Habari JF peoples!
Je ni lazima kumuandika mme/mke wako kwenye simu yako iwapo namba yake unaijua kwa kichwa? Yaani ukitaka kuwasiliana nae una dial tu namba zake kutoka kichwani? Kama kuna umuhimu wa kuisevu ni upi?
Hahaaaaa NN gud reply!
Umuhimu upo. Chukulia kwa mfano umepatwa na dharura, tuseme una kifafa na umeanguka sehemu ambayo hakuna anayekujua. Wasamaria wema wanakuja na kuanza kukupa msaada. Wanaiona simu yako na kuanza kuangalia orodha ya uliowahifadhi.
Wanaona jina la Ashura ambalo umelihifadhi kama 'Ashura - mke wangu'. Wanampigia na kumtaarifu yaliyokupata. Hapo huoni tu umuhimu wake?
NN wewe mzoefu sana utakuwa hata umri unanizidi nakukubali mzee
Du! Mi nimeweka jina lake tu, kumbe niongeze na title ili wakati wa shida atambulike kwa urahisi.
Thanx NN
Kwa kweli sina uzoefu wowote na wala kiumri si mkubwa kama baadhi ya watu wadhaniavyo.
Napenda tu kuongozwa na common sense na niko realistic na practical katika mienendo yangu yote.
Mkuu sijasema una umri mkubwa. Nimesema una umri kunizidi mzee maana mimi sikuwaza ulichoandika nimekuelewa
Unachotakiwa kufanya ni kuwa na orodha ya watu kadhaa ambao - in case of emergency - ndo utapenda wafahamishwe.
Unasave jina kwenye simu yako halafu mbele yake unaandika ICE, kwa mfano, Nyani Ngabu - ICE, Companero - ICE, etc.
ICE hapo inasimama badala ya In Case of Emergency.