Sukari yapotea Arusha, waliofunga Ramadhani wateseka, serikali baridi

Sukari yapotea Arusha, waliofunga Ramadhani wateseka, serikali baridi

Jembe Jembe

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2016
Posts
757
Reaction score
1,822
Wakati wananchi wakikabiliwa na janga la Corona .. mateso mapya ya ukosefu wa bidhaa muhimu ya sukari yameibuka upya Mara baada ya bidhaa hiyo kuadimika madukani katika jiji la Arusha na majumbani mwa watu tangu wiki iliyopita.

Serikali imelalamikiwa na wananchi wakidai kuwa kwann ipo kimya kuzungumzia suala hilo huku baadhi ya wafanyabiashara walioficha wakiwauzia wananchi kwa siri hadi sh 4500 kilo moja.
 
Wakati wananchi wakikabiliwa na janga LA Corona ..mateso mapya ya ukosefu wa bidhaa muhimu ya sukari yameibuka upya Mara baada ya bidhaa hiyo kuadimika madukani katika jiji la Arusha na majumbani mwa watu tangu wiki iliyopita.

Serikali imelalamikiwa na wananchi wakidai kuwa kwann ipo kimya kuzungumzia suala hilo huku baadhi ya wafanyabiashara walioficha wakiwauzia wananchi kwa siri hadi sh 4500 kilo moja.
Sakata la sukari ni zito, sana na halihitaji nguvu kurishughulikia, hata hao ma RC, DC, wanacheza ngoma wasioijua kwa matamko tu, demand inapokuwa kubwa kuliko supply, ni wazi tu kutakuwa na shida!!!! Ni matokeo ya kufanya mambo ki zima moto!!! Leo waziri anakwambia eti corona imechangia upungufu wa sukari nchini, na mzee wa kuibuka (unatengeneza tatizo, kisha una kuja kulitatua ki zima moto) watu wana kuona shujaa!!! Kuna watu watatolewa KAFARA, ili kutuliza hali, kuongoza watz raha sanaa!!!
 
Kulishugulikia hili tatizo, serikali ingeagiza watendaji wa mitaa kuhakikisha sukari inauzwa kwa bei elekezi, wapewe mamlaka ya kukamata iwapo wanamhisi mtu yeyote kuficha sukari.

Lakini hii kufanywa na wakuu wa mikoa mbele ya camera ni changamoto
 
Ni Kweli mkuu, kwa sasa sukari imepotea kabisa. Hili suala limeshindwa kupatiwa suluhisho la kudumu.
 
ni aibu karne hii na miaka hii kuangaika na sukari eti imeadimika..viongozi wetu mnatuangusha sijui shida ni nini aibu sana mambo mengine..😳
 
Hapa ni kuongeza uwekezaji tu kwenye viwanda vya sukari kwa sababu kitu kuadimika inaonekana wazi kwamba uzalishaji ni mdogo kuliko mahitaji,hivyo kama uzalishaji ukiwa sawia na uhitaji ni wazi bei haiwezi kuyumba ovyo
 
Wakati wananchi wakikabiliwa na janga la Corona .. mateso mapya ya ukosefu wa bidhaa muhimu ya sukari yameibuka upya Mara baada ya bidhaa hiyo kuadimika madukani katika jiji la Arusha na majumbani mwa watu tangu wiki iliyopita.

Serikali imelalamikiwa na wananchi wakidai kuwa kwann ipo kimya kuzungumzia suala hilo huku baadhi ya wafanyabiashara walioficha wakiwauzia wananchi kwa siri hadi sh 4500 kilo moja.
Kilo ya Sukari ni Sh ngapi kwa sasa?
 
Back
Top Bottom