Taarifa kutoka Uhamiaji

Taarifa kutoka Uhamiaji

karibukwetusingida

JF-Expert Member
Joined
Mar 10, 2014
Posts
290
Reaction score
138
Baadhi ya vyombo vya habari leotarehe 29 julai, 2014 vimeandikakwa makosa kuwa ajira za uhamiajizilizositishwa jana zinahusiana na70 zilizopatikana baada ya usailiuliofanyika katika uwanja wa taifa.

Ukweli ni kuwa usaili wa nafasi ya mkaguzi msaidizi wa uhamiaji ambao awali ulianzia uwanja wa taifa ulienda vizuri hadi wakapatikana wasailiwa wa kujaza nafasi 70 za mkaguzi msaidizi wa uhamiaji.

Zoezi hilo halikuwa na matatizo yoyote, na waliochaguliwa walitakiwa kuripoti kazini tarehe 29 julai lakini kwa sababu ya sikukuu sasa wataripoti baada ya sikukuu.

Hivyo tunapenda kufafanua kuwa wasailiwa waliochaguliwa kujaz anafasi 70 za mkaguzi msaidizi wa uhamiaji hawahusiki na usitishwaji uliotangazwa jana na wanatakiwa kuendelea na mipango ya kuripoti kazini kama ilivyotangazwa hapo awali.

Wasailiwa wanaohusika nakusitishwa kwa ajira zao ni wale waliokuwa wameshiriki katika zoezi la kuajiri konstebo na koplo wa uhamiaji ambao idadi yao ni 200,ambao walitakiwa kuripoti tarehe 06 agosti, 2014 lakini kwa sasa hawa ndio wanaelekezwa wasubiri hadi hapo watakapopewa maelekezo mengine.

Sgnisaac J. Nantanga

Msemaji wa wizara ya mambo ya ndani ya nchi, 29 Julai, 2014
 
ila msirudie tena ile tabia ya kuita watu elf kumi na mia nane kwa nafasi sabini tu
 
Baadhi ya Vyombo vya Habari leo
tarehe 29 Julai, 2014 vimeandika
kwa makosa kuwa ajira za Uhamiaji
zilizositishwa jana zinahusiana na
70 zilizopatikana baada ya usaili
uliofanyika katika Uwanja wa Taifa.
Ukweli ni kuwa usaili wa nafasi ya
Mkaguzi Msaidizi wa Uhamiaji
ambao awali ulianzia Uwanja wa
Taifa ulienda vizuri hadi
wakapatikana wasailiwa wa kujaza
nafasi 70 za Mkaguzi Msaidizi wa
Uhamiaji. Zoezi hilo halikuwa na
matatizo yoyote, na waliochaguliwa
walitakiwa kuripoti kazini tarehe 29
Julai lakini kwa sababu ya Sikukuu
sasa wataripoti baada ya sikukuu.
Hivyo tunapenda kufafanua kuwa
wasailiwa waliochaguliwa kujaza
nafasi 70 za Mkaguzi Msaidizi wa
Uhamiaji hawahusiki na usitishwaji
uliotangazwa jana na wanatakiwa
kuendelea na mipango ya kuripoti
kazini kama ilivyotangazwa hapo
awali.
Wasailiwa wanaohusika na
kusitishwa kwa ajira zao ni wale
waliokuwa wameshiriki katika zoezi
la kuajiri Konstebo na Koplo wa
Uhamiaji ambao idadi yao ni 200,
ambao walitakiwa kuripoti tarehe
06 Agosti, 2014 lakini kwa sasa
hawa ndio wanaelekezwa wasubiri
hadi hapo watakapopewa
maelekezo mengine.
Sgn
Isaac J. Nantanga
MSEMAJI WA WIZARA YA MAMBO
YA NDANI YA NCHI
29 JULAI, 2014

Sio kwamba hakuna tatzo, tatzo lipo na ni kubwa sema mnataka kujisafisha wakat katib ana watu wake ktk 70
Achen siasa wehu nyie
 
Yana matatizo, mkasome gazeti la Jamuhuri tarehe 29/07/2014! Yarudiwe yote! Tuanze upya tuone kama wale mliowaita watashinda tena!
 
Hapo hakuna suluhisho me naona tatizo lipo palepale tutazidi kupokea wahamiaji haramu kwa kwenda mbele kwa kuwa utendaji mbovu wa kuitana kindugu pamoja na rushwa ya kuwaita wasio na sifa na kuwaacha wenye sifa katika ule usaili wa mkaguzi msaidizi bado undugu pamoja na rushwa zilifanyika hivyo basi serikali ichukue uwamuzi wa kusitisha nafasi zote za kazi uhamiaji walizotangaza....... OVER
 
​kwa mtu mwenye busara na akili japo ndogo tu,huwa anakuwa na tabia ya kuhisi aibu hasa pale linapozuka suala ama jambo lolote lililo na chembechembe za uhuni, upendeleo na hata dhuluma, na bahati mbaya sana huyo mtu akagundulika na kudhibitika kuhusika kwenye tuhuma hizo zinazomsibu.

Hawa ndugu zetu kiukweli walitumia akili kuokoa familia zao lakini tu walikosea katika kufanya sampling ambayo ndiyo ilitibua mambo mara tu baada ya wazalendo na wenye machungu na nchi yao kuligundua hilo na kuamua kulivalia njuga, mpaka pale mambo yalivyokuwa kama yalivyo; nampongeza sana aliyelifanya hilo.

Lakini vilevile kwa mtazamo wa kawaida tu usiohitaji degree yeyote ile, huenda hata hawa walioko kwenye idara ya Utumishi nao wameoza kimaadili, kwa sababu haiwezekani na wao waruhusu itokee kama ilivyotokea ni hujuma na kutokutumia AKILI katika kufanya mambo yao, kwa hiyo kwa ufupi tu ni kwamba; nao pia HAWAFAI KABISA.

Hebu chukulia mfano tu kwamba ni michakato mingapi hawa watu wameziendesha mpaka sasa na mpaka kufikia kukamatwa ni dhahiri kabisa kwamba huu UHUNI wa aina hii ulianza zamani yaani "

Mtoto wa mtanzania Kabwela aliyesoma kwa mkopo, mkopo ambao pia kila kukicha matangazo yanayosisitiza kurejeshwa kwake hayakatiki kwenye vyombo vya habari, hata kufikia kutaka kuzuiwa kwa utoaji wa VIZA kwa hawa Makabwela ambao hasa ndio walengwa kwa sababu ni wao ndio hawataweza kuurejesha huo mkopo, na istoshe wanatambua wazi kwamba HAWA watanzania makabwela hawajapata ajira kwa sababu hawana mtu wa kuwashika mkono.

Wao utawasikia kwenye vyombo vya habari walivyo na moyo wa kusisitiza vijana kujiajiri,wasitegemee kuajiriwa Hebu muulize yeye anayesema hivyo kama mtoto wake amejiajiri?na kama amejiajiri tayari si kwao pesa zipo?

Je huyu Kabwela yeye atatoa wapi mtaji huo wa kujiajiri? Na wengine watasema kuwa MAKABWELA tukakope pesa benki pale ambapo wanatambua hakika kuwa huyu KABWELA mimi siwezi kutimiza vigezo.

Wamebana kila kona hatuna pa kupumulia, Hajira zikitoka wanazikwapua zote, serikali ikitoa mtaji vigezo lundo ili tushindwe,HIVI huyu mtoto wa maskini anapoangaika kutoka MASUMBWE tena kwa basi lenye hadhi ya daraja la TATU siyo kwa sababu hakuyaona hayo yenye hadhi nzuri ama LUXURY zinaitwa, La hasha! lakini ni kwa sababu tu, hana uwezo huyo.

Huyu Mzalendo kabwela anapakia gari kutoka kijijini kwao BUZIMBWE huko Bunda mkoani Mara, ambaye pia hana ndugu wala pa kufikia Dar es salaam anakoitwa kwenye usaili unaochukua takribani siku kadhaa, WAO wakitambua kuwa huyu mtu anapata mateso na manyanyaso makubwa, wanaendelea kumzungusha ili aendelee kupoteza siku DAR ili awakingie kifua watoto wa vibosile ionekane kwamba usaili ulikuwa wa h- yaani hawa ndio watanzania halisi ambao majina yao yanapitishwa kwa MEMO nitakwambia maana ya memo baadaye.

Ninayo mambo mengi ya kuwaambia watanzania wenzangu lakini kwa sababu hayaishi nadhani nitafungua jarida maalumu kwa ajili ya kutoa elimu japo ya USTAARABU kwa HAO wanaojiita WATANZANIA HALISI ili waweze kuwajali hata hawa ndugu wakambo WAZALENDO MAKABWELA japo kwa likombe cha kahawa.
 
Mungu atajibu kwa moto ,watachuma lakini hawatakula,watakusanya wengine watatawanya,Ghadaffi,Saddam etc wako wapi na makusanyo yao?
Sihukumu lakini kwa neno la msalaba wajifunze
 
MSAADAA..!!!hivi hawa 70 walishafanyiwa vipimo tayari vya tayari??!
 
Give the devil his due, kwa usaili wa mkaguzi msaidizi uhamiaji walijitahidi kutenda haki kwa kiasi kikubwa na hata kama kulikuwa na kasoro basi ni za kibinadamu because no one is perfect under the sun and bias is inherent to humman being lakini kwa nafasi ya koplo na konstebo the process was made under nepotism,hivyo basi katibu kusimamisha mchakato huo ni jambo jema na anastahili pongezi
Pili kwa kuwa katibu ameshafanya maamuzi ya kuunda kamati ya uchunguzi,basi sisi watanzania tujikite kwenye kuibua hoja zitakazosaidia kubainisha ukweli badala ya kuongea mambo kwa hisia basi tujitahidi kwenda kwa fact,eti unakuta mtu anaandika afisa utumishi hafai au na wale 70 wafutwe bila kuweka arguments za kwanini iwe hivo,jambo ambalo ukiangalia utagundua wengine wana hasira za kukosa kazi.Tujifunze kwa yule aliyeainisha majina ya waliochaguliwa nafasi ya koplo na konstebo wanavyohusiana na watumishi wa uhamiaji,tuanzie hapo
 
Sio kwamba hakuna tatzo, tatzo lipo na ni kubwa sema mnataka kujisafisha wakat katib ana watu wake ktk 70
Achen siasa wehu nyie

nani mwehu sasa hapa... nenda ofisini kwao ukawaambie...
 
Give the devil his due, kwa usaili wa mkaguzi msaidizi uhamiaji walijitahidi kutenda haki kwa kiasi kikubwa na hata kama kulikuwa na kasoro basi ni za kibinadamu because no one is perfect under the sun and bias is inherent to humman being lakini kwa nafasi ya koplo na konstebo the process was made under nepotism,hivyo basi katibu kusimamisha mchakato huo ni jambo jema na anastahili pongezi
Pili kwa kuwa katibu ameshafanya maamuzi ya kuunda kamati ya uchunguzi,basi sisi watanzania tujikite kwenye kuibua hoja zitakazosaidia kubainisha ukweli badala ya kuongea mambo kwa hisia basi tujitahidi kwenda kwa fact,eti unakuta mtu anaandika afisa utumishi hafai au na wale 70 wafutwe bila kuweka arguments za kwanini iwe hivo,jambo ambalo ukiangalia utagundua wengine wana hasira za kukosa kazi.Tujifunze kwa yule aliyeainisha majina ya waliochaguliwa nafasi ya koplo na konstebo wanavyohusiana na watumishi wa uhamiaji,tuanzie hapo

"UCHUNGUZI" naufananisha na 'daktari anamfanyia operation mgonjwa, mgonjwa anafia kwenye kitanda cha upasuaji, daktari huyo huyo ndio anaandika hati ya kifo'

Kwa kuwa tuna watanzania wengi zaidi kuliko nafasi za kazi, tutengeneze registry ya wataaluma, ikitokea nafasi za kazi wataaluma husika wanaotaka hiyo kazi wanalipia ada online, inachezeshwa open lottery, wanapatikana wataaluma wanaajiriwa, tutaangalia utendaji wao kwenye kipindi cha probation. KWISHA MZIZI WA UPENDELEO.
 
Kwanini wasikubali kushindwa, hafu zoezi zima la kuwania hizo nafasi likaanza na upya?
 
"UCHUNGUZI" naufananisha na 'daktari anamfanyia operation mgonjwa, mgonjwa anafia kwenye kitanda cha upasuaji, daktari huyo huyo ndio anaandika hati ya kifo'

Kwa kuwa tuna watanzania wengi zaidi kuliko nafasi za kazi, tutengeneze registry ya wataaluma, ikitokea nafasi za kazi wataaluma husika wanaotaka hiyo kazi wanalipia ada online, inachezeshwa open lottery, wanapatikana wataaluma wanaajiriwa, tutaangalia utendaji wao kwenye kipindi cha probation. KWISHA MZIZI WA UPENDELEO.

Mfumo wa bahati nasibu ya kazi umewahi kutumika duniani?
 
Baadhi ya Vyombo vya Habari leo
tarehe 29 Julai, 2014 vimeandika
kwa makosa kuwa ajira za Uhamiaji
zilizositishwa jana zinahusiana na
70 zilizopatikana baada ya usaili
uliofanyika katika Uwanja wa Taifa.
Ukweli ni kuwa usaili wa nafasi ya
Mkaguzi Msaidizi wa Uhamiaji
ambao awali ulianzia Uwanja wa
Taifa ulienda vizuri hadi
wakapatikana wasailiwa wa kujaza
nafasi 70 za Mkaguzi Msaidizi wa
Uhamiaji. Zoezi hilo halikuwa na
matatizo yoyote, na waliochaguliwa
walitakiwa kuripoti kazini tarehe 29
Julai lakini kwa sababu ya Sikukuu
sasa wataripoti baada ya sikukuu.
Hivyo tunapenda kufafanua kuwa
wasailiwa waliochaguliwa kujaza
nafasi 70 za Mkaguzi Msaidizi wa
Uhamiaji hawahusiki na usitishwaji
uliotangazwa jana na wanatakiwa
kuendelea na mipango ya kuripoti
kazini kama ilivyotangazwa hapo
awali.
Wasailiwa wanaohusika na
kusitishwa kwa ajira zao ni wale
waliokuwa wameshiriki katika zoezi
la kuajiri Konstebo na Koplo wa
Uhamiaji ambao idadi yao ni 200,
ambao walitakiwa kuripoti tarehe
06 Agosti, 2014 lakini kwa sasa
hawa ndio wanaelekezwa wasubiri
hadi hapo watakapopewa
maelekezo mengine.
Sgn
Isaac J. Nantanga
MSEMAJI WA WIZARA YA MAMBO
YA NDANI YA NCHI
29 JULAI, 2014
Big shame on you!
 
Kwanini wasikubali kushindwa, hafu zoezi zima la kuwania hizo nafasi likaanza na upya?

Wafute kwasababu wewe umesema au kwasababu wote wanafikiri kama wewe unavyofikiri,lete arguments za kwnini wafute,mf.wafute kwasababu usaili ulifanyika Dar tu bila kuhusisha mikoa mingine ya mbali km katavi,umeona hiyo hoja?
 
Suala la kufuta majina yote na kuanza usaili upya sio tatizo ila kumbuka serikali huwa inaenda kwa utaratibu..mfano mchakato mzima wa usaili ulikuwa umeshatengewa fungu kwa ajili ya zoez zima.ukumbi wa kule baraza la maaskofu ulikuwa unalipiwa kwa siku plus watu wote wa kamati walikuwa wakilipwa posho kwa uendeshaji wa mchakato..sasa ukisema tufute ina mana tuanze upya tena watu wafanye usaili upya,twende posta tukachukue barua kwa magar na uchambuz mpya(use of money resource).then tu shortlist na kuanza usaili upya hapo unazungumzia january sasa..then kumbuka kati ya watu 200 sio wote walipendelewa wapo waliokuwa na sifa zote na walifaulu usaili kwa haki ila wapo wachache ambao ndio washukiwa.je hatima ya wale ambao hawausiki na mfano ingekuwa ni wewe ndo ulipita kwa haki ungependa jina lako likatwe sababu ya wengine..ndio mana katibu ametoa taarifa kuwa amesitisha na sio kufuta ili kupisha uchunguzi wa hizo tuhuma zilizofika mezani kwake..kwaiyo sio rahis kusema zifutwe bila ushahid wowote angefanya hivyo angekuwa yupo kinyume na taratibu za kazi.
 
kamati inakwenda kuchunguza all suspects mentioned by the medias..are they related with immigration servants or not..then did they qualified to be employed or not..na je taratibu zote za usaili zilifuatwa au wengine walochomekwa njiani....na point ya msingi ni je..kama kuna watoto au ndugu wa uhamiaji walifanya usaili na kufaulu sawa na wengine je kwann hawa waitwe wengine waachwe..
 
Back
Top Bottom