Sumatra yaipiga ban Champion Bus

Sumatra yaipiga ban Champion Bus

Hii ni kufuatia ajali ya basi la kampuni hiyo mkoani Dodoma.Zuio hilo linaanza kesho,litadumu kwa muda usiojulikana kupisha uchunguzi-sumatra.SOURCE TBC TAIFA-habari.
Vijana wa Mtibwa wamejisahau kuchangi Igunga!!!!!!!!!
 
mi mwenyewe nilikuwa nataka niulize kuhusu Sumry....kila mwezi lazima tusikie ajali ya hili bus.....mbona halifungiwi?....
Waifungie kampuni ambayo mtoto wa mkulima (aliyesaliti wakulima) ana hisa nyingi....

Ila watueleze sababu za msingi kufungia kampuni manake uchunguzi wa ajali sidhani kama ni kazi ya siku mbili, ilitakiwa ufanyike uchunguzi wa kitaalam, sio hizi ramli wanazopiga polisi kila siku, halafu ndio waje na hizo adhabu baada ya kujiridhisha kuwa ni uzembe wa kampuni au negligence ktk mambo ya usalama na sio kukurupuka kufungia kampuni. Je ukifungia kampuni bila kuchunguza chanzo na kusuggest namna ya kuzuia itasaidia kupunguza ajali?
 
Uamuzi huu wa sumatra huenda ni kwa sababu Kikwete alikuwa Dodoma na alikwenda kuwatembelea majeruhi hospitali.
 
&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
We unashangaa ya kutofungiwa hood!Vipi SUMRY zilizokuwa zinafululiza kutuchinja?
<br />
<br />
Hapo ndio utaijua serikali ya ccm wanaofanya makosa makubwa hawaguswi,ila wenye tukosa tudogo tudogo wananing'inizwa mpaka basi.
 
Na mohamed trans???,sumry,abood,hood????au kwakuwa haya ni ya warabu????nadhan sumry na mohamed trans wanaongoza,na leo mohamed limeua tena
Hii ni kufuatia ajali ya basi la kampuni hiyo mkoani Dodoma.Zuio hilo linaanza kesho,litadumu kwa muda usiojulikana kupisha uchunguzi-sumatra.SOURCE TBC TAIFA-habari.
<br />
<br />
 
Asante kwa ipembuzi yakinifu,maana juz nbasi la shukran nalo limeua hukohuko njia ya dodoma,
Uamuzi huu wa sumatra huenda ni kwa sababu Kikwete alikuwa Dodoma na alikwenda kuwatembelea majeruhi hospitali.
<br />
<br />
 
Pumbafu zao Sumatra na traffic police wote! Leo basi la Mohamed(sina uhakika kama ni Classic au Trans) limeua watu wanne likitokea Arusha na lenyewe walifungie au? Sasa hv nipo kwenye basi la Mghamba kuelekea kahama kasi yaje inatisha! Dereva wala hajari bamps mbaya zaidi nipo siti ya mwisho kabisa! Jamaa hajaigopi hata Sekenke mwendo ulelue! maaskari wakitusimamisha wanaongea na konda hata ndani hawaingii mambo yanakwisha! Ipo hvi zaidh ya asilimia 78 ya ajari za mabasi ni uzembe wa madereva.Sasa unafungia kampuni moja nyingine inaua utafungia ngapi? Lazima washughulike na madereva.

Hapo kwenye red nafikiri uzembe uko kwa wasafiri. Imagine wewe mwenyewe uko kwenye basi na unadai eti devera anakimbiza ile mbaya. Badala ya wewe mwenyewe kuchukua hatua, unamlalamika dereva ambaye yuko mita chache kutoka kwenye seat yako. Chukua hatua.
 
Serikali iliyo usingiziniiii ndivyo inavyotenda kazi.A WEAK GOV CAN NOT BREED STRONG SERVANTS hiki ndicho kilichopo TZ.Wanasubiri kuzima moto badala ya kuzuiya moto.HAMKA WADANGANYIKA NA WATUNZANIA TOKA GIZANI.
 
Wandugu maamuzi yanayofanywa na wenye mamlaka katika nchi hii yanasikitisha, kama mtakumbuka miaka kadhaa iliyopita baada ya kufululiza kwa ajali wakasema kila basi lazima kuwe na mlango wa dharura nyuma sasa sijui ilke milango ilyokuwa imewekwa ilifanikiwa kupunguza idadi ya ajali au la!, kama hilo halitoshi sasa hivi wameamua kuibadilisha staili na kufungia mabasi kwa ajali. After all kuifungia kampuni sio suluhisho la ajali bali mikakati thabiti.
WAZO LANGU, NAOMBA SUMATRA IFUNGIWE KWA KUWA INASHINDWA KUDHIBITI AJALI.
 
Kuna kitu wenye mabasi wanawashinda hao wanaojifanya wana ban....wakisema kuwa nalipa loan kila mwezi like 10m kunifungia ina maana utanilipia deni langu maana kama makosa na ajali kila kampuni ya bus inafanya ajali na mbona hatuoni kufungiwa???hapo watawafungulia kesho asubuhi!!kama kila ajali kuanzia sasa bus linafungiwa!!!wameanza tar 1 sept?watafute njia mbadala wakishirikiana na Police kuyakagua mara kwa mara....na kujua ubora wa magari!!wanayaachia magari yanapita kila siku nenda rudi!!!kwa nini wasiyasimamishe kwa kigezo cha ubora???Champion kweli ma bus yake yamechoka sana sana sana....wasisubiri yaue wakayakague yakiwa yanapakia pale stand!!
 
poleni sana majeruhi na wale waliopoteza maisha mungu awarehemu mahali pema pepini amina..
 
Kufungia kampuni si suluhisho la kupunguza ajali,Sumatra wanafanya mambo kama watu wasio na elimu kabisa.Ukaguzi huu wangekuwa wanaufanya kabla wajue gari ina hali gani,viwango vya matairi waliyofunga na huduma ndani ya mabasi yenyewe zikoje kama 1st aid na kizimamoto.Wakibaini kuwa mabasi fulani hayakidhi kiwango ndio wayafungie mpaka yatimize vigezo vyote,aidha kuifungia kampuni baada ya ajali halafu kesho yake ingine inachinja watu mnaonekana mko nyuma sana kielimu halafu very hopeless.Kaeni standby kila stendi ya basi kuyabaini mabasi yasiyofaa wasiyaruhusu kuanza safari.Namkumbuka afisa 1 wa sumatra aliwahi kuniambia tukiwa ktk mazungumzo ya kawaida, watu wote wasio na elimu ya kuhudumia wasafiri stendi itafikia tutawaondoa, sasa mi naona wao sumatra ndio hawana elimu bora hata wapiga debe.
 
KWAHIYO SUMRY LIKO BETTER KULIKO CHAMPION KWENYE KUUA RAIA WEMA SIO??

haingii akilini
 
Back
Top Bottom