Sylvester Ambokile Mwakinyule ateuliwa kuwa Kamishna Mkuu, Idara ya Uhamiaji

Magnus Ulungi alikuwa kama boya pale, ngoja aje huyo pengine ataondoa ule utando a wachaga waliojaa HQ kwa kujifanya wao ndio wamesoma peke yao na kwamba wengine elimu zao wazitumie Tandahimba, Kazulamimba, Nampembe na Chwaka
Poor Ulungi alikuwa amewekwa mfukoni na vilaza Shayo, Mongi Kishe & Co.
 
Uteuzi huu unaenda sambamba na saga za EAC na uozo uliobainika kwa wahamiaji haramu hususan Banyarwanda, TISS hapa wamewajibika vema kutazama the root cause ya hii kitu.

Kwa hiyo umepata sababu ya kuisifia TISS eti? Hapo sio kama kusifia ma.vi kwa sabu yamekauka sasa harufu imepungua!?

mtuwekee cv yake.asije akawa anatoka mlima mulenge

Ila kweli wanaweza kuwepo wanyamulenge wa Katusyo... na mtuwekee cv yake hapa tumjue
 
Simjui vyema huyu Ambokile ila kwa kuwa ushaula ALL THE BEST
Anza na wasomali then malizia na hao wengine wanaofanya TZ shamba la bibi
 
Kwenye hii issue ya uhamiaji wote tuko pamoja hakuna mambo ya vyama. Huyu Kagame lazima ajue TZ siyo ya kuchezea. Namuomba rais afanye kila liwezekanalo Kagame aondoke madarakani ni mtu hatari sana katika ukanda wa maziwa makuu.
 
Mkuu, huyu Chemundugwao si alikuwa anashinda kutwa pale posta mpya na kanisa la St Albans au YMCA?

Nafikiri hizi zote zilikuwa ni kona zake za kukutana na wateja wa passport maana zilikuwa ni karibu na Mambo ya Ndani na tokea Uhamiaji ipelekwe Kurasini biashara si itakuwa ngumu kidogo kwenye usafiri?
ndio huyo huyo mkuu alikuwa mtu wa mission town haina mfano
 
MAMBO KUMI YA KUZINGATIA KWA KAMISHNA MKUU WA UHAMIAJI.
Nimeamua kutoa muongozo huu ukusadie kwa kujua kuwa changamoto kwenye taasisi nyingi za umma kwa kiasi kikubwa zinafanana hivyo naamini pia yanaweza kusaidia kwenye Idara yako.
1. Uzaliwe upya (born again)- Kwa kumtegemea Mungu kikamilifu kwa kufanya aliyoamrisha na kuyakataa aliyoyakataza
2. Utatu shirikishi- Endesha Idara kwa kushirikisha Uongozi,Watumishi na Wananchi. Toa nafasi na uwezekano wa ushirikiano ili kutokomeza kero zinazopigiwa kelele kwenye Idara ya Uhamiaji kama wahamiaji haramu, utoaji wa pasipoti na vibali vya kuishi nchini kucheleweshwa, kutolewa kwa rushwa, na kupewa watu wasiyostahili.
3. Onyesha njia-Amrisha mazuri nawe uwe mfano wa kutenda mazuri mazuri
4. Usifanye upendeleo- Usikumbatie ubaguzi au upendeleo wa dini, kabila, urafiki na jinsia. Uwe mwenye kuunganisha watumishi
5. Toa haki na timiza wajibu- Watumikie wananchi na watumishi wape haki zao kwa mujibu wa sheria. Watendaji wazuri watiwe moyo,walindwe na wapewe nafasi, kuwa mtetezi mzuri na uwe ni msaada na huruma kwa watu.
6. Kuwa jasiri- Watendaji wabovu, wakorofi, wala rushwa, wezi, wabadhirifu wa mali ya umma, walevi wa kupindukia, wavivu, wazembe, wababaishaji, wenye majungu, waliokosa maadili usiwape nafasi wapige chini, kuwa mkali.
7. Kuwa mbunifu- Ibua mambo mazuri yenye tija kwa Idara, Watumishi, Serikali, na wananchi. Ibua vipaumbele vyenye kulenga maeneo muhimu na maalumu kwa Uhamiaji na elekeza nguvu huko na unda kanda maalumu,jua mahitaji, jengo hoja na utetee hoja yako. Uwe mwenye Uthubutu.
8. Chukua hatua za haraka- kuwa mwepesi kwa kutoa maamuzi na kuchukua hatua za haraka zenye manufaa kwa taifa, lakini bila ya kukurupuka, usiwe ni mzigo.
9. Uwe mwenye msimamo na kuangalia mbele- Utathmini mambo, simamia maamuzi na yatekelezwe, ili mradi ulalofanya ni kwa nia njema na halina madhara kwa taifa.
10. Toa nafasi –Wape nafasi wasomi waonyeshe ujuzi wao, wape nafasi wakomavu waonyesha uwezo wao, wape nafasi waadilifu wadhibiti mianya ya rushwa,wizi na ubadhirifu wa mali ya umma.
Mwisho uiombe Serikali ikupatie fungu la kutosha kwa ajili ya kupanga safu yako (timu ya ushindi) ili kupata "Big result now" ikibidi "review organization chart" kwani taasisi nyingi za umma muundo wake wa kiutawala ni mbovu hivyo inapelekea utendaji na utekelezaji wa majukumu kuwa mgumu, nakutakia kila heri katika kutumikia majukumu yako mapya ya kazi.
 
10. Toa nafasi –Wape nafasi wasomi waonyeshe ujuzi wao, wape nafasi wakomavu waonyesha uwezo wao, wape nafasi waadilifu wadhibiti mianya ya rushwa,wizi na ubadhirifu wa mali ya umma.
Mwisho uiombe Serikali ikupatie fungu la kutosha kwa ajili ya kupanga safu yako (timu ya ushindi) ili kupata "Big result now" ikibidi "review organization chart" kwani taasisi nyingi za umma muundo wake wa kiutawala ni mbovu hivyo inapelekea utendaji na utekelezaji wa majukumu kuwa mgumu, nakutakia kila heri katika kutumikia majukumu yako mapya ya kazi.

Hapo kwenye maandishi mekundu natilia mkazo ili upate "big results now" nakushauri kwa nia njema kabisa na wala siyo kwa ubaguzi nashauri wateue watumishi wachapakazi wazuri lakini wenye "kufanana na imani za kilokole lakini wasiyo na ubaguzi wa kilokole" ili wadhibiti mianya ya rushwa, wizi na ubadhirifu wa mali ya umma. katika maeneo ambayo unaona yanafaa kudhibitiwa.
 
Mkuu JamboJema,
Kuijua Uhamiaji mpaka ufanye kazi mikoani?

Ambokile amefanya kazi Uhamiaji hapo makao makuu, Airport, TIC na kwa miaka minane sasa kama Mwambata wa Uhamiaji London. Kipindi chake cha kukaa London kimeongozana na kipindi ambacho Uhamiaji imekuwa issue kubwa kwa hizi nchi za West na hivyo kushirikiana kwa karibu sana na nchi zetu katika kupambana na suala la Wahamiaji haramu. Kwahiyo Ambokile amefaidika na mafunzo na uzoefu ambao utamsaidia sana nyumbani kama ataungwa mkono na wenye nchi.

Lakini pia Ambokile amezaliwa na kukulia Kyela ambako ni mpakani na suala la Uhamiaji sio geni kabisa. Ana Elimu yake nzuri tu ya Bachelor ya UDSM miaka ya 80 na baadaye Masters ya UK.

Kikubwa ni mchapa kazi mzuri na pia ni binadamu kwa utu. Binafsi ninaamini kama wenye nchi Watamuunga mkono basi kuna faida kubwa kwa Ambokile kupewa hiyo nafasi maana hajachafuka na madudu ya Uhamiaji kwa miaka kumi iliyopita. Yeye anakuja kama mtu aliyetoka nje ya Uhamiaji. Na hapa duani ukitaka kufanya mabadiliko ya kweli basi lete mtu toka nje ya organisation.

Mafanikio makubwa mkuu Ambokile. Uzuri matatizo yote ya Uhamiaji unayajua vizuri maana tumeyaongelea mara nyingi sana. Sasa ni kujaribu kuweka kwenye vitendo solutions mbalimbali na kuikoa nchi yetu kutokana na majanga mbalimbali ya Wahamiaji haramu na matumizi mabaya ya passports zetu.

Wish you all the best.

Ninamfahamu kidogo huyu Ambokile.....Na hapa ndo panaponipa wasiwasi. Ni kweli huyu bwana anaijua Uhamiaji? Ni kwamba Ambokile inaaminika tangu aingie Uhamiaji hajawahi fanya kazi nje ya Dar es salaam......yaani baada ya kutoka Dar ni moja kwa moja London. Anajua kimsingi Idara hii inamatatizo gani kiutendaji mipakani, mawilayani hadi mikoani? Isije kuwa ni tatizo lile lile kama la Ulungi ambaye pia hakuwa na 'experience' yoyote na mikoani.
 
Magnus Ulungi alikuwa kama boya pale, ngoja aje huyo pengine ataondoa ule utando a wachaga waliojaa HQ kwa kujifanya wao ndio wamesoma peke yao na kwamba wengine elimu zao wazitumie Tandahimba, Kazulamimba, Nampembe na Chwaka
Poor Ulungi alikuwa amewekwa mfukoni na vilaza Shayo, Mongi Kishe & Co.
Hawajawahi kusema Uhamiaji inaongozwa na Cadema? Maana siku hizi kila uchaga unaunganishwa na Chadema hata ukiwa ndani ya CCM
 
Hawajawahi kusema Uhamiaji inaongozwa na Cadema? Maana siku hizi kila uchaga unaunganishwa na Chadema hata ukiwa ndani ya CCM

Hilo nalo neno Serikali iwe macho asiwe anafanyakazi na mamluki "akawa anatwanga maji kwenye kinu"
 
Mkuu JamboJema,
Kuijua Uhamiaji mpaka ufanye kazi mikoani?

Ambokile amefanya kazi Uhamiaji hapo makao makuu, Airport, TIC na kwa miaka minane sasa kama Mwambata wa Uhamiaji London. Kipindi chake cha kukaa London kimeongozana na kipindi ambacho Uhamiaji imekuwa issue kubwa kwa hizi nchi za West na hivyo kushirikiana kwa karibu sana na nchi zetu katika kupambana na suala la Wahamiaji haramu. Kwahiyo Ambokile amefaidika na mafunzo na uzoefu ambao utamsaidia sana nyumbani kama ataungwa mkono na wenye nchi.

Lakini pia Ambokile amezaliwa na kukulia Kyela ambako ni mpakani na suala la Uhamiaji sio geni kabisa. Ana Elimu yake nzuri tu ya Bachelor ya UDSM miaka ya 80 na baadaye Masters ya UK.

Kikubwa ni mchapa kazi mzuri na pia ni binadamu kwa utu. Binafsi ninaamini kama wenye nchi Watamuunga mkono basi kuna faida kubwa kwa Ambokile kupewa hiyo nafasi maana hajachafuka na madudu ya Uhamiaji kwa miaka kumi iliyopita. Yeye anakuja kama mtu aliyetoka nje ya Uhamiaji. Na hapa duani ukitaka kufanya mabadiliko ya kweli basi lete mtu toka nje ya organisation.

Mafanikio makubwa mkuu Ambokile. Uzuri matatizo yote ya Uhamiaji unayajua vizuri maana tumeyaongelea mara nyingi sana. Sasa ni kujaribu kuweka kwenye vitendo solutions mbalimbali na kuikoa nchi yetu kutokana na majanga mbalimbali ya Wahamiaji haramu na matumizi mabaya ya passports zetu.

Wish you all the best.

Let me simply say 'AMEN'. I hope for the best for the idara.
 
asante mh. kwa hili, uhamiaji haramu ni tatizo kubwa san ahapa nchini, tulifanya kama pripirity, fukuza wote tuanze mojs kama vile ndio tanzania imepata uhuru wake
Ungekuwa unasimamia hoja bila kusukumwa na ushabiki kama hivi tungekuwa mbali sana ktk kutokomeza udhalimu hapa nchini.
 
Toa MaDCI JNIA, KIA, HQ, Namanga waliojazana wakigonga mihuri, kazi ambazo wanapaswa kufanya kazi Mawilayani kama MaDIOs na wakihamioshwa bado wanahonga utumishi na kurejea vituo vya awali,

Matokeo yake mawilayani wakuu wa Uhamiaji huko ni maafisa wanaokaimu wenye vyeo vidogo, Ambokile ukifika ofisini omba orodha ya MaDIOs wote na uombe wakwambie waliothibitishwa na wanaokaimu nafasi hizo na ni kwa muda gani wamekaimu, na je nafasi hizo zinapaswa kushikiliwa na maafisa wa kuanzia vyeo gani?

Kiukweli maafisa wanaopaswa kushika nafasi za wilaya wengi wakipangiwa hawaendi wamejazana ktk vituo vyenye neema kama KIA, Namanga, JNIA, Tunduma, Makao Makuu ila mawilayani hawataki kwa sababu huko maporini hakuna maslahi kwao. Ambokile timua vibabu vyote katika vituo hivyo.

Kuwa makini na Maafisa kadhaa ambao huamua nani afanye kazi wapi? Wao huhakikisha watoto, wajukuu, mashemeji na wapambe wao wanaendelea kufanya kazi katika vituo nilivyovitaja na wengine wasiowajua wakibaki maporini na kustaafia huko,

Ambokile fanya kazi bila woga, usiwe na upendeleo safisha Uhamiaji yote

Nawasilisha
 
Toa MaDCI JNIA, KIA, HQ, Namanga waliojazana wakigonga mihuri, kazi ambazo wanapaswa kufanya kazi Mawilayani kama MaDIOs na wakihamioshwa bado wanahonga utumishi na kurejea vituo vya awali,

Matokeo yake mawilayani wakuu wa Uhamiaji huko ni maafisa wanaokaimu wenye vyeo vidogo, Ambokile ukifika ofisini omba orodha ya MaDIOs wote na uombe wakwambie waliothibitishwa na wanaokaimu nafasi hizo na ni kwa muda gani wamekaimu, na je nafasi hizo zinapaswa kushikiliwa na maafisa wa kuanzia vyeo gani?

Kiukweli maafisa wanaopaswa kushika nafasi za wilaya wengi wakipangiwa hawaendi wamejazana ktk vituo vyenye neema kama KIA, Namanga, JNIA, Tunduma, Makao Makuu ila mawilayani hawataki kwa sababu huko maporini hakuna maslahi kwao. Ambokile timua vibabu vyote katika vituo hivyo.

Kuwa makini na Maafisa kadhaa ambao huamua nani afanye kazi wapi? Wao huhakikisha watoto, wajukuu, mashemeji na wapambe wao wanaendelea kufanya kazi katika vituo nilivyovitaja na wengine wasiowajua wakibaki maporini na kustaafia huko,

Ambokile fanya kazi bila woga, usiwe na upendeleo safisha Uhamiaji yote

Nawasilisha



Hayo unayosema kweli kabisa, vibabu vyenye vyeo vikubwa havitaki kufanya kazi zinazostahili kulingana na vyeo vyao, badala yake vimejazana makao makuu na uwanja wa ndege na border kubwa kama namanga vikiongoza kwa kuomba rushwa na kutia mifukoni nmapato ya serikali,

Uhamiaji ifanyiwe restructure/Reform kama ilivyofanyiwa TRA kwa kuwa mapato mengi sana yanaingia mifukoni mwa watu,

Nashauri yafuatayo yafanyike
1. Kutumia technologia ya kisasa kama mifumo ya hati za kusafiria na hati za ukazi ili mikoani iwe rahisi kufikia makao makuu kwani sasa inachukua muda mrefu kwa mtu kuomba hati hadi kutoka, pia maombi mengi yanakuwa na makosa madogo madogo au kupotea na bila ya kuwa na kumbukumbu, yaani unaomba passport kigoma unaenda kuiulizia baada ya miezi mitatu eti bado haijawa tayari au unaambiwa ombi lako halionekani

2. Kufundisha customercare kwa maafisa uhamiaji kwani wengi wao wanafanya kazi kimazoea, yaani unaenda uhamiaji unaongea na afisa utadhani wewe mtuhumiwa

3. Ambokile awaangalie wasomi waliojazana uhamiajia ambao hawafanyi kazi walizosomea badala yake ni kgonga mihuri mwanzo mwisho kwa kuwa tu mihuri ndio kila kitu ktk maisha.

4. Naungana na Mfereji Maringo kusafisha makao makuu ili kuleta safu mpya na kuwaondoa miungu watu waliojazana hapo makao makuu,

Nawasilisha
 
Back
Top Bottom