Swali: Madhehebu ya wakristo

Swali: Madhehebu ya wakristo

The Boss

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2009
Posts
49,320
Reaction score
117,611
Naomba tujihadhari na mihemko naomba kuuliza kuwa kujua tu niko curious.

Naomba wenye kukashifu mkae pembeni, lengo ni kuelimishana tu.

Swali langu ni hili;

Mtu anaweza kuwa mlokole na still Mkatoliki au Mlutheri?

Je, tunaweza sema mtu anasali kwa Gwajima au TB Joshua but still Mkatoliki au Mlutheri?

Je, Gwajima yeye binafsi anaweza kuwa Mkatoliki pia au Mlutheri?
 
Nijuavyo mimi, madhehebu yote ya kikristu, ukiondoa Roman Catholic, yanaitwa Protestants. Sasa Ukiwa Mkatoliki (kama mimi) hauwezi at the same time ukawa unaprotest against Catholic church, yaani a protestant. Sana sana utakuwa muhudhuriaji tu kwa upande mmojawapo. Hili jibu ni kwa mujibu wa mimi na linahusu Ukatoliki vs Ulokole. Kuhusu Ulokole vs other protestant churches watakuja wajibu wenyewe
 
Nijuavyo mimi, madhehebu yote ya kikristu, ukiondoa Roman Catholic, yanaitwa Protestants. Sasa Ukiwa Mkatoliki (kama mimi) hauwezi at the same time ukawa unaprotest against Catholic church, yaani a protestant. Sana sana utakuwa muhudhuriaji tu kwa upande mmojawapo. Hili jibu ni kwa mujibu wa mimi na linahusu Ukatoliki vs Ulokole. Kuhusu Ulokole vs other protestant churches watakuja wajibu wenyewe


So ni sawa kwa mkatoliki kuhudhuria ibada kwa Gwajima au TB Joshua?
na still akawa mkatoliki?
 
Naomba tujihadhari na mihemko ...
naomba kuuliza kuwa kujua tu niko curious

Naomba wenye kukashifu mkae pembeni..lengo ni kuelimishana tu..

Swali langu ni hili...

Mtu anaweza kuwa mlokole na still mkatoliki au mlutheri?

Je tunaweza sema mtu anasali kwa gwajima au TB Joshua but still mkatoliki au mlutheri?

je Gwajima yeye binafsi anaweza kuwa mkatoliki pia au mlutheri?

Anayeokoa ni Yesu Kristo pekee, sio Martin Luther, Pope, Gwajima, au mwingine yeyote maana hakuna Jina lingine tulilopewa wanadamu chini ya mbingu litupasalo kuokolewa kwako ILA Jina la Yesu pekee.
 
Anayeokoa ni Yesu Kristo pekee, sio Martin Luther, Pope, Gwajima, au mwingine yeyote maana hakuna Jina lingine tulilopewa wanadamu chini ya mbingu litupasalo kuokolewa kwako ILA Jina la Yesu pekee.

Hujanijibu swali bado
 
Swala ni wenye 'MOYO SAFI' wala sio udhehebu. Ukimkiri na kumpokea kuwa bwana na mokozi wako(ukaacha njia zako mbaya) utakuwa umeokoka, tafuta penye mafundisho mazur go ahead
 
So ni sawa kwa mkatoliki kuhudhuria ibada kwa Gwajima au TB Joshua?
na still akawa mkatoliki?
Nikirejea mafundisho niliyopata, kama hakuna kanisa la Kikatoliki lililo karibu, Mkatoliki anaruhusiwa kuhudhuria ibada ya kanisa la Anglican, na kama Anglican hawapo eneo hilo, anaruhusiwa kuhudhuria ibada ya Lutheran, na yote hayo with a condition that hatakiwi kushiriki sakramenti zao (kama zipo), bali kusali tu. Other Protestant churches kama za kilokole hairuhusiwi kwani wamekuwa too critical kwa RC kuliko hata waasi wa mwanzo (Lutheran & Anglican)
 
Mtu anaweza kuwa mlokole na still mkatoliki au mlutheri?

Jibu ndiyo maana mlokole ni mtu aliyeamini moyoni na kumkiri Yesu Kristo kwa kinywa chake ya kuwa ni BWANA na ya kwamba Mungu alimfufua katika wafu

Je tunaweza sema mtu anasali kwa gwajima au TB Joshua but still mkatoliki au mlutheri?

Jibu ndiyo

je Gwajima yeye binafsi anaweza kuwa mkatoliki pia au mlutheri?

Jibu hawezi kuwa mkatoliki wala mlutheri yeye ni pentecostalism
 
Katika kusoma kwangu biblia sijawahi kukutana na hayo maneno "Mlokole, mlutheri, mkatoliki, Muanglican, Wa Gwajima nk" kama substitute ya wafuasi wa Yesu. Nimekutana na Neno moja tu kama Subsitute na liko kwenye maandiko ya biblia..."Na wanafunzi waliitwa WAKRISTO kwanza hapo Antiokia." -Matendo ya Mitume 11:26 ... Ukisoma mistari ya nyuma utagundua kuwa Jina hilo walipewa na gentiles likiwa na maana, "Hawa ni wafuasi/watu wa Kristo, au wanatenda kama Yesu Kristo." Hivyo basi mtu yeyote ambaye hatendi kama Kristo huyo si Mkristo ... Hizo titles zingine sijui mlokole etc hazina maana, yatosha kuitwa Mkristo kama utafahamu uzito na maana yake...!
 
Kajamaa kanazunguuka, Swali lako ni Dk. Slaa kusali kwa Gwajima kunamuodolea ukatoliki wake?? Idiot
 
Katika kusoma kwangu biblia sijawahi kukutana na hayo maneno "Mlokole, mlutheri, mkatoliki, Muanglican, Wa Gwajima nk" kama substitute ya wafuasi wa Yesu. Nimekutana na Neno moja tu kama Subsitute na liko kwenye maandiko ya biblia..."Na wanafunzi waliitwa WAKRISTO kwanza hapo Antiokia." -Matendo ya Mitume 11:26 ... Ukisoma mistari ya nyuma utagundua kuwa Jina hilo walipewa na gentiles likiwa na maana, "Hawa ni wafuasi/watu wa Kristo, au wanatenda kama mkristo." Hivyo basi mtu yeyote ambaye hatendi kama Kristo huyo si Mkristo ... Hizo titles zingine sijui mlokole etc hazina maana, yatosha kuitwa Mkristo kama utafahamu uzito na maana yake...!

Wapo wakristo walokole hawaruhusiwi kuwa na madhehebu mengine...
 
Mtu aliyeenda kwenye ulokole na kushiriki kikamilifu, sio kusikiliza mara moja moja, hawezi tena kupokea sakramenti kwenye katoliki. Na akitaka kurudi hupata mafundisho ya sakramenti upya (isipokua ya ndoa na ubatizo anabakia nazo) ili aweze kushiriki. Kwa anayeenda mara mojamoja kusikiliza lakini hatoi zaka wala kushiriki mambo mengine ni mtazamaji tu hazuiliwi
 
Wapo wakristo walokole hawaruhusiwi kuwa na madhehebu mengine...
Ni kweli; Ni vyema mtu akawa na sehemu ya kukutania na wenzake ktk Imani (Fellowship) & akawa na Mchungaji wa kumlea kiroho. Lakini sio afya kiimani kufungwa katika namna ya kujifunza. Mimi wazazi wangu wote ni Wakristo & walikuwa wanasali ktk denominations tofauti. Mimi naingia popote pale, coz msingi wa Neno/Imani ni mmoja. Lengo ni kujifunza zaidi...! Hao wanaobaguana utafikiri ni Imani tofauti, inabidi warudi wayachunguze maandiko vizuri.
 
Kajamaa kanazunguuka, Swali lako ni Dk. Slaa kusali kwa Gwajima kunamuodolea ukatoliki wake?? Idiot

Sijui kama Slaa anasali kwa Gwajima..
nimeuliza baada ya kuona picha za Lowassa na Magufuli kwa TB Joshua
halafu tunaambiwa ni RC na Lutheran...nilifikiri ni walokole
 
My dear
Ulokole sio dini wala dhehebu.
Ni hali ambayo baadhi ya watu hujitangazia kuwa wako ktk hali tofauti ya kiimani kuliko wengine. If that is the case then hata mkatoliki au mlutheri anaweza kujiita mlokole. Waingereza wanawaterm as born again Christians. Who is not is the matter of debate.

Haya makanisa ya watu mara nyingi ni ministries yaani vituo vya huduma maalumu. Wengine inakuwa huduma ya kufunguliwa aka delivarence kama SCOAN.
Madhehebu mara nyingi yanakuwepo kila sehemu lkn ministries ndio utasikia kwa kakobe.

Kama hivyo ndivyo mkatoliki anaweza kwenda kwenye huduma say kwa mwakasege lkn kama ni jumapili basi anatakiwa aanze kushiriki misa kanisani kwake.

Nilishaenda kwa T.B Joshua, kwa Mwakasege, na huduma mbali mbali Emaus Catholic Charismatic Center
 
Back
Top Bottom