tpaul
Platinum Member
- Feb 3, 2008
- 27,198
- 27,822
Wakati nafuatilia uchambuzi wa magazeti kupitia RFA leo asubuhi, nimesikia gazeti/magazeti yakimnukuu makamu mwenyekiti wa bunge la katiba bi samia suluhu akisema kwamba 2/3 ya kura kutoka zanzibar zilizokuwa zikiwaumiza kichwa sasa zimepatikana. Ijapokuwa sikuweza kunasa gazeti lililoandika habari hizo, bila shaka itakuwa mojawapo ya magazeti ya chama au yale magazeti yanayoegemea chama.
Chanzo: RFA
MAONI YANGU
Baada ya UKAWA kuondoka Dodoma suala lililokuwa likiwanyima CCM usingizi ni akidi ya 2/3 kutoka Zanzibar. Kuna uhakika usiopingika kwamba wabunge 16 wanahitajika kutoka Zanzibar ili kutimiza akidi, na wadadisi wa mambo ya siasa wanatathmini kwamba kuna wajumbe 21 kutoka kundi la 201 ambao wanawaunga mkono UKAWA. Sasa hiyo akidi iliyotimia imetoka wapi? CCM watakuwa wamewanunua wajumbe wa UKAWA ili kutimiza akidi, hivyo viongozi wao wanapaswa kuwa makini na usaliti huu. Au huenda wamejiandaa kuchakachua kura ili kulazimisha akidi. Haiwezekani Suluhu aropoke tu bila kuwa na uhakika.
:israel:
Chanzo: RFA
MAONI YANGU
Baada ya UKAWA kuondoka Dodoma suala lililokuwa likiwanyima CCM usingizi ni akidi ya 2/3 kutoka Zanzibar. Kuna uhakika usiopingika kwamba wabunge 16 wanahitajika kutoka Zanzibar ili kutimiza akidi, na wadadisi wa mambo ya siasa wanatathmini kwamba kuna wajumbe 21 kutoka kundi la 201 ambao wanawaunga mkono UKAWA. Sasa hiyo akidi iliyotimia imetoka wapi? CCM watakuwa wamewanunua wajumbe wa UKAWA ili kutimiza akidi, hivyo viongozi wao wanapaswa kuwa makini na usaliti huu. Au huenda wamejiandaa kuchakachua kura ili kulazimisha akidi. Haiwezekani Suluhu aropoke tu bila kuwa na uhakika.
:israel: