Sugu a.k.a Mr II aombe msamaha wasanii

Hivi wale wasanii walioipigia kampeni sisiem wamelipwa pesa zao za kampeni? Inasemekana walikuwa wanapigwa danadana mara baada ya kampeni.
 
wasanii wengi wa bongo tatizo lao kubwa ni njaa kali waliyonayo na kukosa elimu wengi wanaamini pasipo sisiem maisha hayapo. Umefika wakati kwa wasanii wa aina hii tuwasaidie wajikomboe
 
Basi wadau, nimeshusha mikono kweli Mh. Mr. II a.k.a Sugu hana cha kuomba msamaha, ila kwa ufupi nilivyoona maoni yenu, siasa na wasanii ni kama upepo, ukikuvumia vizuri basi unakuwa mshindi, ukivuma vibaya basi wewe umeshindwa, Sugu yupo juu!!!! Na wasanii wanatakiwa wajifunze kuwa na moral conscience itakayowafanya waweze kuwa na utambuzi wa alama za nyakati, kwani sasa watanzania tumechoka, tunahitaji ukombozi, na inavyoonekana siasa ndiyo njia pekee ya ukombozi, na kupitia uimbaji kama wa wasanii wanaweza kutoa mchango mkubwa katika huu ukombozi!!!!

Badilisha title ya post yako basi! Napendekeza iwe, Mr II Hureeee, Uko Sahihi, Wasanii Uchwara Watoswe.
 
umeandika tread yako bila kufikiria kwa ubongo bali umefkiria kwa uti wa mgongo..
Msanii anaejua haki zake hawezi kuipigia kura ccm kisa ahadi ya studiop ya wasanii... Sasa uchaguzi umeisha na iyo studio sio ya serikali iko chini ya clouds na tht...
 
Kwanini watu hawataki kuambiwa ukweli? Kama Sugu amesema ukweli, hata kama unauma, ndio sawa hiyo ili watu wajirekebishe kwa wakati mwingine.

Hongera Sugu
 
ukweli unauma hizo milioni 200 za kulipia cost ya uendeshaji wa chama cha wasanii zinakwenda wapi ruge anajifanya yeye ndo kila kitu bora wamchane tu kwenye antivirus na hiyo ngoma yake wanajiona wadau kumbe wezi tu wasanii wanalipwa pesa ndogo kwa albamu wenzao uganda wanamaisha mazuri wanadrive mavogue wanaishi maisha ya kuunga unga chumba kimoja sinza wanaona ndo wamefika mh sugu zidi kuwakomboa watakuelewa tu kaka hawajui walitendalo
 
Back
Top Bottom