Habari wapendwa wooote humu ndani......
Natumai wote tuko kamili saaanaa kama unastress ni kitu cha kawaida ..
Nimegundua, wengiii tunatatizo la kukata tamaa pale tunapowapoteza wale tuliowapenda sanaaa ( wapenzi na dearest wake/waume zetu) na kuhisi hakuna atakaye tokea kama yeye.
Hapo unatokea mtawanyiko wa watu sasa,
1.kuna wale wanaingia kwenye mahusiano mengine kwa kulipa kisasi alichofanyiwa na mtu aliyempenda kwa dhati.Hii huishia kuwaumiza wengine wasio na hatia.
2.kuna wale wanaoamua kuoa/kuolewa kwajili ya kujikinga kutoumia/kumkuta kama yaliyopita.
3.Anaamua kujizira kwa maana anaingia kwenye relationship 100 ndani ya wakati mmoja.
4.kuna sisi ambao we dont feel love kabisaaa mpaka watu wa karibu wanahisi mtu unafanya uchaguzi sana kumbe no affection.
5.kuna wale wanaojikuta wanajiingiza kwenye tabia tofauti kama, alikuwa si mlevi akaamua kupiga gambe la hatari na kujikuta akipoteza uelekeo kabisaaaaa...
Kama kuna niliowasahau naomba mnisaidie kuongezea hapo...
Nyie mliosimama kwenye mahusiano/ndoa zenu na sie wahanga hebu tusaidiane mawazo..
Nini cha kufanya pale unapokuwa umeumia/umeumizwa....ulimwacha mtu unaempenda na kujikuta unaangukia hapo/uliacha...
Let us be serious on this....tusaidiane.
Unayejua huna comment tafadhali soma na kaa kimya sipendi kwenye ishu serious kuleta utani/mawazo ya hafifu.
Div 6 not needed here.