka 31, Mfanyabiashara, Mkazi wa Tabata Kinyerezi, akiwa na Bunduki aina ya SMG iliyofutwa namba zake ikiwa na risasi 10. Mtuhumiwa alikamatwa kufuatia taarifa toka kwa msiri kuwa anajihusisha na uhalifu wa kutumia silaha.

Uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa mtuhumiwa HEMED S/O HASSANI akishirikiana na wenzake ambao wanasakwa, wanajihusisha na unalifu wa kutumia silaha. Atafikishwa mahakamani mara uchunguzi utakapokamilika.


unnamed%2B%252890%2529.jpg

Naibu Kamishna wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam (DCP), Simon Sirro akiwaonesha
baadhi ya waandishi wa habari (hawapo pichan) Bunduki aina ya (SMG) iliyofutwa namba zake ikiwa na risasi 10.

Katika tukio lingine, mnamo tarehe 01/06/2015 majira ya saa 02:00 huko maeneo ya Tegeta Mashimo ya Kokoto, Polisi walifanikiwa kukamata risasi 49 za bunduki aina ya Short Gun zikiwa katika mfuko wa Rambo baada ya kuwakurupua vijana wanaokaa katika vijiwe vya mashimoni hayo.


Hii ni kufuatia kundi la vijana wanaokadiriwa kufikia kumi wakiwa na mapanga na silaha nyingine za jadi kuvamia nyumba ya VERONICA D/O SABATH MAMBOYA na kuiba vitu mbalimbali vikiwemo vitambulisho, TV, Laptop na Pesa taslim TSHS. 300,000/=. Baada ya tukio mlalamikaji alitoa taarifa kituo cha polisi Kawe na ufuatiliaji ulianza mara moja. Polisi walifanikiwa kuwakamata vijana watatu ambao walionyesha vijiwe vya vijana wenzao.

unnamed%2B%252888%2529.jpg

Naibu Kamishna wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam (DCP), Simon Sirro akiwaonesha risasi
zilizokamatwa katika oparesheni hiyo.

Wakati polisi wakijiandaa kuwakamata walikurupuka na kukimbia ndipo polisi walifanya upekuzi wa eneo hili na kufanikiwa kupata risasi hizo zikiwa katika mfuko wa plastiki maarufu kama "mfuko wa Rambo". Watuhumiwa waliokamatwa ni pamoja na;

1. RAMADHANI S/O NUHU, Miaka 20, Mkazi wa Kiwangwa.
2. ABED S/O SALUM, Miaka 18, MKAZi wa Kibaoni.
3. HANIF S/O HAMIS, Miaka 19, MKAzi wa Tegeta.

unnamed%2B%252889%2529.jpg

Naibu Kamishna wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam (DCP), Simon Sirro Sirro akiwaonesha
baadhi ya waandishi wa habali hawapo pichan Bembe za Ndovu zilizo kamatwa maeneo ya Kimara Suka
katika oparesheni ukaguzi wa magari.

KUKAMATWA KWA ROLA 15 ZA NYAYA ZA UMEME PAMOJA NA WATUHUMIWA SABA.

Katika hatua nyingine Jeshi la Polisi Kanda Maalum limefanikiwa kukamata kontena lenye namba 00LU2876031 likiwa na rola 15 za nyaya (zenye thamani ya shilingi 150,000,000/= milioni mia moja na hamsini) zilizoibwa tarehe 26/02/2015 zikiwa zinasafirishwa kuelekea mkoani Kagera kwa ajili ya mradi wa umeme vijijini (REA). Baada ya wizi wa kontena hilo kesi ilifunguliwa kituo cha Polisi Buguruni na watuhumiwa watano walikamatwa na kufikishwa mahakamani.

Wakati upelelezi ukiendelea ndipo tarehe 25/05/2015 Polisi Buguruni walipokea taarifa toka kwa msiri kwamba huko maeneo ya Kibamba mtaa wa Kibwegele wilaya ya Kimara Mkoa wa Kipolisi Kinondoni kuna kontena limefichwa katika kiwanda cha kutengeneza matofali.

Askari wa kikosi kazi walifika eneo la tukio na kukuta kontena hilo lenye namba 00LU2876031 na walimhoji mlinzi wa eneo ili kupata mmiliki wa eneo na kontena hilo. Ilipofika saa 23:55hrs mmiliki wa eneo hilo aitwaye DONESIA D/O AIDAN @ KIFYOGA, Miaka 40, Mfanyabiashara, Mkazi wa Mbezi Makabe ambaye ni mtuhumiwa wa sita.

Taratibu zilipokamilika kontena hilo lilifunguliwa ndipo zilipokutwa rolla za nyaya zipatazo 15 kati ya 17 zilizokuwepo katika kontena hilo siku lilipokuwa linasafirishwa. Tarehe 27/05/2015 majira ya saa 00:30hrs maeneo ya Kimara mwisho alikamatwa mtuhumiwa mwingine wa saba PROSPER S/O MTEI, Miaka 43, Mfanyabiashara na upelelezi unaendelea ili aweze kuunganishwa na watuhumiwa wengine katika kesi ya msingi.

KUKAMATWA KWA BASTOLA MOJA NA MAGANDA YA RISASI
Mnamo tarehe 28/05/2015 majira ya saa 23:00hrs maeneo ya Kiwalani Minazi Mirefu Kata ya Ilala WIlaya ya Ilala jijini Dar es Salaam, Polisi walifanikiwa kukamata silaha Bastola yenye nambari 05532 pamoja na maganda mawili ya risasi aina ya SMG katika eneo la tukio baada ya majambazi kuitelekeza mara walipozingirwa na wananchi waliotaka kuwakamata.

Majambazi hao walikuwa wamefanya tukio la uporaji maeneo ya vingunguti wakitumia pikipiki mbili ambapo moja ina namba za usajili MC610 ABU aina ya Boxer rangi nyekundu ambayo pia waliipora kwa mtoa taarifa.

Aidha katika tukio hilo pia majambazi hao walimpiga mtoa taarifa na kitako cha bunduki waliyokuwa nayo kisha kumpora pikipiki hiyo na pesa taslim shilingi 300,000/= Hata hivyo majambazi hao walifanikiwa kutoroka. Polisi kwa kushirikiana na wananchi waliweza kuikamata pikipiki hiyo.


KUKAMATWA KWA VIPANDE 20 VYA PEMBE ZA NDOVU.
Katika oparesheni iliyoendeshwa tarehe 25/05/2015 na idara ya INTERPOL jijini Dar es Salaam ya kukamata magari, madawa ya kulevya na uhalifu mwingine. Ilipofika majira ya saa 18:00hrs maeneo ya Kimara Suka ambapo kutokana na foleni ya magari iliyosababishwa na ukaguzi wa magari katika zoezi hilo alishuka kijana mmoja mwenye umri kati ya miaka 39- 45 kwa dhumuni la kukodi pikipiki.

Katika hali isiyokuwa ya kawaida baada ya kuwaona askari wa unifomu kijana huyo alitupa kifurushi alichokuwa nacho na kukimbia. Askari walilichukua hilo furushi na kulipekuwa na kukuta kuna meno ya tembo vipande ishirini pamoja na nguo kuku. Kielelezo kilipelekwa kituo cha Polisi Mbezi na kufunguliwa jalada la uchunguzi KMR/PE/67/2015.

KUKAMATWA KWA MLIPUKO, VIFAA VYA KUVUNJIA, DAWA ZA KULEVYA PAMOJA NA MTUHUMIWA.
Tarehe 04/06/2015 majira ya saa 10:00hrs maeneo ya Chamazi ulifanyika msako mkali wa kupambana na uhalifu na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa MICHAEL S/O KASAMBALE, Miaka 28, Mkazi wa Chamazi akiwa na mlipuko mmoja na vifaa vya kuvunjia. Mtuhumiwa atafikishwa mahakamani upelelezi utakapokamilika. Aidha mtuhumiwa huyo amekamatwa na kete kadhaa za madawa ya kulevya.

KUKAMATWA KWA MTUHUMIWA AKIWA NA BASTOLA BANDIA
Polisi wamefanikiwa kuwakamata watuhumiwa JACOB S/O NATHANIEL MWETA, Miaka 30, Mfanyabiashara, Mkazi wa Kimara ambaye alikuwa anaitumia kutishia watu kisha kupora. Mtuhumiwa ame kiri kuhusika katika matukio kadhaa ya unyang'anyi hasa katika maeneo ya Tegeta na Kunduchi jijini Dar es Salaam.

MAFANIKIO MENGINE YA OPARESHENI INAYOENDELEA JIJINI DAR ES SALAAM.
Aidha, Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam linaendelea na oparesheni ya kupambana na uhalifu katika jiji la Dar es Salaam na kufanikiwa kukamata vitu vifuatavyo:

1. Mitambo mitano (5) ya kutengeneza pombe ya moshi (Gongo)
2. JUmla ya lita mia mbili (200) za pombe ya Moshi (Gongo)
3. Gunia mbili za banghi.
4. Kupatikana na Mirungi box moja (1).
5. Kete kadhaa za madawa ya kulevya.

SIMON SIRRO – DCP
KNY. KAMISHNA WA POLISI KANDA MAALUM
DAR ES SALAAM

Chanzo: Michuzi

 
Nilidhani AK 47 kumbe hizo toy...........wako pamoja hao labda wamepunjana mgawo tu ndo mana.
 
Nilidhani AK 47 kumbe hizo toy...........wako pamoja hao labda wamepunjana mgawo tu ndo mana.

Majitu mengine mnakera sana, we unadhani ukishaitwa mpinzani basi we ni kupinga tu kila kitu, hata maswala ya kukabiliana na ujambazi we unapinga tu! Kweli nimeamini, ukiwa mfuasi wa Chadema akili zako zinakua sawa na nyumbu!
 
Majitu mengine mnakera sana, we unadhani ukishaitwa mpinzani hata maswala ya kukabiliana na ujambazi we unapinga tu! Kweli mfuasi wa Chadema akili sawa na nyumbu!

Akili za nyumbu,haya......kilichopingwa ni nini apo?.
 
Kuna kitu ambacho sijakielewa ukigoogle AK47 picha inayokuja inafanana na hiyo bunduki ya smg sasa nini tofauti ya SMG na AK47?
 
Huwa nashangaa sana haya matukio,zinapokuwa zimekamatwa silaha watuhumiwa huwa hawaonyeshwi,zinaonyeshwa silaha tu.huwa nina wasiwasi pengine huwa zinachukuliwa ghalani na stori zinaundwa ili kuonyesha kuwa watu wako macho kikazi.
 
Kuna kitu ambacho sijakielewa ukigoogle AK47 picha inayokuja inafanana na hiyo bunduki ya smg sasa nini tofauti ya SMG na AK47?

SMG ni generic term na AK 47 ni specific name! Yaani ndani ya SMG (Sub Machine Gun) Ndimo kuna AK 47, G3, uzz gun, HK MP5, HK UMP, et al et al et al...


Huwa nashangaa sana haya matukio,zinapokuwa zimekamatwa silaha watuhumiwa huwa hawaonyeshwi,zinaonyeshwa silaha tu.huwa nina wasiwasi pengine huwa zinachukuliwa ghalani na stori zinaundwa ili kuonyesha kuwa watu wako macho kikazi.

Nadhani sababu ni kubwa zaidi ya uliyoitaja! Labda kwa ajili ya upepelezi unaoendelea.
 
Majitu mengine mnakera sana, we unadhani ukishaitwa mpinzani basi we ni kupinga tu kila kitu, hata maswala ya kukabiliana na ujambazi we unapinga tu! Kweli nimeamini, ukiwa mfuasi wa Chadema akili zako zinakua sawa na nyumbu!

Ha,ha,ha,haaa...hii kali
 
Back
Top Bottom