Kahumbi Lumola
JF-Expert Member
- Mar 3, 2012
- 359
- 2,569
Mimi naitwa Lumola Steven Kahumbi ni Waziri mkuu wa serikali ya wanafunzi DIT, juzi tarehe 14/08/2014 saa 2 usiku, mimi pamoja na Mh. Mwenyekiti halali wa TAHLISO MUSA MDEDE, Rais wa DITSO, Spika wa bunge IFM, Mweka HAZINA WA TAHLISO, Spika wa bunge DITSO pamoja na Waziri wa fedha IFM tulikamatwa na watu waliojitambulisha kuwa wao ni polisi tukiwa tunakula chakula kisha walitufunga pingu wakatupeleka kituo cha polisi Osterbay ambapo walituchukua maelezo mpaka saa 8 asubuhi baada ya maelezo walituweka mahabusu kwa tuhuma ya uchochezi.
Asubuhi walitutawanya katika vituo tofauti tofauti vya polisi na ilipofika mchana waliturudisha osterbay ambapo tuliongea na RPC kinondoni na baadae alikuja afisa kutoka kanda maalumu ya Dar es salaam. mpaka hivi sasa sisi sote tumeachiwa kwa dhamana. Mapema katika wiki zilizopita tulitoa tamko la kuipa serikali kuu siku 7 wawe wametimiza malipo ya fedha kwa ajili ya field ambayo wameyachelewesha kwa wiki 5 lakini siku 7 zilikwisha na serikali haikutimiza agizo letu kwao, tukakutana tena na vyombo vya habari tarehe 13/08/2014 ambapo tulitangaza maandamano nchi nzima kwa ajili ya kuishinikiza serikali kulipa fedha hizo Kwa ufupi hiyo ndio ilikuwa sababu ya sisi kukamatwa.
Katika HIstoria ya nchi yetu tangu tulipozaliwa kama Taifa huru haijawahi kutokea Uzembe na Makusudi kama haya kwa serikali kuchelewesha fedha za field kwa wiki saba. Ni tukio jipya kabisa ambalo kwa kila anayejua umuhimu wa field kwa wasomi lazima ataishangaa serikali yetu kwamba Inafikiria nini. Walituhoji sana kuhusu kibali lakini tulichowajibu, tuliwaambia hayo yanayoitwa maandamano bado hayajafanyika kwahiyo hatuwezi kuhoji juu ya uhalali au uharamu wake.
Asubuhi walitutawanya katika vituo tofauti tofauti vya polisi na ilipofika mchana waliturudisha osterbay ambapo tuliongea na RPC kinondoni na baadae alikuja afisa kutoka kanda maalumu ya Dar es salaam. mpaka hivi sasa sisi sote tumeachiwa kwa dhamana. Mapema katika wiki zilizopita tulitoa tamko la kuipa serikali kuu siku 7 wawe wametimiza malipo ya fedha kwa ajili ya field ambayo wameyachelewesha kwa wiki 5 lakini siku 7 zilikwisha na serikali haikutimiza agizo letu kwao, tukakutana tena na vyombo vya habari tarehe 13/08/2014 ambapo tulitangaza maandamano nchi nzima kwa ajili ya kuishinikiza serikali kulipa fedha hizo Kwa ufupi hiyo ndio ilikuwa sababu ya sisi kukamatwa.
Katika HIstoria ya nchi yetu tangu tulipozaliwa kama Taifa huru haijawahi kutokea Uzembe na Makusudi kama haya kwa serikali kuchelewesha fedha za field kwa wiki saba. Ni tukio jipya kabisa ambalo kwa kila anayejua umuhimu wa field kwa wasomi lazima ataishangaa serikali yetu kwamba Inafikiria nini. Walituhoji sana kuhusu kibali lakini tulichowajibu, tuliwaambia hayo yanayoitwa maandamano bado hayajafanyika kwahiyo hatuwezi kuhoji juu ya uhalali au uharamu wake.