Mwenzenu nimeulizwa hili swali na watoto wangu niimeona ni vema kama nikipata msaada wenu kwani kwangu lilikuwa swali gumu kidogo. Swali lasema hivi:- Hivi kwa nini viumbe hai vyote vizaliwapo havina meno na baada ye huota meno? Na kwa mfano binadamu, baada ya kukua na kufikia miaka 4 mpaka labda 13 meno ya utatoni hutoka na kuota mapya. Na halafu jinsi wazeekavyo hupoteza meno yote. hivi ni kwanini?