Pengine hakuna ubishi kuwa watu wanapona kwa kunywa hii dawa. Nasema pengine kwasababu mimi binafsi sijakutana nao. Ubishi uliopo ni kama uponyaji huu unatoka kwa Yesu Kristu au mungu mwingine. Wakristu tuna Utatu Mtakatifu, kwahiyo ninaposema Yesu nawaunganisha Mungu Baba na Mungu Roho pia. Na nimeamua kutumia Yesu ili kutofautisha na hao miungu mingine.Waandishi Wetu
MCHUNGAJI Ambilikile Masapila anayetoa tiba ya magonjwa sugu katika Kijiji cha Samunge, Loliondo amewataka wagonjwa kuendelea kutumia dawa za hospitali hata baada ya kunywa dawa yake.Akizungumza kijijini hapo jana, Mchungaji Masapila alisema hakuna madhara kwa mgonjwa kuendelea na dawa zake za awali hata baada ya kunywa dawa yake na kwamba si vyema kuacha ghafla kutumia dawa hizo.Hii dawa yangu inatibu, lakini haizuii kunywa nyingine, unaweza kunywa na ukiona umepona kabisa usiendelee kunywa dawa hizo, alisema.
MWANANCHI.
Habari hii imeandikwa na Salim Mohamed, Neville Meena na Mussa Juma, Samunge.