BUBU MUONGEAJI
Member
- May 15, 2013
- 44
- 8
Kuna watu wameshaanza tayari ,nina uhakika watu hawa wanatumiwa.
Wanapinga Rasimu ya Serikali tatu kwa kigezo cha Gharama.
Eti Nchi itakuwa na Gharama Kubwa ku Run na Marais wa Tatu.
Watu kama hawa wanastahili Kukumbushwa kuwa kwa Sasa Nchi ina Ma Rais wa Tano na Wa Tatu wanatokea zanzibar.
Watu hawa wamekuwa wapofu kuona kuwa Tume ya Warioba imependekeza Baraza lenye Ma Waziri wasiozid 15.
Kwa Sasa Baraza lina Zaid ya Mawaziri 45, Mbona hawasemiGharama kubwa za ku Run the Current Baraza la Mawaziri?????
Hawaoni kuwa kwa Kupunguza Baraza la Mawaziri Mpaka 15 tUtakuwa tumeokoa Kiasi kikubwa sana Cha Fedha.
Watu wanaopinga Serikali 3 Hawastahili kuishi Tanzania,
TUSIMAME KUWAPINGA HAWA WACHUMIA TUMBO
tusishabikie serikali tatu kwa maana ya kulinganisha na mfumo mbovu uliopo, tume inabidi kuungwa mkono kwa jambo zuri na si serikali tatu, serikali moja ndio kitu muhimu saana kwa uchumi wa nchi hii.
serikali tatu, ndege za maraisi watatu, ikulu tatu, cabinet tatu, mabunge matatu, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, maspika, hawa watu wakistaafu nini kinatokea! ni kuubaka uchumi wa nchi hii, wananchi wanalipa kodi kwa nguvu zao zote na still watu wachezee pesa. thats non sense. serikali tatu ni upungufu wa fikra na kufikiria kutatua migogoro kwenye katiba. huo ni upungufu wa mawazo chanya kwa nchi yetu na watu wake. Tuwe makini, hakuna barabara za kuunganisha nchi yetu, foleni Dsm zinaua uchumi badala ya kupeleka pesa kule tunataka kuhalalisha ulaji kwenye katiba.
tuwe makini saana katika maoni ya katiba.
serikali tatu ni ubeberu kwa mwananchi mlalahoi