Mnyamahodzo
JF-Expert Member
- May 23, 2008
- 1,935
- 1,006
Jakaya Kikwete alipochaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano 2005 mwishoni, mwaka 2006, Januari, mwanzoni kabisa alitangaza Baraza la Mawaziri (ambalo hadi sasa ndilo pekee liliovunja rekodi ys kubwa kupita yote toka Uhuru wa Tanganyika, Mapinduzi ya Zanzibar, kuundwa kwa Tanzania ).
Siku alipokuwa anatangaza Baraza hilo kuna maeneo alikuwa makini (serious) na mengine alifanya mizaha, mfano pale alipomwita Steven Wassira, "Tyson" huku akiwa anacheka.
Alipokuwa anataja jina la Dr. Asha-Rose Migiro alibadilika usoni kidogo, kupata haiba siyo ile ya utani. Kilichofuata ni kutamka " usizime simu yako, ninaweza kukupigia wakati wowote hata usiku".
Swali, kwanini Rais Kikwete alitamka hadharani akiwa na haiba ile mara tu alipotamka jina la Dr Asha- Rose Migiro, tena kwa Migiro pekee?
Ikumbukwe, awali Migiro alikuwa ni Waziri wa Wizara ya Maendeleo ya Wanawake, Jinsia na Watoto ktk Serikali ya Rais B. Mkapa; anajua utendaji kazi Serikali.
Siku alipokuwa anatangaza Baraza hilo kuna maeneo alikuwa makini (serious) na mengine alifanya mizaha, mfano pale alipomwita Steven Wassira, "Tyson" huku akiwa anacheka.
Alipokuwa anataja jina la Dr. Asha-Rose Migiro alibadilika usoni kidogo, kupata haiba siyo ile ya utani. Kilichofuata ni kutamka " usizime simu yako, ninaweza kukupigia wakati wowote hata usiku".
Swali, kwanini Rais Kikwete alitamka hadharani akiwa na haiba ile mara tu alipotamka jina la Dr Asha- Rose Migiro, tena kwa Migiro pekee?
Ikumbukwe, awali Migiro alikuwa ni Waziri wa Wizara ya Maendeleo ya Wanawake, Jinsia na Watoto ktk Serikali ya Rais B. Mkapa; anajua utendaji kazi Serikali.