Asante kwa mchango wako nimeupokeaYaani una miaka 22 unasimulia story ya maisha yako uko seriously kweli?
Duuh kweli mmegundua wanna jf wana hali ngumu Koo wanapenda story za kuwafariji na nyie mnawaletea story kila uchao
Sema me mtu anaekaa kwao hawezi akanipa story ya maisha yake
Endeleza story weweAsante kwa mchango wako nimeupokea
😂😂😂 pole mkuu ila kuwa pamoja nami nitakusimulia nivyokua nateka watu simu hususani ni wanafunzi na mabishoo plus masista duuh...Musoma? kuna shule hapo kyabakari ilikuwa inaitwa Musoma Utalii. Mimi na mwanangu mmoja tulitoroka siku moja kwa kuruka fensi eee bwana eee tulikamatishwa na wahuni huko msituni simu ikaenda, viatu tukavulishwa mbaya zaidi na stori za kuwa tumekatwa mapanga zikawafikia wazazi. Ila hatukukoma kesho yake tulitoroka tena alfajiri tukasepa zetu Town. Shule ilikuwa ya kiboya sana ile.
kumekucha aiseeInaendelea
Kwanza samahani kwa kuchelewa kuleta muendelezo ni kutokana kutingwa na shughuli za kutafuta future's.
Haya tuendelee sasa
Baada ya kuhama kwenye nyumba mpya na mtaa mpya kiukweli maisha yalibadilika sana kwanzia mazingira na aina ya marafiki wapya nilio wapata hapo.Nyumba ilkua kubwa Vyumba 5,choo ni ndani kwa ndani.Lakini hapo tulipo hamia tulikumkuta jamaa mmoja ambae ni mtoto wa mwenye nyumba,alikua anakaa kwenye chumba kimoja vinne vilivyo baki tulkua tunakaa sisi.
Huyo mtoto wa mwenye nyumba kipindi hicho alikua amemaliza 4m 6 alkua anajiaanda kwenda chuo.Muda wa chuo ulivyofika akasepa zake chumba chake akaniachia niwe nalala.Jamaa alitokea sana kunikubali japokua nilikua bado yunk kuna vitu vyake vya siri alkua ananiambia.Tuachane nae kwanza huyu jamaa nitamuelezea mbele maana vitendo nilivyomfanyia tuliishia mwisho mbaya.
Mwaka 2008 nikiwa darasa la sita ckumbuki mwezi ila familia yangu iliyumba kiuchumi kidogo kutokana Baba yangu kusimamishwa kazi kwa muda kupisha uchunguzi ( alituhumiwa kutembea na wanafunzi kimapenzi ) ko hali ya kifedha ikawa chenga mama nae alikua kastop biashara yake tulkua tunaishi kwa kudra za mwenyezi Mungu tu.
Siku moja Mama aliniandika kibarua hivi na kutaka ni mpeleke binamu yangu ambae alikua anafanya kazi Garage ( hio garage ipo maeneo ya Mtaa wa Gandhi karibu na Mwigobero ) kwenye hicho kibarua alikua anataka msaada wa pesa tu.niliipeleka fresh tu na kweli nilipewa 20k siku hyo na maisha yakaenda.Me nilivyoona hivyo nikasema basi hapo ndo nitakua napata hela.Nilichokua nafanya nilkua naandika kabarua na kumpelekea huyo binamu yangu,yeye alikua anajua kinatoka kwa Mwana mother kumbe ni mimi muhuni ndo nilkua naratibu mambo .Kweli pesa nilkua napata 20k,10k zilkua hazinikosi kwa huyo binamu.
Huo mchezo uliendelea hivyo hivyo Mama akiwa hajui nilifanyalo mpk nilivyofika form one 2010 ngoja nieleze nilivyonaswa.
Siku hyo nilkua sina Do ( pesa) nikimuomba Mama ananirusha Mzee ndo kabisaa nilikua cthubutu kabisa kumuomba nilikua na muogopa.Sasa cku hyo baada kuwaza sana nitapata wap hela ndo nikakumbuka kuwa kuna mkombozi wangu binamu.Nikaandika kabarua kama kawaida kesho yake nikakapeleka tena cku hyo niliomba nipewe 30k za Dawa ( nilkua nadanganya kuwa Mama ndo anataka ) basi midaa ya mchana baada kutoka shule nikala then nikaelekea garage,nilimkuta vizur tu nikampa kale ka ujumbe ni kamwambia Mama kanituma akakasoma.Alivyomaliza kukasoma nikawanaona mtu anajisachi,alikuwa hana hela siku hyo,akanambia nitangilie home yeye atakuja baada ya kutoka job.Nilivyockia hivyo moyo ulienda mbio kwa hofu nikawa najisemea moyoni kuwa leo nimeisha tamaa zangu zimeniponza.Nilienda home nikiwa nawaza sasa huyu akija itakuaje.Nilifika home nikamkuta Mama kalala zake kwenye sofa hana hata habar na Mtu nikatoka nje lengo ni kumsubir huyo binamu kama akina nimdanganye kuwa Mama hayupo.nilipokua nawaza hayo ghafla binamu huyo akaja na Pikipiki yake nilitetemeka vbya mno mpk jasho lilinitoka puani .Aliniuliza tu Shangazi yupo ndani badala ya kusema hayupo nikasema ndio yupo nadhani ni kutokana na hofu.Alivyoingia ndani nikaona isiwe kesi wala nini nikaamua kukimbia home kuepuka ile noma......
Nitarudi kukikucha.........