1) Mayai ya kuku wa kienyeji mawili, unatowa ute kinabaki kiini tu (manjano).
2) Samli safi ya Ng'ombe ya kienyeji na si ya makopo. Vijiko viwili vya chakula.
3) Sukari guru vidonge viwili saizi ya kijiko cha chakula.
4) Asali vijiko viwili vya chakula.
Changanya hivyo vitu pamoja na kula vyote kabla hujala kitu asubuhi, usile kitu mpaka saa sita mchana, hata maji usinywe. Saa sita mchana funguwa kinywa kwa vipande viwili au vitatu vya matikiti (ukipata ya kienyeji ndio mazuri zaidi). Baada ya kula matikiti kaa saa moja nzima usile kitu, baada ya hapo kula upendacho, avoid vyakula vya mafuta.
Endelea na hiyo tiba kila siku, zisipinguwe siku 90 lakini ukiona ndani ya siku hizo 90 mambo yamebadilika unaweza kusitisha na kutazama hali ikoje.
Husninyo, unasemaje kuhusu hii tiba, uliwahi kuisikia?
Cupid na Erector hazipatikan mkubwa, hakuna dawa nyingine itakayonisaidia?
Tafuta daktari mwingine kwa ushauri zaidi, pia jaribu na supu ya pweza.....lol...
tehtehe.. no commentpole mkuu! Sometimes konyagi inasaidia sana! Mimi ninayoexperience frm my b.f! Nakuhakikishia kwa hilo!
Katavi hii supu ya pweza kiboko nimewahi kufululiza mwezi mzima nakunywa, si mchezo kule kwenye winchi unaweza kufunga mzigo wa kilo tatu ukaubeba kwa nusu saa bila kuchoka, hii supu siitaki tena unaweza kufanya mauaji bila kukusudia.
Msaada hapo mazoezi ya kegel ndiyo yapi?
Ndugu zangu wanaJF hii imekuwa siri yangu ya muda mrefu bt leo naiweka wazi, ikiwezekana mnipe ushauri. Mwenzenu kwa muda sasa nimekua nikipatwa na yale matatizo ya kiume wakati wa mambo fulani, kifupi huwa nachemsha. Nilienda hospital kwa matibabu dokta akanishauri nitumie super shaft kwan huwa inasaidia kiasi fulani kuongeza nguvu. Nimezitumia sana sana bt hazifanyi kazi kabisa, tatizo lipo pale pale na huzuni zangu zinazidi kukua siku hadi siku... Ninahofu ya kukimbiwa na mpenz wangu, hapa niliposina jinsi, naombeni ushauri wenu juu ya hili..