Swali kwa wanawake na wanaume wazoefu

Swali kwa wanawake na wanaume wazoefu

Wanawake wanatupiwa lawama wakati wote kwa kuwa ule mshahara wa kuvunja amri ya sita unaonekana physically kwao kwa ile mimba.Imetokea mara nyingi uchumba umevunjika kwa msukumo wa familia au marafiki eti kwa vile binti alikuwa na historia ya kuwa na wanaume wengi wakati huohuo huyo mwanaume siyo clean kihivyo.
Mfano mzuri upo kwa madenti wa kike,huwa wanafukuzwa shuleni na hata nyumbani wakipata mimba na wakati mwanaume aliyempa mimba ametulia tu na ndio kwanza anapongezwa eti kidume cha mbegu.mfano mwingine ni pale inapotokea mwanaume amepata safari ya kimasomo nje ,akifika huko anabadilisha wanawake atakavyo,na itokee mkewe akajaribu hata mara moja na kupanda mimba utasikia kasheshe yake.
Na hata hiyo bikra zamani katika makabila walikuwa wanaangalia kwa binti tu na sio mwanaume.Yani wanakuwekea mashangazi hiyo siku ya kuolewa wakukague usipokutwa nayo ni fedheha kwa familia yako yote na mwanaume hawamuangalii kama na yeye ni bikra.
kwa hayo huoni kuwa hakuna balance hapo katika hilo swala?Kama wanaume wangekuwa wanabeba mimba nao ingekuwa rahisi kuwakamata wasikane pale wanapoharibu.

bikira ya kiume inachunguliwa vipi?
 
Watu wanaanza huo mchezo mapema. Tunapenda kuonja au kuonjwa ili atakapoolewa au kuoa asionekane mgeni katika mambo ya sita kwa sita.
 
Asante mkuu kwa maoni yako/swali lako.
Je umewahi fikiria kwamba wanawake wengi wanatengeneza bikira?
na kwamba wanawake wengi wanawdanganya waume wao kwamba hawajakutana na wanaume kumbe danganya toto?
na kwamba wanaume ni waaminifu zaidi kusema ukweli wa historia ya mapenzi yake kuliko walivyo wanawake?

Naomba na hayo muyaangalie wana-jamii na kutoa uzoefu wenu.
 
Asante mkuu kwa maoni yako/swali lako.
Je umewahi fikiria kwamba wanawake wengi wanatengeneza bikira?
na kwamba wanawake wengi wanawdanganya waume wao kwamba hawajakutana na wanaume kumbe danganya toto?
na kwamba wanaume ni waaminifu zaidi kusema ukweli wa historia ya mapenzi yake kuliko walivyo wanawake?

Naomba na hayo muyaangalie wana-jamii na kutoa uzoefu wenu.


Kama hivi ndivyo..basi kuna walakini somewhere.Kwanini wanawake wafanye hivi?.... inaonyesha kuna nguvu fulani inawasukuma wanawake kufanya hivyo....ONDOENI HIYO NGUVU na kila kitu kitakuwa sawa.
 
Kama hivi ndivyo..basi kuna walakini somewhere.Kwanini wanawake wafanye hivi?.... inaonyesha kuna nguvu fulani inawasukuma wanawake kufanya hivyo....ONDOENI HIYO NGUVU na kila kitu kitakuwa sawa.

Hivi wa kuiondoa hiyo nguvu ni wanaume au wanawake wenyewe? Je hiyo nguvu iko kwa wanawake pake yao? Na kama iko pia kwa wanaume, nani aliiondoa kwao?
 
Yote tu ni fedheha babu Asprin sijaona ushujaa wowote hapo,mmegaji na mmegwaji wote ni yale yale tu.
Ukweli utabakia kuwa ukweli daima. Mbona sisi hatuogopi kusema tukimega? Au kumega ni ushujaa na kumegwa ni fedheha?
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom