Kinachowaweka watu wawili kwenye ndoa sio 'huruma' bali ni mapendo na mapenzi. Maana huruma itakapoisha ndio visanga vitakapoanza!
Pili ile heshima na hofu ya ushemeji haitokaa itoke kwangu (labda ndio ninavyoulinda moyo wangu na vishawishi vya shemeji wakware). Sithubutu kumvulia nguo na mume wangu anahisi ataniona na kunishangaa huko aliko!
Kwa majibu hayo mawili, shemeji hawa watoto ni wako wasaidie unapoweza. Mie mkubwa nitajiju, hapana ahsante!