Student's unlimited freedom

Student's unlimited freedom

Deadbody

JF-Expert Member
Joined
May 30, 2015
Posts
4,274
Reaction score
6,632
WALIMU WETU NA ELIMU KUANZIA OKTOBA 06, 2016

Binafsi sikutaka kabisa kuzungumzia suala la walimu wa mafunzo /Field wakiongozwa na Frank Msigwa kumtesa mwanafunzi Sebastian katika shule ya Sekondari ya kutwa ya Mbeya (Mbeya Day). Watu mbalimbali wakiwepo walimu na marafiki zangu kunitaka kuzungumzia jambo hili.

Lakini pia katika makundi ya whatasaap ya CHADEMA, makundi ya walimu ya whatasaap na hata Facebook nimona mawazo ya watu mbalimbali wengine wakiunga mkono adhabu hiyo na kutetea walimu kwamba ni halali adhabu hiyo kali na walimu wameonewa kufukuzwa vyuo.

Wengine wameonekana kukerwa sana na adhabu hiyo ya kikatili kwa mwanafunzi na wengine wameeleza kwamba kama Sebastian angekua mwana wao wangewamaliza walimu katika kundi hili Walimu wametukanwa kila aina ya tusi ikiwa ni Pamoja na kuitwa "MSHETANI" "HAWAIJUI LEBA / CHUMBA CHA KUJIFUNGULIA", "MAJAMBAZI ", " WAUAJI "," VILAZA WALIOFELI ", na matusi mengine mengi sana ya aibu mengine yakiwa ya nguoni.

Baada ya kujiridhisha maoni ya watu wa pande mbili nimegundua kwamba kwa sasa elimu yetu itaonekana upya na itaanza upya katika suala la uhusiano wa walimu, wanafunzi na wazazi. Walimu wameonesha kueleza kwamba wameonewa Sana kupewa adhabu ya kufutwa vyuo na kufunguliwa mashtaka.

Walimu wanadai, madaktari wamefanya operation na kusahu nyembe katika mwili, wamesahahu sindano au vitu vingine lakini hawajafukuzwa Kazi nk. Wamehoji mateso aliyoyapata mwananchi mmoja huko Mlowo Mbozi kwa udhururaji kwa kipigo cha mbwa mwizi na Polisi na kufariki hali iliyopelekea wananchi kuandamana kukataa kuzika.

Madhaifu ya wazi na sirini yamejitokeza katika taaluma za uhandisi, jeshi la polisi, Udaktari nk. Lakini hakuna hatua zilizochukuliwa dhidi yao. Ghorofa lililoanguka na kuua watanzania Dar Es Salaam mwaka 2012 na 2013 mpaka leo hakuna hatua zilizochukuliwa dhidi ya wahandisi...

Nimeona walimu wameamua kuanzisha uhusiano mpya ili kulinda vibarua vyao. Walimu wanasema kwamba kuanzia sasa kazi ya mwalimu itakua ni kufundisha tu. Walimu wengi wanasema kwamba mwanafunzi aje shule asije hatafuatiliwa. Mwanafunzi avute bangi asivute hakuna wa kujihusisha naye. Mwanafunzi akiwa na uhusiano wa kimapenzi asiwe na uhusiano hakuna kumfuatilia.

Mwalimu akitoa kazi mwanafunzi afanye asifanye hakuna wa kumfuatilia. Mwanafunzi alewe asilewe hakuna wa kumfuatilia. Mwanafunzi achelewe shule, atukane walimu, wanafunzi wagombane, wanafunzi wakifanya chochote wataachwa huru. Mwalimu atafundisha na kuondoka. Hakuna adhabu yoyote kwa mwanafunzi yeyote labda mwanafunzi akipata mimba au kuacha shule mwenyewe lakini walimu watajiondoa kuwa walezi /wazazi wa wanafunzi.

Hii ni kuepusha uhasama wa wanafunzi na wazazi wao dhidi ya walimu. Walimu Kazi wanayosema wamebaki nayo ni kufundisha tu basi. Mengine ni kazi ya mzazi. Uhusiano huu wa wazazi na wanafunzi dhidi ya walimu utawapa uhuru usio na mipaka wanafunzi (Student's unlimited freedom) na matokeo yake yanakuja wazazi, walimu, wanafunzi na serikali tujiandaye kupokea matunda na matokeo ya uhusiano huu mpya wa STUDENT'S UNLIMITED FREEDOM.
 
Kama wanajipenda naamini hawatafanya mambo yaliyo nje ya mikataba walioingia na waajili wao. Kama Luna kipengele cha kutoa adhabu katika mikataba yao basi watekeleze tofauti na hapo yatakayowapata yanawastahili
 
Hiyo nini maana yake? Walimu mmeamua kususa/kununa? Unasema walimu wameamua? Walimu wa wapi hao? Idadi yao?

Ndugu usijaribu kuwakilisha mawazo ya walimu wote nchini utakuwa unajipotosha bure tu. Ngumu jambo hilo kufanikiwa. Mwalimu anayejua nini maana ya wajibu wake kwahakika atatimiza wajibu wake shule iwe sehemu salama kwa mwalimu na mwanafunzi pia. Migogoro itaendelea kuwepo na ufumbuzi utapatikana tu.....ndivyo ilivyo.
 
Hiyo nini maana yake? Walimu mmeamua kususa/kununa? Unasema walimu wameamua? Walimu wa wapi hao? Idadi yao?

Ndugu usijaribu kuwakilisha mawazo ya walimu wote nchini utakuwa unajipotosha bure tu. Ngumu jambo hilo kufanikiwa. Mwalimu anayejua nini maana ya wajibu wake kwahakika atatimiza wajibu wake shule iwe sehemu salama kwa mwalimu na mwanafunzi pia. Migogoro itaendelea kuwepo na ufumbuzi utapatikana tu.....ndivyo ilivyo.
walimu msidanganyike kazi ya kuchapa wanafunzi niyamwalimu mkuu kama sheria zinavyojieleza kwanza yeye anaposho tofauti na mwalimu wa kawaida wazazi wa wasimamie watoto wao wenyewe wewe kama mwalimu hayo yakuvuta bangi mwanafunzi yanakuhusu nini achaneninao tu
 
walimu msidanganyike kazi ya kuchapa wanafunzi niyamwalimu mkuu kama sheria zinavyojieleza kwanza yeye anaposho tofauti na mwalimu wa kawaida wazazi wa wasimamie watoto wao wenyewe wewe kama mwalimu hayo yakuvuta bangi mwanafunzi yanakuhusu nini achaneninao tu
Unadhani mihemuko yako itasaidia? Eti waache kufuatilia wanafunzi wanaokosea? Kwasababu wewe "slimshedy" umezira? Hiyo haiwezekani mwalimu anayefahamu vema kazi yake/mkataba wake wa kazi atatimiza yote tu. Mark my words....siku zitajongea na walimu wataendelea kufanya kazi zao kama kawaida. Madai ya walimu wanataka kupiga kwa kudhalilisha wanafunzi hayana nguvu yatapotea kama moshi unavyopotelea angani.
 
Jamani walimu acheni hasira,tunajua nyinyi ni wazoefu hamuwezi kupiga mtoto vile wale walikuwa tu ni vijana wa field wenye mzuka wa Jkt!! chonde chonde sisi wananchi bado tunawapenda na kutambua mchango wenu walimu wazoefu acheni hasira tulijenge taifa eee baba!
 
Walimu mnazidi kujidhihirisha jinsi gani mlivyo hasa walimu wa shule za serikali. Kwanini tukio kama lile haliwezi kutokea kwenye shule binafsi?
Kwanini mambo ya ajabu tu yanatokea kwenye shule za serikali?
Hivi amuwezi kujiuliza ni kwanini yanatokea shule za serikali tu?
 
Walimu mnazidi kujidhihirisha jinsi gani mlivyo mambumbu hasa walimu wa shule za serikali. Kwanini tukio kama lile haliwezi kutokea kwenye shule binafsi?
Kwanini mambo ya ajabu tu yanatokea kwenye shule za serikali?
Hivi amuwezi kujiuliza ni kwanini yanatokea shule za serikali tu?

Ndivyo unavyojidanganya? kwa taarifa yako private ndio kuna ushenzi hatari.. utofauti uliopo ni katika kushughulikia haya masuala
 
Ndivyo unavyojidanganya? kwa taarifa yako private ndio kuna ushenzi hatari.. utofauti uliopo ni katika kushughulikia haya masuala

Huo ushenzi uko wapi?
Ni lini umesikia suala la ajabu ajabu limetokea shule binafsi?
Tatizo lenu walimu wa serikali mnafanya kazi kwa mazoea
 
Back
Top Bottom