Milonji
Senior Member
- May 26, 2022
- 153
- 494
Salaam wapendwa.
Shule Sasa zinafunguliwa na Wazazi Sasa tunapeleka Watoto wetu Shule.
Sina shida na watoto wa Shule za Msingi za Serikali kwa sababu wanaenda Shule kwa Kutumia usafiri wa umma (Daladala) au kwa miguu.
Hapa nazungumzia watoto wa Shule za Msingi za Mchepuo wa Kiingereza (English Medium) na wanaotumia Usafiri wa Shule (School bus).
Hizi school bus zina mambo yake, naomba Wazazi na Mamlaka husika tufuatilie kwa umakini.
Yaani unakuta basi limejaa kupita Kiasi hadi watoto wamepakatana. Mbaya zaidi watoto wa Jinsia tofauti wanapakatana. Unakuta Kijana amempakata Binti. Hivi hapo watoto hatuwafundishi ufirauni kweli?
Mabasi mengine unakuta Mtoto Mkubwa wa Kiume amempakata Mtoto mdogo wa Kiume. Hivi huku siyo kufundisha watoto tabia za Kifirauni kweli?
Je, Sheria za Usalama barabarani zinaruhusu watoto kupakatana kwenye Mabasi? Wizara ya Elimu, mnaruhusu watoto kupakatana kwenye Mabasi? Wazazi, tunaruhusu watoto wetu wapakatane kwenye Mabasi?
Jamii, tumeruhusu watoto wapakatane kwenye Mabasi?
Kwa hili wadau naomba tupaze sauti zetu ili hatua zichukuliwe.
NB:
Naomba Kuanzia Sasa Wanajamii Forums wote tutakao ona Basi la Shule limebeba Wanafunzi na wamepakatana. Tupaze Sauti zetu kwa kutaja;
1. Jina la Shule
2. Namba ya Gari (Ukiweza)
3. Mkoa ilipo Shule.
4. Wilaya ilipo Shule.
Taarifa hizi zitasaidia Mamlaka husika kuchukua hatua stahiki.
"Change begins with us"
Shule Sasa zinafunguliwa na Wazazi Sasa tunapeleka Watoto wetu Shule.
Sina shida na watoto wa Shule za Msingi za Serikali kwa sababu wanaenda Shule kwa Kutumia usafiri wa umma (Daladala) au kwa miguu.
Hapa nazungumzia watoto wa Shule za Msingi za Mchepuo wa Kiingereza (English Medium) na wanaotumia Usafiri wa Shule (School bus).
Hizi school bus zina mambo yake, naomba Wazazi na Mamlaka husika tufuatilie kwa umakini.
Yaani unakuta basi limejaa kupita Kiasi hadi watoto wamepakatana. Mbaya zaidi watoto wa Jinsia tofauti wanapakatana. Unakuta Kijana amempakata Binti. Hivi hapo watoto hatuwafundishi ufirauni kweli?
Mabasi mengine unakuta Mtoto Mkubwa wa Kiume amempakata Mtoto mdogo wa Kiume. Hivi huku siyo kufundisha watoto tabia za Kifirauni kweli?
Je, Sheria za Usalama barabarani zinaruhusu watoto kupakatana kwenye Mabasi? Wizara ya Elimu, mnaruhusu watoto kupakatana kwenye Mabasi? Wazazi, tunaruhusu watoto wetu wapakatane kwenye Mabasi?
Jamii, tumeruhusu watoto wapakatane kwenye Mabasi?
Kwa hili wadau naomba tupaze sauti zetu ili hatua zichukuliwe.
NB:
Naomba Kuanzia Sasa Wanajamii Forums wote tutakao ona Basi la Shule limebeba Wanafunzi na wamepakatana. Tupaze Sauti zetu kwa kutaja;
1. Jina la Shule
2. Namba ya Gari (Ukiweza)
3. Mkoa ilipo Shule.
4. Wilaya ilipo Shule.
Taarifa hizi zitasaidia Mamlaka husika kuchukua hatua stahiki.
"Change begins with us"