Mkurabitambo
JF-Expert Member
- Feb 3, 2010
- 230
- 57
Juzi wakati wa kuchangia hoja ya bajeti ya serikali ya mwaka 2012/13,Vita Kawawa alisimama na kujaribu kueleza kuhusu deni la taifa.Kiukweli ninachoweza sema alijitahidi kutuhadaa watanzania kwa mahesabu yake yasiyo na tija.
Vita alisikika akisema kila mtanzania anadaiwa tSH 440000 Ambayo ukiigawa kwa idadi ya siku na kwa riba ya mkopo inaonyesha kila mTanzania anahitajika kulipa shilling 17 kila siku kulipia deni la Taifa.
Turudi katika hoja ya mch Msigwa mbuge wa Iringa,yeye alisema kwamba kulingana na takwimu zilizopo asilimia 50 ya watanzania ni watoto,na wengine 25-30 ni wazee,hivyo kuifanya Tanzania kuwa na wazalishaji wachache zaidi ya walaji.
Hoja yangu ni juu ya Vita Kawawa kudai eti deni hili linabebeka, atuambie linabebekaje? chukulia mfano wa Mtanzania wa kawaida mwenye familia ya watoto watano, na ndugu wamtegemeao 3 hivyo kufanya ratio kati ya mzalishaji na walaji kuwa 1:8.Hivyo deni la watu nane linahudumiwa na mtu mmoja.
Tunaposema deni la taifa limepanda bwana Vita ujue kwamba tunaolihudumia linatuumiza,usijifananishe eti Tanzania na Japan wapi na wapi bwana..Tunatarajia wawakilishi wetu Bungeni mtumie ubongo kufikiri na sio masaburi
TAIFA LINAANGAMIA KWA KUKOSA MAARIFA NA UDHAIFU WENU VIONGOZI NA USHABIKI WAO WA KISIASA
Vita alisikika akisema kila mtanzania anadaiwa tSH 440000 Ambayo ukiigawa kwa idadi ya siku na kwa riba ya mkopo inaonyesha kila mTanzania anahitajika kulipa shilling 17 kila siku kulipia deni la Taifa.
Turudi katika hoja ya mch Msigwa mbuge wa Iringa,yeye alisema kwamba kulingana na takwimu zilizopo asilimia 50 ya watanzania ni watoto,na wengine 25-30 ni wazee,hivyo kuifanya Tanzania kuwa na wazalishaji wachache zaidi ya walaji.
Hoja yangu ni juu ya Vita Kawawa kudai eti deni hili linabebeka, atuambie linabebekaje? chukulia mfano wa Mtanzania wa kawaida mwenye familia ya watoto watano, na ndugu wamtegemeao 3 hivyo kufanya ratio kati ya mzalishaji na walaji kuwa 1:8.Hivyo deni la watu nane linahudumiwa na mtu mmoja.
Tunaposema deni la taifa limepanda bwana Vita ujue kwamba tunaolihudumia linatuumiza,usijifananishe eti Tanzania na Japan wapi na wapi bwana..Tunatarajia wawakilishi wetu Bungeni mtumie ubongo kufikiri na sio masaburi
TAIFA LINAANGAMIA KWA KUKOSA MAARIFA NA UDHAIFU WENU VIONGOZI NA USHABIKI WAO WA KISIASA