Sura mbili za Lissu, kabla na baada ya kulamba asali

Kiturilo

JF-Expert Member
Sep 27, 2021
709
2,858
Nimepitia maktaba yangu ya mambo ya siasa nimegundua pasi na shaka siku Tundu Lissu mwaka 2014 akikutana na Tundu Lissu wa mwaka 2022 'watauana' .

Tundu (2014) hakuwa kwenye gubu. Alikula kiapo asilani hatochangamana na Lowassa na team yake. Ni Tundu aliyepinga kwa namna yoyote ile Raisi wa nchi kusafiri nje ya nchi kiasi cha kumuita JK mtalii. Aliamini kuwa ili nchi inufaike na rasilimali ni lazima mikataba ivunjwe bila kusita kwani aliamini Barrick, wamiliki wa vitalu vya uwindaji n.k wanaiba hivyo wataifishiwe. Alitumia vema jukwaa la Leat kufikisha ujumbe wake.

Tundu (2022) ni mwenye unyenyekevu mkuu wa wazungu na wanyonyaji, pia yupo radhi kutoa ushirikiano kwa maadui wa taifa ili tushindwe. Anaamini bila wazungu yeye na wenzake hawawezi kushika dola. Yupo radhi nchi iingie machafuko ili wapate fursa ya kuundwa serikali ya umoja wa kitaifa ili na yeye siku moja awe kiongozi wa serikali.

Hakika, orodha ni ndefu lakini kama ikatokea Tundu (2014) akikutana na Tundu (2022) 'watauana'.

Nitaendelea kuwaletea Mbowe, Lema, Msigwa nk wa mwaka 2014 jinsi watakavyogombana na wale wa mwaka 2022.

Karibuni
 
Mh Mbowe wa sasa si yule kabla hajapelekwa mahabusu kwa kosa la ugaidi.

Mh Lissu wa sasa si yule kabla hajalipwa mafao wake kama mbunge mstaafu.

Wote kwa pamoja hawana ajenda kwa ajili ya watoto wetu na wajukuu zetu kama ilivyo kwa CCM.

Mission accomplish. VITA WALIYOPIGANIA IMEKWISHA.

Nilichojifunza siasa ni moja tu ya njia ya kujinufaisha binafsi na familia yako.

Naamini kwenye kikao chake cha kwanza Mbowe na Mama aliulizwa shida yako nini/ unataka nini. Yeye akajibu nataka kuliowa fidia hasana aliyoipata baada ya kuvunjiwa ofisi yake. Na kwamba asipopewa fidia atakomaa na katiba mpya. Na baada ya kufanikisha hill ndipo akawaalika wasadizi wake kwa ajili ajenda ya chama bila kulazimisha/ kushinikiza.

Nasikia kwa mbali Lissu na Mbowe wakinijibu mzee nawe Fanya yako uwapatie watoto wako Mahitaji ya msingi vinginevyo utapata Tabu Sana
 
Sawa Mkuu ila Fanya Kazi uwapatie watoto wako Mahitaji ya msingi vinginevyo Hutapata Tabu Sana.
Kisa tu kawataja hao mabwana shamba sio? Unadhani nani hafanyi kazi au unataka tufanye kama yako ndio ujue tunafanya kazi?

Nani amekwambia mleta mada ana watoto? Ukute wewe ndo unataabika. Huna uwezo wa kuipigania chadema wewe.
 
1654330981723.png
 

Attachments

  • 2878995_images_9.jpeg
    2878995_images_9.jpeg
    35 KB · Views: 22
Kiongozi yeyote wa kisiasa anapigania njaa zake, ndio lengo la msingi la kufanya saisa, hayo mengine sijui kutafuta usawa sijui uongozi bora huwa ni extra tu. Huwa nawaangalia tu vijana wadogo wanatumiwa kupush agenda na kushabikia kwa hisia kali na hawafaidiki na chochote, wanakujaga kushtuka badae sana
 
Huwezi tumia nguvu kummaliza mpinzani wako tumia pesa utambomoa, nguvu ni gharama utatumia pesa nyingi Sana na still utashindwa huku umepoteza pesa nyingi Sana na matokeo sifuri zaidi ya kumjenga zaidi mpinzani wako. Hakuna mtawala yeyeto duniani aliyewahi Pambana na watu na akawashinda zaidi ya yeye kufa kwa kuuwawa au maradhi ya moyo.

Mfanye adui kuwa rafiki Ili ummalize.

Mtu yeyeto mweusi ni mkate mbele ya chai, mtu masikini Katu hawezi kuwa mwanasiasa bora.

Pesa huwa inaficha aibu mtu akipiga Sana kelele kukunyima usingizi muite pembeni mpe chai, kisha muingize kwenye payroll kila mwezi afiche aibu ya njaa, atopiga tena kelele zaidi atabweka kutimiza wajibu Ili aonekane yupo nao.
 
Kiongozi yeyote wa kisiasa anapigania njaa zake, ndio lengo la msingi la kufanya saisa, hayo mengine sijui kutafuta usawa sijui uongozi bora huwa ni extra tu. Huwa nawaangalia tu vijana wadogo wanatumiwa kupush agenda na kushabikia kwa hisia kali na hawafaidiki na chochote, wanakujaga kushtuka badae sana
Siasa za Tanzania ni za maji taka, nilisha jitoa kushabikia.
 
Mama umefanya vizuri sana kumlipa Lisu haki zake na kumfutia kesi zake zote hapo ushammaliza kwa gharama nafuu atakuonea aibu.

Mbowe nae mrudishie bilicana yake tukakumbushie ujana. Mrudishie mali zake zote.

Ukifanya hivyo umewamaliza.

Vita ni upumbavu havijawahi leta majibu, mtapigana wee at the end lazima mrudi mezani tena
 
Mama umefanya vizuri sana kumlipa Lisu haki zake na kumfutia kesi zake zote hapo ushammaliza kwa gharama nafuu atakuonea aibu.
Mbowe nae mrudishie bilicana yake tukakumbushie ujana. Mrudishie mali zake zote.
Ukifanya hivyo umewamaliza.
Vita ni upumbavu havijawahi leta majibu, mtapigana wee at the end lazima mrudi mezani tena
Mali ya NHC arudishiwe mbowe?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimepitia maktaba yangu ya mambo ya siasa nimegundua pasi na shaka siku Tundu Lissu mwaka 2014 akikutana na Tundu Lissu wa mwaka 2018 'watauana' .

Tundu (2014) hakuwa kwenye gubu. Alikula kiapo asilani hatochangamana na Lowassa na team yake. Ni Tundu aliyepinga kwa namna yoyote ile Raisi wa nchi kusafiri nje ya nchi kiasi cha kumuita JK mtalii. Aliamini kuwa ili nchi inufaike na rasilimali ni lazima mikataba ivunjwe bila kusita kwani aliamini Barrick, wamiliki wa vitalu vya uwindaji n.k wanaiba hivyo wataifishiwe. Alitumia vema jukwaa la Leat kufikisha ujumbe wake.

Tundu (2018) ni mwenye unyenyekevu mkuu wa wazungu na wanyonyaji, pia yupo radhi kutoa ushirikiano kwa maadui wa taifa ili tushindwe. Anaamini bila wazungu yeye na wenzake hawawezi kushika dola. Yupo radhi nchi iingie machafuko ili wapate fursa ya kuundwa serikali ya umoja wa kitaifa ili na yeye siku moja awe kiongozi wa serikali.

Hakika, orodha ni ndefu lakini kama ikatokea Tundu (2014) akikutana na Tundu (2018) 'watauana'.

Nitaendelea kuwaletea Mbowe, Lema, Msigwa nk wa mwaka 2014 jinsi watakavyogombana na wale wa mwaka 2018.

Karibuni
Kwani kinana na nape wa 2014 na wale wa 2018 wanafanana?.....SSH je?
 
Back
Top Bottom