Sumu inazuiwaje na maziwa

Sumu inazuiwaje na maziwa

ashidodi

JF-Expert Member
Joined
Sep 4, 2016
Posts
291
Reaction score
341
Poleni na majukumu wana jamii wenzangu,

naomba kufahamishwa zaidi kwa hiki ambacho nimezoea kukiona bila kukifuatilia kwa undani, maziwa huzuiaje madhara ya sumu mwilini?

Nawasilisha

IMG_20170819_231200.jpg


MAJIBU YALIYOTOLEWA NA WADAU
Ni kwa namna gani MAZIWA hufanya kazi kupunguza makali ya sumu mwilini ?

Katika ukurasa wangu huu nitakua nikizungumzia masuala mbalimbali yanayohusu mambo kadha wa kadha yanayohusu mifugo/wanyama, ufugaji na wafugaji. Nitaelezea masuala kadhaa yanayohusu, historia, tamaduni, tabia, teknolojia na mambo ya kustaajabisha ya mifugo na mazao yake hali kadhalika wafugaji.

JE, MAZIWA YANAFANYAJE KAZI KUPUNGUZA SUMU ? JE, YANAPUNGUZA UWEZO WA DAWA MWILINI ?

Maziwa ni kimiminika cheupe ambacho huzalishwa kutoka kwenye kiwele cha mamalia jike kwa ajili ya chakula cha mtoto wake mara baada ya kuzaa.

Maziwa dhidi ya sumu, dawa na pombe;

Kwa asilimia kubwa maziwa ni protini, umbo la protini linaweza kuharibiwa (protein denaturation) kwa joto, pombe, asidi, besi au chumvi ya metali nzito (salts of heavy metals).

Asilimia kubwa ya sumu zilizopo ni chumvi za metali nzito hasa Mekyuli/Zebaki na Fedha (Lead). Unapokua umekunywa sumu za aina hiyo kisha ukanywa maziwa, metali zilizopo kwenye sumu zitakwenda kwenye maziwa kuchanganyikana ili kuiharibu protini iliyopo kwenye maziwa. Kwa kufanya hivyo kiwango cha sumu amabacho kingeudhuru mwili kinapungua (badala ya sumu kuudhuru mwili inayadhuru/inachanganyikana na maziwa). Kutilia mkazo nizungumze kakimombo hapa “the poison acts on the protein in milk rather than on the proteins of various body parts”
Baada ya hapo mtu anatapika ili kuondoa sumu iliyochanganyika kwenye yale maziwa.

Kwa upande wa dawa (ambazo ndani yake kuna asidi,besi au matali nzito) na pombe, maziwa yanapunguza nguvu ya dawa na pombe hiyo kwa kuifanya dawa IYATIBU maziwa na pombe KUYALEWESHA maziwa kuliko mwili au mtu.

Ukiamua kunywa sumu basi fanya hivyo siku amabayo ni zamu yako kukamua na ukiwa baa usimchekelee muuza maziwa utapata hasara.

“RAHA YA BIERI (BIA) KULEWA”

Credit; Kwa Jamaa Fulani Facebook


Sent using Jamii Forums mobile app
 
kuna andiko moja nililiona Facebook linazungumzia hiyo issue, ngoja nikutafutie nilete hapa naamini utapata mwanga
 
Ni kwa namna gani MAZIWA hufanya kazi kupunguza makali ya sumu mwilini ?

Katika ukurasa wangu huu nitakua nikizungumzia masuala mbalimbali yanayohusu mambo kadha wa kadha yanayohusu mifugo/wanyama, ufugaji na wafugaji. Nitaelezea masuala kadhaa yanayohusu, historia, tamaduni, tabia, teknolojia na mambo ya kustaajabisha ya mifugo na mazao yake hali kadhalika wafugaji.

JE, MAZIWA YANAFANYAJE KAZI KUPUNGUZA SUMU ? JE, YANAPUNGUZA UWEZO WA DAWA MWILINI?
Maziwa ni kimiminika cheupe ambacho huzalishwa kutoka kwenye kiwele cha mamalia jike kwa ajili ya chakula cha mtoto wake mara baada ya kuzaa.

Maziwa dhidi ya sumu, dawa na pombe;

Kwa asilimia kubwa maziwa ni protini, umbo la protini linaweza kuharibiwa (protein denaturation) kwa joto, pombe, asidi, besi au chumvi ya metali nzito (salts of heavy metals).

Asilimia kubwa ya sumu zilizopo ni chumvi za metali nzito hasa Mekyuli/Zebaki na Fedha (Lead). Unapokua umekunywa sumu za aina hiyo kisha ukanywa maziwa, metali zilizopo kwenye sumu zitakwenda kwenye maziwa kuchanganyikana ili kuiharibu protini iliyopo kwenye maziwa.

Kwa kufanya hivyo kiwango cha sumu amabacho kingeudhuru mwili kinapungua (badala ya sumu kuudhuru mwili inayadhuru/inachanganyikana na maziwa). Kutilia mkazo nizungumze kakimombo hapa “the poison acts on the protein in milk rather than on the proteins of various body parts”
Baada ya hapo mtu anatapika ili kuondoa sumu iliyochanganyika kwenye yale maziwa.

Kwa upande wa dawa (ambazo ndani yake kuna asidi,besi au matali nzito) na pombe, maziwa yanapunguza nguvu ya dawa na pombe hiyo kwa kuifanya dawa IYATIBU maziwa na pombe KUYALEWESHA maziwa kuliko mwili au mtu.

Ukiamua kunywa sumu basi fanya hivyo siku amabayo ni zamu yako kukamua na ukiwa baa usimchekelee muuza maziwa utapata hasara.

“RAHA YA BIERI (BIA) KULEWA”

Credit; Kwa Jamaa Fulani Facebook
 
NDIO walewale,
Eheee hapo sawa nimepata mwanga,ila bado kwenye kutapika, MTU hutapishwa au ile reaction ya maziwa na sumu ndo humtapisha? Asante sana#ndio walewale

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Action ya maziwa ni kweny sumu zenye asili ya Asidi tu, hvyo bac kaz yke kubwa ni kunutralize ile acid kuwa chumv na maji.. Mbadala wa maziwa ni MgOH solution.
 
Maziwa ni protein hivyo yanakuwa denatured na hiyo sumu na hivyo kuzuia ile sumu kuingia mwilini.
 
Maziwa yana madini mengi ya calcium. Sasa calcium huungana na sumu na kutengeneza complex salts/chumvi tata ambazo haziwezi kunyonywa kuingia kwenye damu kutoka tumboni. Ndiyo maana haishauriwi kunywa maziwa na baadhi ya dawa kama tetracycline au ciprofloxacin sababu calcium itaungana nazo na kusababisha dawa isinyonywe kwenda kwenye damu.
 
Mtu akinywa vidonge vingi vya ALU mkampa maziwa ndio mnazidi kumuua

Maziwa hu"chelate" sumu na kuizuia isiwe absorbed

Sent using Jamii Forums mobile app
Hii iko tofauti. Maziwa husaidia kunyonywa kwa ALU na inashauriwa unapomeza ALU umeze na maziwa. Sasa mtu akijioverdose na ALU na ukampa maziwa maana yake unamzidishia ALU inayoenda kwenye damu na kumuua.
 
Vp kuhusu maziwa na vumbi au moshi? imekuwa mazoea kwa watu wanaofanya kazi kwenye maeno yenye vumbi au moshi kunywa,je ni kweli maziwa yanasaidia athari zinazo sababishwa na vumbi au moshi?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom