Kwanini wanawake hatujifunzi Wanaume ni tunda la msimu hawana guarantee.

lara 1

JF-Expert Member
Jun 10, 2012
15,700
29,111
Igweeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee!

Hii topic naiongea kila siku mpaka mtaona niko obsessed na haya mambo ila mkiona naongea ujue huku kishanukaaa. Same old story, same old shit ila people never learn. Sijui kwanini. I just dont know.

Mid January 2016 alirudishwa my sis, ni cousin ila alikulia nyumbani. Aliolewa na amezaa fasta fasta watoto wa 3. Sasa kilichonisikitisha huyu cousin ni msomi kabisaa alikuwa kazi bank, ambayo bi mkubwa ili apewe hio kazi na alienda kwa waziri flani kupiga magoti. Mi mwanae hajawahi kunipa msaada huo, ila yule ndugu yangu alimsaidia vile sijui alimloga au vipi bi mkubwa wangu mgumu sanaaa, kama mimi kubwa la maadui yeye Teminator hatakagi ujinga. Akasimamia tu she had to do that cause yule ndo tegemeo la familia yao, akiinuka yule familia yao itainuka. She jus had to do it.

2 yrs kazini kapata mume shosti kaolewaaa. Basi maneno kumtokaaa. Sio kutusema sisi na bi mkubwa wetu. Bi mkubwa akasema fadhila mfadhili mbuzi utamnywa mchuzi binadamu atakuuzi. Wakaparangana kwanza wadogo zake tumbo moja hasomeshiii, mmoja tukapata taarifa anafanya u hausgeli wa ndani Tanga huko. Wa form 4. Anafua kabisa mi chupi kwa watu. Akaenda kumchamba na mimi mchambaji msaidizi. Akawa anatoa majibu mepesi kwa hoja nzito kuwa sasa mimi nifanyaje si kaamua kuwa hausgirl. Mama anamwambia mbwa wewe nisingejinyima kukusomesha si ungekuwa unafua chupi kwa watu, kamfate mtoto. Ooooh mume hataki. Bi mkubwa akamwambia Mume ndugu wa kinenaaa. Mtu umekutana ukubwani, umesoma, unangaa, sio ndugu huyo rafiki tu. Usipomfata mtoto undugu wetu umekufa. Na hakumfataaa.

Ukapita mwezi akamfata bi mkubwa mwenyewe na kumpeleka ualimu, sahivi ni mwalimu huyo dada. Alilia siku aliofatwa, kumbe alikuwa anateseka hakuna mfano. Bi dada huku kazi yake majungu tu, wanaionea wivuuuu, wanioneaaa wivuuu. Bi mkubwa akamuuliza tukuonee wivu kwa hizo vuzi ulizofuga, mume mwenyeww Free P, unamlisha na kumfuga, tukuonee wivu upi. Hakujibu. Biff likaendela kunoga.

Tukaja kusikia kachukua mkopo million 15. Bi mkubwa akawahi kumdai deni lake milion 2 hakumlipa wakati alikopa wakaandikishiana. Sisi wote anatudaigi mpaka kwa mjumbeee, mpaka kwa baba, utamlipa tuuu hana ujinga kwenye pesa mchaga yule, ila mwenzetu alimshindwa. Bi dada Akaja kuniambia nimempa hela shemu wako million 15, nataka umpe conection afanye business. Mmmmh! Nikamwambia si ufanye wewe hio biashara shoga angu, utusaidie mizigo pale nyumbani, si unajua pale palivokuwa na mizigo ya ada. Mzee kasatafu, sterling sahivi bi mkubwa nae hana miaka 5 anastaafu, ukipata wewe tumepata sisi akipata mumeo wamepata ndugu zake hivooo.

Akaniambia hujaolewaaa, hujui ndoaaaa. Ndoa haitaki uchoyo, huwezi kuelewa ndoaaa, ndoa kuelewana. Nikamwambia wewe mama yako mzazi si aliolewa mbona alikimbia kwa mume. Shauri yako unachezea maisha. Akaniambia kwa uchoyo mlio nao na mama yenu huwezi kuishi na mwanaume hata siku moja, mjomba kamvumilia sanaa mama yenu. Hahahaaa. Mxiuuuuuuuu. Nikamwambia mi connection sinaaa.

Huku na huku kamnunulia huyo kaka kirikuu, akamfungulia na duka lipia frame sijui nini. Million 15 pyuuuu. Kirikuu hesabu haleti waweke kwenye rejesho, kimshahara kina fyekwaaa. Huku na huku kumbe waliuziwa gari bovu, likafa miezi 6 tu. Na duka likafa. Na bank yao wakapunguza watu, akapunguzwa manake hakusoma chochote miaka yote akiuwa anachukua maternity tu.

Maisha yamekuwa magumuuu magumuuj, anatupigia kutuomba kodi. Nani ampe. Anamsumbua yule ticha hausgeli. Nikamwambia ukimpaaaa, utakuwa mjinga, bora umpe mke wa mjomba wako anywe bia tu. We wakati unasugua vyoo si alikuwa analea ndoaa, ana drive na nini mbona hakuuona undugu wenu. Ticha akasema mi siwezi kumnyima nikamwambia mwambie Lara amesema nisikupe, ole wangu nikupe wananitenga. Huku na huku karudi nyumbani na watoto wa 3.

Kavizia bi mkubwa hayupo anafanya kazi mkoani, sasa mzee kajichokea drama drama nyingiii, afu mzee mjomba wake, anamchukulia mtoto wa dada yake poaa tu. Mzee alijua karudi temporary, baada ya wiki kamwambia nimerudi permanent, yule bwana tumeshindwana alivoina bi dada kafilisika kaamia kwa mdada mwingine boss wa TBL, na kashampa mimba. Sasa anamwambia Mzee inabidi hawa watoto niwaache hapa nikatafute maisha. Heheheeee! Sasa akaamuliza unawaachaje na ada zao na matumizi au vipi. Mjomba mi ada napata wapi? Mjomba akamwambia hapa mke wangu ndo anasimamia show, business zangu zote, investment zangu anasimamia yeye na kila kitu, si unajua mi nimezeeka anasimamia anatunza hili zigo hapa, mi nakula pension tu ambayo hainitoshi hata kwa bia. Labda umwambie yeye.

Bila hayaaaa akatuma sms, mmmmhhhh! Kifupi bi mkubwa kamtimuaaaa kama mbwa, kamwambia watoto wapeleke kwa baba yao, hawataki wapeleke kijijini. Nisikute zigo nililoliacha limeongezeka hata robo. Usinitanie. Mi nifanya kujirudisha miaka nyuma kila kukicha nisi staafu, naumwa nakomaa hivi hivi umepata maisha umechezea bibi zimaaa. Bora wenzio wanadanganywa form 2, 3, 4 utasema wamezidiwa akili ndo maana niliwapa second chance na wamejifunzaaa. Ndoa imejambaaa kwenuuu Marangu sitaki kabisaa mazoea. Basi anajibalaguza wanangu wamekukosea nini mpaka uwafukuze kwako. Akamuuliza wamemkosea nini baba yao kawatimuaaaa. Usinibaneee, sitakiiii.

Sahivi yupo kijijini na wanae, wanasoma shule elimu bure, yeye anauza papa tu. Anawagaia watu wa bank za Marangu pale, akiitwa dar aje apige night worker anafikia kwangu analiwaa, anapewa hela ya sabuni na wembe anarudi kulea watoto. Life can be cruel. Zamani wakati ana vihela wanae walikuwa kama yai, wakija nyumbani anawabagua na watoto wa pale as if wale watoto ni contaminated au waathirika. Anawadekezaaa, kitu kidogo Lara hujazaa wewe hujui uchungu wa mtoto. Nilivoenda Marangu eeeeeh anavowatukana watoto utasema sio wake. Mitusi ya nguoniiii. Mpaka nikaingiwa imani. Nikamkumbusha sijazaaa ila hayo sio malezi. Analalamika wamenilostishaaa, wameniaribia future yangu, wangese kama baba yao. Mmmmmmh! Maisha yanajua kuvurugaaa.

Kazi kupata mke wa mtu mwenye watoto wa 3 sio rahisi kabisaaa. Ukizingatia bank kule hakutumia mda ule kujenga career base alikuwa anazaa tu. Maternity nyingi kuliko time worked. Uzazi na shida anaonekana mzee kumbe toto dogo na akisema ana watoto wa 3 ndo anazidi kuonekana mzee, toto la 1986. Na still mawazo yake ataolewa tena kutoka kimaisha tena heheheeee. Very optmistic.

Kinachonisikitisha wanawake wenzangu WHY HATIJIFUNZII? Haya mambo si mageni si mapyaa. Hapo home watu kibao wanazaa vinajambaaa wanakazi ya kusaidiwa kuelea, wengine waliolewa ovyo ovyo washaachika wapo na mizigo yao wengine wameolewa ila wanajikazaaa tu kwa aibu kurudi, na wanajua hio option ya kurudi hawajapewaaa wanakomaaa tu, wengine wana bahati wamaolewa sehemu nzurii for now ila ndo watu wa mashauziiii hawakumbuki kabisaa walikotoka, wanaweka heshima mjini, kuwaona na kina Shamim na wadada wa mjini sio jambo geni kabisaa, hawajiwekezei chochote, hawainvest popote, ndo zimejibu, pale ndo wamefikaaa jiji liwajue. Sasa unajiuliza hawaoninyaliowakuta wenzao au vipi? Family Holiday za dubai, USA, Paris na sisi tunaponea hapo hapo kusema yule ndugu yangu bwanaaa. Kabisaaaa, kabisaaaa. Ukiwakuta wanavobeza walioachika kama wana undugu wa karibu na Sir God. Bi mkubwa kashatoa tamko, ukitibua kwako kapange, ghetto lako lilishapangishwa, vyumba vimejaaa. # Kila mtu abebe msalaba wake.

Anakwambia UNAJIONA SPECIAL, VERY SPECIAL , HAYAWEZI KUKUKUTA, YALIOWAKUTA WAJINGA, WAZEMBE, WENYE MIKOSI UNASAHAU DUNIA INAZUNGUKA, JUST MATTER OF TIME. HIVI KUNA UGUMU GANI KUONA YAMEMKUTA FLANI NIFANYE MAANDALIZI KAMA KUJIFANYIA INVESTMENT ZAKO BINAFSI WALAU USIONDOKE MIKONO TUPU. KILA SIKU UNASIKIA VINAJAMBA HUKO KWA WENZIO, KWANINI USICHUKUE TAHADHARI?

Eti kwanini wanawake hatujifunzi.? Nimeona niandike one more time maana ni kama wimbo.
 
Lara uko nchi gani? huku bongo hata mods wamelala juu ya keyboard mida hii..!!
 
Lara mm ni mwanaume,ki ukweli sisy ako ni Mjinga wa karne kwani kuolewa hakuna maana kuwa umetengana na familia yako kiasi huwez kuwaboost japo kidogo walau to show mpo pamoja,binafsi najua kuwa wanaume wengi hatuna mawazo ya kudumu,kwani mnaweza ishi hata miaka 15 ndo ukaona chombo inaenda mrama.ushauri wangu kwenu siku hizi ndoa nyingi ni kama muziki wa bongo fleva yaani una hit leo,kesho hhaupo,chukua hatua kukabiliana na siku ndoa ikichacha.mm ninafanya yafuatayo:kwa Kwa ninaamini mawazo yangu co ya kudumu najenga nyumba nyingine ili kama mawazo yangu yanabadilika nahamia kwenye nyumba hio na ninamuacha mke na watoto wangu salama na ikitokea hakuna kitu basi nyumba hiyoitakuwa our source of income, ndoa za siku hizi hazitabiriki sio mke wala mume.Ahsante.
 
Nadhani sasa wanaume mmeelewa kwanini msioe wanawake wa kichaga...tena kwa ujumbe huu km hujaelewa shauri yako...wao ndoa ni investment ya kutoka zaidi kimaisha...funzo kwa wanaume,kwa wanawake lenu mshapewa
 
Nadhani sasa wanaume mmeelewa kwanini msioe wanawake wa kichaga...tena kwa ujumbe huu km hujaelewa shauri yako...wao ndoa ni investment ya kutoka zaidi kimaisha...funzo kwa wanaume,kwa wanawake lenu mshapewa
Wewe nawee,,,kwaaiyo unahisi investment ni swala uchaga au nimipango tuu mtu ,,ukiwa na kipato niwe nimeolewa niwe sijaolewa lazima niwekeze sio swala la ukabila istoshe nawekeza na pesa yangu shida nin sasa! Wachaga wenyw hatukutaki ,,povu la omo
 
Hahahahahah lohh mfanyakazi wa Benki sio kwa mnyoosho huo Dar to Marangu...heheh wanaume ni nyooko ukiwa hujielewi utaendeshwa kama gari bovu,na kuzaa zaa ovyo ovyo jmn tujiangalie wanawake.,
Na watu tuwe humble pia mana maisha hamna mwenye guarantee kwa Mungu, Ayubu tu hakukosa lolote kwa Mungu ila ndo vile alilosti ile mbaya sembuse sieeee heheh
 
Nadhani sasa wanaume mmeelewa kwanini msioe wanawake wa kichaga...tena kwa ujumbe huu km hujaelewa shauri yako...wao ndoa ni investment ya kutoka zaidi kimaisha...funzo kwa wanaume,kwa wanawake lenu mshapewa
Tatizo hujaelewa mada na wewe...
Na ishu ya kutoka kimaisha kupitia ndoa ni mchezo wa wanawake wengi sana,go figure..
 
Sina hata mia mfukoni ya kununua ndizi, lakini uzuri sipendi ndizi zenyewe mbichi:p
 
Wewe nawee,,,kwaaiyo unahisi investment ni swala uchaga au nimipango tuu mtu ,,ukiwa na kipato niwe nimeolewa niwe sijaolewa lazima niwekeze sio swala la ukabila istoshe nawekeza na pesa yangu shida nin sasa! Wachaga wenyw hatukutaki ,,povu la omo
Si nimewashauri wanaume wenzangu jamani...mbona unajaa sumu...sasa kumshauri mwanamke afanye mambo kibunafsi kisa wanaume hawaeleweki si bora umshauri asiolewe kbs ili kazi yake ya bank akope afanye miradi mingine tatizo lenu kujitongozesha tu na kupenda msipopendwa mixer kung'ang'ania...ila ndoa tamu tu unless uwe na mwanamke wa kichaga
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom