SWALI: Vitu vipi vilivyo kwenye matumizi yetu ya kila siku vinaweza kuwa hatari kwenye maisha ya mwanadamu? .

Chachasteven

JF-Expert Member
Jul 4, 2014
1,883
1,853
Habari wanajukwaa? Ni imani yangu kuwa mpo salama na buheri wa afya zenu. Kwa wale ambao mna utata kidogo na maisha poleni sana na kwa wale ambao mpo safi tuendeleeni na safari hivyo hivyo bila kuyumbishwa.

Kama kichwa cha huu uzi kilivyojieleza. Lengo langu ni kutaka kuweka awareness/kutoa elimu kwa watu na si vinginevyo. Kwa kuwa ninaamini humu ndani tunao watu wa kila aina basi bila shaka swali langu litapata majibu ambayo nayategemea kwa asilimia kubwa kama sio asilimia mia moja.

Turejee kwenye swali: Maisha yetu yamezungukwa na vitu vingi sana. Iwe tunavyokula au tunavyofanyia kazi. Ni kweli vinarahisisha sana shughuli lakini kuna wakati vinaweza kuwa na madhara. Kwa mfano moto na maji. Ukivitumia hivi viwili kwa usahihi ni burudani kwenye maisha yako, lakini ukijichanganya vinakuwa karaha. Hivyo nikawa najiuliza na ndio nawauliza na ninyi pia sasa hivi. Ni vitu vipi ambavyo vipo kwenye matumizi yetu ya kila siku - Kama madawa ya mifugo na sumu za wadudu mashambani - vinaweza kuwa hatari na hata kusababisha madhara, kama kifo, kwa mwanadamu. Kwa mfano kuna zile tetesi kuwa ukichanganya asali na tunda fulani ni sumu na unaweza kufa. Je ni kweli?? Kama vipo tuvitaje hapa chini kwa manufaa ya kila mmoja ili awe makini navyo kwa watoto na kwake pia.

Ahsante.
 
Mkuu ,wanasema ukila ndizi mbivu pamoja na yai lakuchemsha inamadhara,je hii imekaaje?
Hio kitu haina ukweli hata 000.0001%

Mimi ni mlaji mzuri wa huo mchanganyo. Nilishaangaa zaidi kuona kigogo mmoja wa serikali amewepa dp yenye kusema ulaji wa yai na ndizi ni hatari
 
Hio kitu haina ukweli hata 000.0001%

Mimi ni mlaji mzuri wa huo mchanganyo. Nilishaangaa zaidi kuona kigogo mmoja wa serikali amewepa dp yenye kusema ulaji wa yai na ndizi ni hatari
Theory ni nyingi sana kuliko tafiti. Hii ndigo Tanzania yetu bhana.
 
Mkuu ,wanasema ukila ndizi mbivu pamoja na yai lakuchemsha inamadhara,je hii imekaaje?
Madhara mpaka ukitohoa saaaaaaaaaaana ndo unayakuta.

Ukitazama Ayuverdic medicine ndo kuna hint ya jibu. Hawa ndio wamekaziakazia chakula na lifestyle.

Ni kwamba mmengenyo wa ndizi ni polepole na ina tabia ya kupunguza kasi ya mmengenyo wa chakula hasa ikiliwa mara baada ya chakula.

Kwa upande wa yai ni protini ambayo huwahi kuchacha, inapendeza ichakatwe harakaharaka tumboni iondoke ili isitokeze gesi na sumu(sio sumu kiviiile ni vile tu kama chakula kilichochacha ni 'sumu').

So kihekima kama ukilitambua hilo inakuwa sio vizuri kuchanganya ndizimbivu na mayai. Hata kama madhara ni kujambajamba sana kwa nini tu usiwe mwanadamu mwenye upendo kuwaepushia adha waliokaribu nawe?

NB: ukiwauliza madaktari wa kawaida wataita 'bullshit' maana haipo kwenye mtaala kuvisoma tabia za vyakula kihiiiivyo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom