Sumaye apinga SERIKALI TATU

No data no research no right to speak, wa kwanza kuulizwa swali hili alikuwa ni Sumaye ila sikumbuki alikuwa nchi gani ya Ulaya, lakini alikuwa tayari ni Waziri Mkuu mstaafu. nina hakika na hili kwa asilimi 1000.
Acha upuuzi! umekwisha sema hukumbuki ni nchi gani aliongelea,sasa tunauhakika gani kuwa unakumbuka kuwa ni Sumaye au Rais Kikwete?
 
wapo wachumia tumbo wanaona wamepata mbinyo wa maana. ukwel ni kwamba watz weng hawapend kufanya kaz, kujfunza nk.. sasa walitegemea mgongo wa aliyoko magogoni kuendesha familia.. mungu ni mwema sana, lazma tufanye kaz , Sio Kula juu ya migongo yetu. maana kuna maprofesa na madokta na mambumbumbu wanaoish kwa umbeya na fitna tu.,.. no longer at ease!!! huyu SUMAYE ana hak kusema ivo maana maslah yake( ndot za urais) yamekunwa!!
 
hapa piga ua hatutaki serikali tatu ambayo ni mzigo kwetu tunataka serikali moja tu na zanzibar liwe mkoa au jimbo na siyo nchi.
 
Akili ya Sumaye ilishachoka siku nyingi, alishawahi kuhojiwa ni kwa nini Tanzania ni maskini akajibu hata yeye hajui ni kwa nini, imagine miaka 10 kama Waziri Mkuu hujui nchi ni kwa nini maskini ulikuwa unafanya nini kwenye hiyo nafasi?

Rasimu ya katiba mpya ni maoni yetu Wananchi yeye akafie Uyole kama anadhani hizi bado ni enzi za haambiliki.

Aliyeulizwa kwa nini nchi ni masikini akashindwa kujibu ni jk.
 
Serikali tatu kimtazamo wangu kweli ni mzigo kwa wananchi kukatwa kodi ya kuhudumiwa viongoni wake.pia ni njia ya kuwaongezea wakubwa na watoto wao ulaji tu.
 
hapa piga ua hatutaki serikali tatu ambayo ni mzigo kwetu tunataka serikali moja tu na zanzibar liwe mkoa au jimbo na siyo nchi.
Unafahamu kama jambo hilo limemsha nyerere?nani mwengine atakeweza kuifanya z'br jimbo?
 
WAZIRI wa Fedha Dk. William Mgimwa, amesema hajui kwanini Watanzania ni masikini. Amesema kutokana na hali hiyo Wizara yake imeandaa mpango kabambe wa kukabiliana na umasikini, kupitia Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini namba mbili (MKUKUTA II).

Kauli hiyo aliitoa Dar es Salaam jana, alipozungumza na waandishi wa habari, baada ya kuzindua mpango huo ambapo alisema, Serikali kupitia mpango huo itakuwa inafanya kazi ya kufuatilia kero za wananchi moja kwa moja.
 
Kweli kabisa 2naitaji serikali moja2au la sivyo kwa maoni yangu na kwa jinsi ninavyo fikiri mm waiache Zanzibar iende zake 2baki na Tanganyika ye2.
 
Nimemsikia Frederick Sumaye akisema Serikali tatu ni mzigo kwa Tanzania ambayo uchumi wake si mkubwa. Anasema hata waasisi wa Muungano waliliona hilo. Amezungumza akiwa Afrika Kusini.

chanzo: BBC

Angalizo: Nadhani ana hoja

Mzigo ni wa kuchukuliwa. Mbona bado tunambeba (kwa mafao na huduma) yeye hiyo haoni kuwa ni mzigo kwa Taifa?
 
Kuna watu wameshaanza tayari ,nina uhakika watu hawa wanatumiwa.
Wanapinga Rasimu ya Serikali tatu kwa kigezo cha Gharama.
Eti Nchi itakuwa na Gharama Kubwa ku Run na Marais wa Tatu.
Watu kama hawa wanastahili Kukumbushwa kuwa kwa Sasa Nchi ina Ma Rais wa Tano na Wa Tatu wanatokea zanzibar.
Watu hawa wamekuwa wapofu kuona kuwa Tume ya Warioba imependekeza Baraza lenye Ma Waziri wasiozid 15.
Kwa Sasa Baraza lina Zaid ya Mawaziri 45, Mbona hawasemiGharama kubwa za ku Run the Current Baraza la Mawaziri?????
Hawaoni kuwa kwa Kupunguza Baraza la Mawaziri Mpaka 15 tUtakuwa tumeokoa Kiasi kikubwa sana Cha Fedha.
Watu wanaopinga Serikali 3 Hawastahili kuishi Tanzania,
TUSIMAME KUWAPINGA HAWA WACHUMIA TUMBO

Inasikitisha sana kuona hata baada ya siku takribani tano kupita tangu hii rasimu kutolewa bado watu hawajaelewa the whole concept of serikali tatu. tunazungumza baraza limepungua na kusahau kwamba kutakuwa na baraza lingine la Tanganyika kubwa kuliko hilo la muungano.

Na kama humu ndani watu wameshindwa kuelewa, sina hakika kule mfaranyaki na magagula itakuwaje. it is a full confusion.Hongera Warioba kwa kuwachanganya wananchi hata wasomi.
 
mbona mi nakubali serekali tatu: Tanganyika, Pemba na Unguja! Kila mtu na chake yaishe!

Tunahitaji ziwe nne.

Iongezeke na Serikali ya Mafia.

Pia tutoe mwaliko kwa nchi jirani kujiunga na Shirikisho la Tanzania.
 
Msisahau kuna bahari hapo katikati ambayo hutenganisha mabara duniani kote! Muungano wetu ni mpango wa Mungu kweli?
 
Back
Top Bottom