SUMATRA vipi tena!!!

Mzee

JF-Expert Member
Feb 2, 2011
13,597
5,788
Huwa naangalia sana magari ya Mbagala, Mbezi, G/Mboto n.k, yanajaza sana. Yanazidisha abiria zaidi ya 100%.
Je! Tatizo la usafiri linaruhusu sheria za usafirishaji zisifuatwe? Au wanasubiria litokee lakutokea ili waunde tume?
Kama sheria inaruhusu nchi kavu kuzidisha abiria kutokana na tatizo la usafiri kwanini na majini isiwe hivyohivyo?
Sumatra vipi tena, hatuwaelewi.
Nawakilisha.
 
Kweli hili ni tatizo kubwa sana.Nilijaribu kufuatilia tatizo hili kutaka kuju kwa nini wanafanya hivi miaka ya 2006 .Mambo yalikuwa ni mengi sana.Ila moja kubwa nililoligundua ni kuwa wasimamizi wa usalama barabarani ambao ni traffic wengi wao wanafumbia macho kwa sababu ndio wamiliki wa hivi vyombo.Kwa hiyo hata hivyo ambavyo havilikiwi na wao wanashindwa kuvichukulia hatua madhubuti kutokana na hilo.
 
Back
Top Bottom