WomanOfSubstance
Platinum Member
- May 30, 2008
- 5,457
- 972
Gents pia mnaruhusiwa kuchungulia...maana na nyie siku hizi hamshikiki kwenye kujiremba lol!
Nimeshawishika kuandika mada hii na nyingine zitakazofuata kwa kuona jinsi wanawake tunavyodanganywa katika "kununua matumaini".Nimeona wanawake wa kipato kidogo sana wakitumia 90% ya rasilimali fedha walizo nazo katika kununua uzuri au urembo.Wapo akina kaka/baba ambao huchangia pia katika ununuzi wa urembo kwa wake zao na wapenzi wao.
Nyingi ya vipodozi au urembo huu hasa wa bei poa ni short-lived au huleta madhara kwa mtumiaji au hata uzao wake.Inasikitisha kuona mama mjamzito au anayenyonyesha akijikoroga kwa vipodozi vyenye kemikali hatari kama zebaki n.k au mikorogo inayotengenezwa uchochoroni na wafanya biashara wasio na ethics ( biashara ni ushindani na mara nyingi ushindani hauna adabu!).
Kwa sasa hivi, soko la vipodozi na urembo limevamiwa na wakongo na wanaijeria ambao huchanganya madawa makali na kuyafungasha katika vifungashio vya kuvutia na kuvipa majina ya kuvutia - extra light, super white etc.Wachina nao wameshanusa na kujua mwafrika anataka nini na hivyo kujibu kiu ya soko kwa bidhaa kadha wa kadha.
Biashara yoyote yenye kulenga urembo wa mwanamke huuza.Kwanini? kwasababu kila mwanamke anapenda kujali muonekano wake.Amelelewa ( socialized) kutaka kuwa na ngozi nyororo isiyokuwa na mawaa, awe na nywele nzuri - ndefu, zenye kung'ara, awe na kucha zilizonakshiwa zikavutia, awe na umbo lililokaa vema - kutegemeana na mhusika anayotaka.Kuna wenye kupenda unene, wembamba nakadhalika.Wapo wenye kupenda kuonekana warefu zaidi, japo sijui kama wapo wenye kupenda ufupi n.k.Kuna wenye kupenda waonekane wamejaaliwa vifuani, kwenye makalio,hips na kadhalika.
Tukitizama vigezo vyote hivi tutaona kuwa kuna biashara lukuki zenye kulenga maeneo hayo yote niliyoyaainisha.
1. Nywele - dawa na mafuta ya kulainisha, kuviringisha, kubadili rangi, kuna kusuka, kukuza nywele, kujaza nywele n.k.
2.Ngozi -dawa na mafuta ya kulainisha, kung;arisha, kufanya iwe na rangi ya kung'aa, kuifanye iwe nyeupe na kwa vile naangalia zaidi urembo wa kiafrika sijui kama kuna virembesho vya kuifanya iwe nyeusi! wazungu wanazo tans etc.Kuna mikorogo ya kienyeji n.k.
3. Kucha - dawa za kurefusha, kubandika ziwe ndefu, kusafisha,kuna rangi n.k
4.Maumbile - kuna mazoezi kupunguza au kujenga sehemu husika, kuna dawa siku hizi za kupaka na kumeza kuongeza au kupunguza, kuna upasuajia nk.Kuna nguo za kubana matumbo, makalio, kuna viatu kuongeza urefu
5. Mvuto - kuna manukato, dawa za usafi zenye kulenga maeneo mbalimbali ya mwili wa mwanamke...
Kwa kifupi UREMBO WA MWANAMKE NI BIASHARA KUBWA.kwavile inahusu kuuza na kununua matumaini...siku zote wenye kuifanya wana uhakika wa kutajirika.....There is always hope
Je ladies..are you aware of how much u r contributing to enriching unscrupulous business men and women ?
Kama mlengwa wa hizi biashara, unachukua hatua gani kuhakikisha hauingii kwenye mitego ya kukufukarisha badala ya kukupa tumaini unalolitazamia.?
Are you aware kwamfano kuna njia nyingi salama na za bei nafuu za kukupa urembo wa ngozi yako na nywele?..Urembo wa ngozi na nywele zako unaweza kupatikana kwa kula chakula bora ,kunywa maji ya kutosha - mwili wa binadamu asilimia zaidi ya 70 ni maji! Huhitaji kutumia kemikali kusafisha ngozi yako auaweza kutumia matunda na mboga kusafisha ngozi yako kwa mfano ndimu au limao, huhitaji mikorogo bali waweza kujipaka mafuta unayoweza kutengeneza mwenye ( mwenye kutaka ani PMnimjuze)..Unweza kudumisha urembo wako kwa kujipa mawazo safi akilini mwako, kupumzisha akili na mwili wako, kufanya kila kitu kwa kiasi - kula, kunywa, na vingine ambavyo siyo vizuri kuvisema hapa.
itaendelea......
Nimeshawishika kuandika mada hii na nyingine zitakazofuata kwa kuona jinsi wanawake tunavyodanganywa katika "kununua matumaini".Nimeona wanawake wa kipato kidogo sana wakitumia 90% ya rasilimali fedha walizo nazo katika kununua uzuri au urembo.Wapo akina kaka/baba ambao huchangia pia katika ununuzi wa urembo kwa wake zao na wapenzi wao.
Nyingi ya vipodozi au urembo huu hasa wa bei poa ni short-lived au huleta madhara kwa mtumiaji au hata uzao wake.Inasikitisha kuona mama mjamzito au anayenyonyesha akijikoroga kwa vipodozi vyenye kemikali hatari kama zebaki n.k au mikorogo inayotengenezwa uchochoroni na wafanya biashara wasio na ethics ( biashara ni ushindani na mara nyingi ushindani hauna adabu!).
Kwa sasa hivi, soko la vipodozi na urembo limevamiwa na wakongo na wanaijeria ambao huchanganya madawa makali na kuyafungasha katika vifungashio vya kuvutia na kuvipa majina ya kuvutia - extra light, super white etc.Wachina nao wameshanusa na kujua mwafrika anataka nini na hivyo kujibu kiu ya soko kwa bidhaa kadha wa kadha.
Biashara yoyote yenye kulenga urembo wa mwanamke huuza.Kwanini? kwasababu kila mwanamke anapenda kujali muonekano wake.Amelelewa ( socialized) kutaka kuwa na ngozi nyororo isiyokuwa na mawaa, awe na nywele nzuri - ndefu, zenye kung'ara, awe na kucha zilizonakshiwa zikavutia, awe na umbo lililokaa vema - kutegemeana na mhusika anayotaka.Kuna wenye kupenda unene, wembamba nakadhalika.Wapo wenye kupenda kuonekana warefu zaidi, japo sijui kama wapo wenye kupenda ufupi n.k.Kuna wenye kupenda waonekane wamejaaliwa vifuani, kwenye makalio,hips na kadhalika.
Tukitizama vigezo vyote hivi tutaona kuwa kuna biashara lukuki zenye kulenga maeneo hayo yote niliyoyaainisha.
1. Nywele - dawa na mafuta ya kulainisha, kuviringisha, kubadili rangi, kuna kusuka, kukuza nywele, kujaza nywele n.k.
2.Ngozi -dawa na mafuta ya kulainisha, kung;arisha, kufanya iwe na rangi ya kung'aa, kuifanye iwe nyeupe na kwa vile naangalia zaidi urembo wa kiafrika sijui kama kuna virembesho vya kuifanya iwe nyeusi! wazungu wanazo tans etc.Kuna mikorogo ya kienyeji n.k.
3. Kucha - dawa za kurefusha, kubandika ziwe ndefu, kusafisha,kuna rangi n.k
4.Maumbile - kuna mazoezi kupunguza au kujenga sehemu husika, kuna dawa siku hizi za kupaka na kumeza kuongeza au kupunguza, kuna upasuajia nk.Kuna nguo za kubana matumbo, makalio, kuna viatu kuongeza urefu
5. Mvuto - kuna manukato, dawa za usafi zenye kulenga maeneo mbalimbali ya mwili wa mwanamke...
Kwa kifupi UREMBO WA MWANAMKE NI BIASHARA KUBWA.kwavile inahusu kuuza na kununua matumaini...siku zote wenye kuifanya wana uhakika wa kutajirika.....There is always hope
Je ladies..are you aware of how much u r contributing to enriching unscrupulous business men and women ?
Kama mlengwa wa hizi biashara, unachukua hatua gani kuhakikisha hauingii kwenye mitego ya kukufukarisha badala ya kukupa tumaini unalolitazamia.?
Are you aware kwamfano kuna njia nyingi salama na za bei nafuu za kukupa urembo wa ngozi yako na nywele?..Urembo wa ngozi na nywele zako unaweza kupatikana kwa kula chakula bora ,kunywa maji ya kutosha - mwili wa binadamu asilimia zaidi ya 70 ni maji! Huhitaji kutumia kemikali kusafisha ngozi yako auaweza kutumia matunda na mboga kusafisha ngozi yako kwa mfano ndimu au limao, huhitaji mikorogo bali waweza kujipaka mafuta unayoweza kutengeneza mwenye ( mwenye kutaka ani PMnimjuze)..Unweza kudumisha urembo wako kwa kujipa mawazo safi akilini mwako, kupumzisha akili na mwili wako, kufanya kila kitu kwa kiasi - kula, kunywa, na vingine ambavyo siyo vizuri kuvisema hapa.
itaendelea......