SUA badilikeni, achaneni na Panya imetosha

Panya wa kutambua viongozi bora, panya wakutambua mafisadi, panya wa kufanya auditing
Kwa taarifa yako:
1. Sua wanafanya tafiti nyingi sana, hiyo ya panya ni ndogo tu.
2. Hujui sua wametengeneza chanjo za magonjwa mengi ya wanyama ikiwemo kuku? Wiraza zenu izinaendelea kuabudu chanjo kutoka nje. Sio kosa la sua
3. Vipi vipaumbele vya taifa kuhusu maendeleo? Je wametenga bajeti kiasi gani na sua wakashindwa kuomba na kutekeleza? Umeelewa?
4. Training kubwa ya MSC na PhD sehemu kubwa tumeachia wafadhili, wakija na ajenda za panya wasiombe fund?
Yako mengi nadhani mleta mada anaufinyu mkubwa wa uelewa kuhusu hali za vyuo vyetu. Afanye tafiti kabla ya kukurupuka kuandika
Naishia hapo
Nilidhani ume outline tafiti zingine ambaxo wamefanya, kumbe unatetea bila strong base. Chanjo ya kuku waliyotafiti ulikubaliwa?
 
Naunga mkono hoja. Ndiyo maana kina msukuma, kibajaji, kishimba, Gwajima na mamburula lukuki yamekamata podium kuongelea mambo mazito mazito ya kitalaamu wasiokuwa na uelewa nayo wao wapo tu na vipanya wao.

No wonder world ranking ya vyuo vyetu iko huko uliko kwenye maelfu kadhaa.

Mama Samia ana kazi kubwa ya kuturejesha mstarini.

Total overhaul ya system inaweza kuwa ndiyo njia ya kuchukua.
Elimu yako tafadhali Cc Wangari Maathai
 
Nakuunga mkono, labda ibaki kama maonyesho lakini si kuhesabu kuwa ni mafanikio.
 
Dogo umepotea kweli, unatakiwa kurudi sekondari

Dogo umepotea kweli, unatakiwa kurudi primary

Hivi una hata mwaka JF kweli wewe? Alaah!

IMG_20210515_134247_922.jpg


Kumbe wewe ni ile mipambe ya propaganda za Corona na wizi wa uchaguzi 2020.

Hiiiiii bagosha!
 
Na Thadei Ole Mushi.

SUA wamekuja na panya wa Kupima Corona... Mimi nshaanza kuchoka na hawa panya wa SUA.

Sayansi hii ya kufundisha wanyama kunusa (Sniffing) kwa wenzetu ilianza muda mrefu sana. Ni mojawapo ya Technolojia ya kizamani kabisa. Huko Cuba Panya wameanza kutumika toka 1954 kunusa maeneo yenye madini, mobomu nk. Kwa sasa haitumiki Sana kwa kuwa njia za kisasa zaidi zimeendelea kugundilika kila kukicha.

Ni wakati sasa wa kuwaambia SUA badala ya kutrain Panya zaidi ambao hatuwatumii popote wajikite kwenye kugundua mabomu ambayo tutayauza au wajikite kwenye kufanya tafiti tunawezaje kutumia uranium iliyopo kule Dodoma kuzalisha nguvu za Nyuklia. Au wajikite kutengeneza Chanjo ya Corona ambayo tutaiuza.

Waliwahi kuja na panya wa kutambua TB lakini hakuna Hospital hata Moja inayotumia Panya kunusa makohozi. Bado njia za kisasa za kupima TB ndizo zinazoendelea Kutumika mahospitalini.

Hata hii ya kutegua Mabomu kwa kunusa ni ya zamani Sana. Majeshi ya wenzetu hawatumii Tena sniffing technology Sana nadhani tunapaswa kuanza kufikiria kubadilika.

Sio kwamba wenzetu hawawezi ku train Panya kufanya sniffing. Wanaweza Sana Ila ni technolojia ya Zamani mno watu walishahama huko wanaitumia technolojia hii mara Chache Sana.

Yaani Maabara za Dunia zipo busy kutengeneza Chanjo na Makampuni yanashindana kwenye kutengeneza Chanjo sisi tunamuwaza panya tu atusaidie kunusa watu wenye Corona.

Tuwekeze kwenye tafiti zitakazoleta faida na uvumbuzi wenye tija kwa Taifa na Dunia. Naona SUA wao kila kitu ni kuwaza Panya wao tu. Tumekuwa kama tumesimama mahali pamoja wenzetu wanakwenda mars na kurudi sisi tunalisha Panya Pumba tu hapo SUA. Na wameona hakuna Cha maana wanachofanya wameamua kuanzishwa course za Education. Jamani nafikiri hivi vyuo kila kimoja ki-save purpose yake.

Je kitu Wanachokiweza SUA ni Kutumia panya Kunusa Tu? Vyuo vikuu vingine wao kwani wanasemaje? Muhimbili pale kile kijumba Cha kujifukiza bado kipo?

Tunakwama wapi? Leo Tarehe 15/5/2021 asubuhi hii China imefanikiwa kurusha kifaa kwenda Sayari ya Mars na kimetua vizuri na kitakaa huko Miezi 3 kutafiti kama Kuna uwezekano wa maisha kwenye Sayari hiyo. Huko Sua Profesa anaamka na Box la Panya anaenda kuwachungulia na anatokea hadharani anasema amevumbua kitu.

Tubadilike... Dunia inakimbia sisi tumekaa kabisa na tumeanza kulala.

Ole Mushi.
0712702602

View attachment 1785585
UDSM wao wanatengeneza Smoothie na maji ya kujifukiza.
 
Wewe jamaa kilaza kweli, aliyekwambia tafiti zinazofanyika SUA zinahusu panya wa kunusa pekee ni nani? aliyekwambia tafiti zinazohusu sniffing animals zimekufa duniani ni nani? kama zimekufa inakuwaje hao wazungu wanaendelea ku-fund hiyo research? hebu twambie serikali yako inatoa kiasi gani cha pesa kwenda kwenye vyuo vikuu au kwenda COSTECH kwa ajili ya ku-fund research....au umekuja kuhara tu humu kisa una machungu ya kuliwa kichwa hapo SUA.
 
SUA hawataona huu ni ushauri,ni kweli kwa dunia ya leo kufanya utafiti wa panya sijui atambue nini,ni uzembe wa kiwango cha lami;
ningesikia wana-design sensors kwa ajili ya utambuzi wa magonjwa mbalimbali sawa,ila panya hapana;
Kama sniffing dogs wanatumika kwanini iwe ajabu panya kutumika?
 
Back
Top Bottom