Swali kwa Mungu (Allah)

Swali kwa Mungu (Allah)

Swali la kwanza:

Kwenye kitabu chako cha Qur-an, unasifia kuwa ni kitabu ambacho hakiwezi kubadilishwa maneno yake na maudhui yake Abadan Abadan, je ilikuwaje ukaanza na kushusha kitabu chako cha INJILI ambacho kiliweza kubadilishwa kiurahisi?

Swali la pili:
Kwanini katika kitabu chako cha Qur-an umeweka mkatazo mkubwa kuwa (hauzai wala hauzaliwi wala hauna mshirika) hii imeonyesha kuwa unachukua sana watu wakisema kuwa unazaa na una mshirika, je kwanini usiweke hilo na katika injili, zaburi na torati?

Swali la tatu:

Umesema katika Qur-an kuwa swala yetu na Ibada zetu hazikuongezei chochote wala havikupunguzii chochote katika ufalme wako je kwanini unaonyesha kuchukia sana sisi tunapotenda dhambi?, au madhambi yetu kuna kitu yanapunguza katika ufalme wako?,
Stimu zimelipiwa
 
Kitabu chochote kinabeba lugha na utamaduni wa mwandishi au jamii iliyomkuza mwandishi. Hakuna namna ambayo kitabu kinaweza kutafsiriwa kwenye lugha yenye utamaduni tofauti na maana ikabaki ile.ile100% mfano kwenye kingereza hakuna kuoa na kuolewa , ila kwenye kiswahili ipo. Na mambo mengine mbalimbali, pia kazi iliyotafsiriwa inaweza kiamwezwa na itikadi za mfasiri. Na kupotosha maana iliyokusudiwa
 
Qur'an Tukufu imeshazungumzia watu wanaopinga uwepo wa Mwenyezi Mungu na wanaokataa Qur'an kwa kudai ni hadithi za zamani. Aya nyingi zinaelezea suala hili. Moja ya aya maarufu ni:


Surat Al-Anfal (8:31):


"Na wanapo somewa Aya zetu husema: 'Tumeshasikia! Lau tungelitaka, sisi pia tungezua maneno mfano wa haya. Hayakuwa haya ila ni hadithi za watu wa zamani.'"





Pia, Qur'an inasema katika:


Surat Al-Mutaffifin (83:13):


"Anapoisomewa Aya zetu, husema: 'Haya ni hadithi za watu wa zamani!'"





Na Mwenyezi Mungu anasema kuhusu watu hawa katika:


Surat Al-Baqarah (2:6-7):


"Hakika wale waliokufuru, ni sawa kwao ukiwaonya au hujawaonya, hawaamini. Mwenyezi Mungu amepiga muhuri juu ya nyoyo zao na masikio yao, na mbele ya macho yao pana kifuniko; na watapata adhabu kubwa."





Kwa ujumla, Qur'an inaeleza kwamba watu hawa:


Wanakanusha kwa kiburi na ujeuri, si kwa kukosa ushahidi.


Wanadai kuwa Qur'an ni hadithi za zamani ili kuhalalisha ukaidi wao.


Wamefungwa mioyo na macho yao, hivyo hawawezi kuelewa au kuamini.
 
Back
Top Bottom