Suala la gesi mtwara maana yake wananchi wanataka serikari ya majimbo

Suala la gesi mtwara maana yake wananchi wanataka serikari ya majimbo

lengijave

Senior Member
Joined
Apr 4, 2012
Posts
116
Reaction score
36
Ndugu wadau wa jamii forum:
Baada ya kufuatilia kwa umakini sakata la Gesi huko Mtwara linanipa picha ifuatayo
1} Watanzania sasa wanahitaji serikari ya majimbo
2) Wananchi wamechoshwa na umaskini uliokithiri huku familia za watawala wakiendelea kuwa mamilionea
3} Wananchi wamegundua central government haiwezi kuwa msaada kwa raia wote 44 milioni
4) Hakuna uwiano wa maendeleo na viongozi wana amuasehemu wanayotaka maendeleo yaenda kama pinda na Katavi
5) kwamba central government inahitaji viongozi waadilifu na wenye hofu ya mungu kama Nyerere ambao hawapo kwenye enzi ya sasa ya kashfa kama za EPA,BUZWAGI.TWIGA,BULYANKULU NK
6) Kwamba hata safari za rais za kwenda ulaya na usa zaid ya mara 300 ni sababu hela inatoka Mtwara,mwanza,Arusha wao wanajipangia
7) Kwamba zile hela wanazopeleka Central government ndio zinazotumika kwenda kuwatibu watawala nje ya nchi na kuwapa posho mbali mbali wakati wananchi hawawezi hata kupata kidonge kimoja cha Tsh 50.00
8) Kwamba baada ya hela kwenda kufanyia mambo ya msingi na kulipa mishahara wafanyakazi wa serikari hasa walimu,madaktari,mapolisi,na wafanyakazi mbalimbali inatumika kununua mashangingi kwa watawala wasio na uwezo wa kuleta maendeleo kwa wananchi,na hizo pesa hutumika kutesa wananchi na kuwatupa mabopandwe
9) Wananchi wamegundua hela hizo ambazo zinapelekwa Dar ndio zinazotumika kuhonga na kuingiza viongozi vibaraka kwa watawala
10).................................

MZOZO WA GESI MTWARA NI UHITAJI WA WATANZANIA KWA SERIKALI YA MAJIMBO AMBAYO KILA JIMBO LITAKUWA LINALINDA RASILIMALI ZAKE NA GAVANA WA JIMBO ATAWAJIBIKA KWA WANANCHI WA ENEO HUSIKA
 
Wiki iliyopita, baadhi ya wakazi wa Mkoa wa Mtwara waliandamana kupinga usafirishaji wa gesi kutoka mkoani humo kwenda mkoani Dar es Salaam.

Wakazi hao walifanya maandamano ya amani ambayo yaliratibiwa na vyama vya siasa kwa huku wakiapa kuwa hawataruhusu mpango huo utekelezwe kwa kuwa kufanya hivyo ni kuwaacha wao bila kunufaika na rasilimali hiyo.

Hatua ya wananchi hao imeungwa mkono na baadhi ya wanasiasa na wanharakati ambao wanadai kuwa serikali inakimbilia kusafirisha gesi asilia kutoka katika mikoa ya kusini ya Lindi na Mtwara na kuwaacha katika umaskini wa kutupwa. Hata hivyo, upande mwingine unaweza kusema kuwa wananchi hao hawakuchukua hatua sahihi ya kuandamana na kwamba huenda wanachochewa na wanasiasa pamoja na wanaharakati.

Lakini kuna baadhi ya wanasiasa, wakiwamo wawakilishi wa wananchi hao waliotoa maoni yao na kukubaliana na hatua ya kukosoa utekelezaji wa mradi huo. Kwa mfano, Mbunge wa Jimbo la Mtwara Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Asnan Murji, amekaririwa akisema kuwa yupo tayari kufa na kupona kwa ajili ya kutetea maslahi ya wananchi wa mkoa wa Mtwara ambao wanapinga kusafirisha gesi kutoka mkoani humo kwenda jijiji Dar es Salaam.

Murji alisema kuwa amepongeza kitendo hicho kwani kimedhihirisha kuwa wananchi wa Mtwara hawaungi mkono mpango wa serikali kusafirisha gesi pasipo kuwa na sheria maalumu inayoeleza ni jinsi gani wakazi wa maeneo ambayo bomba hilo linapita watanufaika.

Kadhalika, Mbunge huyo alieleza kushangazwa kwake na hatua ya serikali kuanza mchakato wa kutaka kusafirisha gesi kabla ya kukamilika kwa sheria ya gesi asilia, ambayo hata rasimu iliyoandaliwa haionyeshi jinsi gani wananchi wa maeneo husika wataweza kunufaika.

Hoja hizo zinazotolewa na makundi kadhaa ya jamii hazipaswi kupuuzwa kwa kuwa ni changamaoto kwa serikali. Kwa hiyo serikali inapaswa kuziangalia kwa mapana na marefu ili kurekebisha pale itakapoona kuna kasoro katika mchakato huo. Inachopaswa kufanya serikali ni kuwapatia wananchi hao majibu yenye uhakika ili waamini ahadi zinazotolewa kwao kwamba watanufaika kutokana na rasilimali hiyo inayowazunguka.

Jambo la msingi ni kwamba serikali inaweza kufanikiwa kuwashawishi wananchi hao kuiamini na kuwa na subira kupitia utoaji wa elimu kuhusiana na mpango mzima wa uchimbaji wa gesi. Aidha, elimu huyo hainabudi kutolewa kwa wananchi katika maeneo yote nchini ambayo hivi karibuni yatachimbwa gesi na mafuta. Elimu hiyo itasaidia wapate uelewa mzuri kuhusiana na namna Watanzania wote wakiwemo wao watakavyonufaika kwa uchimbaji wa rasilimali hizo badala ya kupotoshwa na baadhi ya makundi yenye maslahi binafsi.

Bila kufanya hivyo, tunaweza kujikuta ukizuka uhasama kati ya kampuni za uwekezaji wa kuchimba mafuta na gesi na wakazi wanaoyazunguka maeneo ya uchimbaji kama ilinavyotokea hivi sasa katika baadhi ya nchi za Afrika zenye machimbo ya mafuta na gesi.

Kwa mfano, Eneo la Niger wakazi Delta nchini Nigeria kwa miaka kadhaa limezua uhasama baina ya wakazi wake na kampuni za kigeni zinazochimba mafuta. Miongoni mwa matukio yanayotokea kila uchao ni kutekwa kwa raia wa kigeni na makundi ya wenyeji na kuweka masharti ya kulipwa kiasi kikubwa cha fedha kabla ya kuwaachia. Wakati mwingine mitambo ya kuchimba mafuta imekuwa ikishambuliwa. Tunaamini kuwa ahadi za serikali kwa wakazi wa mikoa ya Lindi na Mtwara kuhusiana na watakavyonufaika kutokana na gesi zitakuwa za kweli. Kinachotupatia uhakika ni kauli iliyotolewa na Rais jakaya Kikwete juzi wakati wa hotuba yake ya mwaka mpya wa 2013 kwa kuwahakikishia wakazi hao ambako gesi asilia ilipogunduliwa au popote itakapogundulika, kuwa watanufaika sawia na katu hawatasahaulika.

Alisema rai yao ya kutaka na wao wanufaike inakubalika na Serikali inajiandaa hivyo na kwamba viongozi wa Mikoa ya Lindi na Mtwara kwa mfano, wanajua maelekezo aliyoyatoa kuhusu kuiandaa miji ya Mtwara na Lindi kupokea uchumi wa gesi.

Hata hivyo, tunakubaliana na kauli ya Rais Kikwete kuwa sharti la kutaka gesi isisafirishwe kwenda kokote na kwamba kila kitu kifanyike kwao halikubaliki. Kama alivyo sema Rais kuwa rasilimali inayopatikana popote katika nchi hii ni mali ya taifa zima na hutumika kwa manufaa ya taifa na katu siyo mali ya watu wa pale ilipogundulika au pale shughuli hizo zinapofanyika.

Tunatarajia kuwa sakata hili la gesi ya Mtwara halitabaki kuwa ahadi hewa bali litafanyiwa kazi ili Watanzania wote wanufaike kwa rasilimali hii.




CHANZO: NIPASHE

 
Ahadi ya barabara kukamilishwa imechukua muda mrefu?Mtwara Corridor[mipango ya kupanua bandari ya mtwara,kuwavutia wawekezaji,kujenga viwanda] na mipango mingine ya maendeleo kwa mikoa ya pembezoni haijatekelezwa.
 
Mh! Tumechoshwa na PROPAGANDA hakuna uhalisia wowote juu ya ahadi za MSHUA JK...Barabara kutoka Dar to Mtwara ni miaka 51 haijakamilika kwa nini bomba la gesi ni miezi 18? 'TAFAKARI'
 
Siasa chafu za kifisadi ndo chanzo cha vurugu zote. Wananchi wa Mtwara wanajua kinachofanyika huko Mererani, Nyamongo, Kahama na kwingineko ambapo raslimali husika haziwasaidii wananchi. Viva wananchi wa Mtwara!!!!!
 
wewe ungefika Mtwara na kukaa siku tatu tuu usingeandika habari hii. Mtwara ni moja ya mikoa iliyodharaulika sana hapa tanzania .mpaka gengeni mama ntilie anashindwa kuuza ugali na nyama au kuuza wali kwa maharage. unakuta mama ntilie anuza ugali kwa mchicha au mboga ya maboga maana nyama hawezi kabisaa kuaford.

Mtwara mjini kwa uzuri hapafikii kabisaa vingunguti machinjioni. watu humaliza shughuli za kila siku saa tisa mara baada ya wafanyakazi wa serikalini kurudi nyumbani. Yaani mtwara mjini pana umasikini wa kutisha utadhania nchi haijapata uhuru . nawaunga mkono wakazi wa mtwara kwa ujasiri wao maana hiyo rasilimali ni njia pekee ya kuwaboreshea maisha yao ingawa ni mali ya wa TZ wote.

shule ya msingi Mbawala ipo katika maispaa ya mtwara na ukiingalia utadhania ni zizi la ng'ombe jinsi ilivyo chakaa. Yaani mikoa hii ya Mtwara, Lindi na Ruvuma , kwa kweli ilidharauliwa sana. sasa kuna kiwanda kikubwa cha mBolea serikali ilitaka kukijenga Mtwara lakini wapo wajanja wanataka kiende mikoani mwao na wanchelewesha ujenzi wa kiwanda hicho mpaka uchaguzi mkuu umalizike . Unaona jinsi wakazi wa Mtwara wanavyodhulumiwa haki zao. Mwara hakuna viwanda vya sido wala Umeme wa kidatu.
 
vipi na sisi tukizuia dhahabu isitoke buzwagi?????? Ndizi zisitoke karagwe?????? Dagaa zisitoke Kigoma ?????? Chumvi isitoke uvinza?????? Machungwa yasitoke Mheza???????
Mtwara, mambo gani hayo?????? Mbona mnaturudisha kwenye ujima?????? Aibu hiyo.
 
[h=5]kama serikali inaona wananchi wa mtwara ni wabaguzi kwa kudai kunufaika na rasilimali gesi inayowazunguka, basi ifanye hvo hvo kwa rasilimali zote, kwa mfano. Ijenge bomba la kusafirisha dhahabu toka arusha, mwanza, shinyanga, chunya kwanda dar, pia ijenge bomba la kusafirisha wanyama kutoka mbuga zote kwenda dar, ijenge bomba la kusafirisha misitu ya saohill kwenda dar. Nk kwa rasilimali zote . Sioni 7bu yao ya msingi zaidi ya siasa tu, kwani kikijengwa kituo cha kuprocess hiyo gesi mtwara au kituo cha umeme mtwara wananchi wakapata ajira na umeme ukatumwa kwaenye grid ya taifa kama wafanyavyo kwanye (hep) tutakuwa hatujagawana rasilimali? Mhongo kajidharirisha, muhongo kaiharibu siasa na siasa imemuharibu yeye. Tafakari!
[/h]
 
kama serikali inaona wananchi wa mtwara ni wabaguzi kwa kudai kunufaika na rasilimali gesi inayowazunguka, basi ifanye hvo hvo kwa rasilimali zote, kwa mfano. Ijenge bomba la kusafirisha dhahabu toka arusha, mwanza, shinyanga, chunya kwanda dar, pia ijenge bomba la kusafirisha wanyama kutoka mbuga zote kwenda dar, ijenge bomba la kusafirisha misitu ya saohill kwenda dar. Nk kwa rasilimali zote . Sioni 7bu yao ya msingi zaidi ya siasa tu, kwani kikijengwa kituo cha kuprocess hiyo gesi mtwara au kituo cha umeme mtwara wananchi wakapata ajira na umeme ukatumwa kwaenye grid ya taifa kama wafanyavyo kwanye (hep) tutakuwa hatujagawana rasilimali? Mhongo kajidharirisha, muhongo kaiharibu siasa na siasa imemuharibu yeye. Tafakari!


......
kama huna chakusema si lazma kuanzisha uzi.Hebu angalia sehemu zenye rangi nyekundu;hivi ulifikiri kabla ya kuandika?
 
kama serikali inaona wananchi wa mtwara ni wabaguzi kwa kudai kunufaika na rasilimali gesi inayowazunguka, basi ifanye hvo hvo kwa rasilimali zote, kwa mfano. Ijenge bomba la kusafirisha dhahabu toka arusha, mwanza, shinyanga, chunya kwanda dar, pia ijenge bomba la kusafirisha wanyama kutoka mbuga zote kwenda dar, ijenge bomba la kusafirisha misitu ya saohill kwenda dar. Nk kwa rasilimali zote . Sioni 7bu yao ya msingi zaidi ya siasa tu, kwani kikijengwa kituo cha kuprocess hiyo gesi mtwara au kituo cha umeme mtwara wananchi wakapata ajira na umeme ukatumwa kwaenye grid ya taifa kama wafanyavyo kwanye (hep) tutakuwa hatujagawana rasilimali? Mhongo kajidharirisha, muhongo kaiharibu siasa na siasa imemuharibu yeye. Tafakari!
Mbeya tumekuwa tukitoa gesi ya CO[SUB]2 [/SUB]kwa zaidi ya miongo miwili bila kudai kiwanda kijengwe Tukuyu au Kyejo kwenyewe.
Wakifanikiwa Mtwara kila mtu atafuata kigezo cha kunufaika moja kwa moja na rasilmali zake.
 
Mambomba ya kusafirisha dhahabu, almasi toka kanda ya ziwa yapo mengi tu fungua macho utayaona. Pia ya kusafirisha mapato ya mbuga za wanyama toka Arusha, Moshi na kwingineko yapo sema wewe bado umelala!
 
kama serikali inaona wananchi wa mtwara ni wabaguzi kwa kudai kunufaika na rasilimali gesi inayowazunguka, basi ifanye hvo hvo kwa rasilimali zote, kwa mfano. Ijenge bomba la kusafirisha dhahabu toka arusha, mwanza, shinyanga, chunya kwanda dar, pia ijenge bomba la kusafirisha wanyama kutoka mbuga zote kwenda dar, ijenge bomba la kusafirisha misitu ya saohill kwenda dar. Nk kwa rasilimali zote . Sioni 7bu yao ya msingi zaidi ya siasa tu, kwani kikijengwa kituo cha kuprocess hiyo gesi mtwara au kituo cha umeme mtwara wananchi wakapata ajira na umeme ukatumwa kwaenye grid ya taifa kama wafanyavyo kwanye (hep) tutakuwa hatujagawana rasilimali? Mhongo kajidharirisha, muhongo kaiharibu siasa na siasa imemuharibu yeye. Tafakari!

Tusiyapeleke mbali mambo ya Mtwara na kuanza kujaribu kulinganisha uwezekano wa kusafirisha gesi na dhabu.

Ktk harakati za Mtwara ni matokeo ya tabia ya wanasiasa wetu. Ni muendelezo wa ‘struggle' za wananchi kama ilivyo Nyamongo-Tarime, Kahama na hata kule Geita walioondolewa kwa nguvu kwenye maeneo yao na kuachwa kuishi kwenye majengo ya mahakama na mashule kwa miaka.

Baada ya natukio yote yaliyopita, kwenye migodi na utalii, huwezi ukasema eti serikali hii ina niya yoyote njema na matumizi ya rasrimali ya nchi hii. Kumbuka mambo ya Roliondo na vitalu vya uwindaji, Angalia pale Kilimanjaro na makampuni ya utalii, angalia mahoteli yanayojengwa ndani ya Serengeti, n.k hakuna unapoweza kusema mwananchi wa kawaida anapata faida yoyote ya kutumaiiwa.

Kwa ujumla Mtwara wako sahihi kabisa na naweza nikasema CHADEMA waliposema serikali za majimbo wako sahihi kabisa!

Hatuhitaji kila kitu kipelekwe DSM halafu ndo tena eti mambo yapangwe kwa nchi nzima. Hatuna viongozi wenye akili ya kufanya hivyo ktk serikali hii zaidi ya kuangalia akina Riziwani wao.
 
Kwahiyo mtwara wanataka serikali ya majimbo baada ya gas kugundulika?
 
Siasa chafu za kifisadi ndo chanzo cha vurugu zote. Wananchi wa Mtwara wanajua kinachofanyika huko Mererani, Nyamongo, Kahama na kwingineko ambapo raslimali husika haziwasaidii wananchi. Viva wananchi wa Mtwara!!!!!

i salute you with this comment....FACTS
 
Back
Top Bottom