Story: Mahusiano

Money Penny

JF-Expert Member
Jun 20, 2016
15,920
14,819



SEHEMU YA 1

A. NINAITWA MTUMISHI PAPA

Mtumishi Papa:
Penny wewe unapenda stori jaman sijakuona sikunyingi ujue!

Money Penny: basi tukasalimiana hapo wee tukajikumbushia ya zamani akyanani sikuamini Patric amekuwa Mtumishi wa Mungu

nakuambia kweli mpenzi msomaji Patric namwelewa kuliko maelezo, ni wale best friend wa zamaaan kabla sijaolewa nikiwa mafiaaaa (mtundu-mkorofi)... huyu jamaa Patric alikuwa ni noumeeer alikuwa na roho ngumu vibaya mnooo... watu wa kwenye shishtimu walishamtumiaga sana mpaka tukahisi yupo huko lakini nahisi yupo ngoja kwanza niendelee na stori utajaza mwenyewe mpenzi msomaji!

Patric Darasani alikuwa Kilaaaazaaaaa namfundishaaa anafeli nampiga pindi anafauluuu... tukamaliza form 6 sikumwona tena mpaka siku moja natoka zangu ofisi moja Posta namwona anapita amevaa suti nyeusi kwasababu nilikuwa nimemzoeaaa nikamwita bila wasiwasii wewe PAPAAAAA, hakugeuka nikarudiaaaa hakugeukaaa nikamwita kwa mara ya mwisho huku watu wananiangalia na walinzi wa ofisi wameshaanza kusogea nikaita we PATRIIIIIIIC PAPAAAA ndio akageuka, aliponiona hakushtuka akaondoka walikuwa na wenzake 3 wamevaa suti nyeusi na miwani meusi ( asomaye na afahamu)

Basi Penny bila mafanikio nikaondoka zangu, kufika nyumbani napokea simu naskia ananiita we PAPA mamboooo?! ulikuwa wapi nyau we nakutafutaa!?

sikuelewa Patric alipata wapi mobile no yangu lakini alikuwa nayo tukaomgeaaaa akaomba anione usiku huo huoooo maana alfajiri anaamsha anaenda KUWAIT

Money penny tena, nikajongea fastaaa Serena Hotel!... tukasalimiana, tunakumbatiaaaanaaaa, tunachekaa kama watotooo!

baada ya kula na kunywa Patric akafungukaaa

Papa: Penny unajua umeniharibia sana pale umeniita nilikuwa kazini, kazini wananiitaga PAPARAZI ila marafkizangu wananiitaga PAPA kwasababu yako Penny, ujue Penny mimi na wewe vilikuwa vinaiva sana tulipokuwa shuleni, mpaka kunipa jina la Papa na kuwaambiwa office mate waniite papa yote ni kwa ajili yako,

Money Penny: i know! enhe niambie unafanya kazi wap umepataje kazi wakati sisi bado tupo IFM tunasoma tunasotaaa na kiadvance diplomaa?!

Papa: we acha si unajua form 6 nilipataga div 0.. nikatoka pale nikaenda kujiunga na jeshi, nikapigaaa nikapata kazi

Money Penny: mbona hauna mavazi ya Jeshi sasa? naona umepiga suti mara Tshirt za form 6 vepee?

Papa: nilipokuwa Jeshi pakanishinda mafunzo magumuu na vile nilikuwaga kimbaombao nikaacha katikati nikasepa, baadae akaja mzee mmoja akaniomba nirudi nikitoka hapo atanipa ajira! basi nikaenda kumalizia kwa heshima na usimamizi wa yule mzee nikafaulu nikarudi uraiani nikasota mwaka yule mzee nikaona kama amenidanganya kumbe sio kweli

Baada ya mwaka nanusu yule mzee akarudi! akaniambia nisamehe mwanangu niliumwa nikapoteza simu ila kwakuwa kwenu napajua ndio nimekuja, kazi yako bado ipo ndioo nimepewaaa nimeanza miezi 6 ijayo... nafanya kitengo maalum uje unisalimie akanielekeza ofisini kwao akaniambia nasafiri naenda KUWAIT nikirudi nakualika uje!

Money Penny: nikachokaa! cha, huyu kilaza amekuwa mtu mkubwa anavuta hela ndefuuu macho yakanitokaaa nikamuomba nikimaliza shule aniweke hata BANK jamaaa njaa inauma si unajua tenaaa!

Papa: akacheka sanaa aaah Penny nimekumiss sana we maliza shule nitakusaidia!

Baada ya usiku ule hatukuonana kweli akasafiri.. ikapita miaka 2 nikapata tena simu ya PRIVATE NO, nikajua tu ni yeye, akaniambia njoo Kempinski nimekumiss mtoto mzuri, ah ngoja kwanza nitakupigia simu ikakatwa, sikumsikia mpaka miezi 6 ilipopita akanipigia na simu ya TTCL we PAPAAA njooo Kanisa flan nakusubiria ukichelewa naondokaaa!

Money Penny: nikajongeaaa! huko ndani ndani dar es salaam silitaji jina kabisaa! dah kufika naona kanisa la udongoo... heee we Papaaa, vepee? mbona upo huku umekuja kuua mtu au?

Papa: akacheeekaaa! Penny bwana, haya karibu, nikapewa kigoda nikakaa nashangaa watu wanakuja wanamsalimia shikamoo Mtumishi shikamoo Pastor, shikamoo Mchungaji

Papa anawakaribisha pale karibuni na maneno ya kilokole

Money Penny: namshangaa huyu muhuni kachanganyikiwaa?
hapo natamani kucheka sina mbavu wai kwani huyu Papa kawa mchungaji saa ngapi?

Papa: Penny bwana mimi ni mchungaji msaidizi kwenye hili kanisa la Waenda Mbinguni

Money Penny: kwa mshangao nikamjibu naonaa! kwanini?

Papa: Penny ile kazi nilishaiacha stress kibao nikaamua kumrudia Mungu, riziki popote penny, Mungu atanitunza

Money Penny: aisee! hongera sana kwahiyo sasa mama mchungaji hapa yupo wapi? namaanisha mkewako

Papa: hilo ndio nimekuitia best wangu najua unazo akili, kuna demu nimemwona hapa nimempenda sana, nisaidie kumchunguza tafadhali, ila niletee details za ukweli, ukinidanganya tutagombana sana! akaingiza mkono mfukoni akatoa picha huyu hapa anaitwa ANITA!

Money Penny: nikachokaa! heee huyu demu nae kaokoka au? mbona mzuri sana?

Papaa: ndio nataka umfuatilie kama kweli kaokoka au la! kabla sijaoa binti nataka kujua sanaaa nimchunguze sana, wewe fanya upande wako na mie nafanya wangu.. akaingiza mkono mfukoni akatoa ATM card ya benki akanipa, tumia hii bank card password ni **** fanya urafiki na ANITA mpe anachotaka mfanye awe rafiki yako wa karibu akupe siri zako za zamani na mpaka sasa, tutakuwa tunawasiliana kwa namba hii akanipa business card imeandikwa Pastor Patric!

hapa usiwe unakuja plz plz maana nitaonekana vibaya si unajua walokole walivyo! na haya mavazi yako ya jeans na vimini huku usije nayo katafute mashuka uvae ukija huku!

kwaheri mimi naingia kwenye ibada... fanya kazi yangu kama nilivyokuagiza plz usiniangushe maana haukuwahi kuniangusha sikuwahi kufeli mitihani ila wa form 6 tu! plz nenda tutawasiliana

akainuka akaingia ndani mimi nikasimama kwenye ukuta wa majani ya nazi pembeni kuna dirisha namwangalia mwenyewe anaongoza ibada ananena kwa lugha! nilichoka Penny huyu muhuni kawa Mchungaji tena?! uuuuwi kichwa kiliniumaaa nikajikaza nikaondoka... nikiwa njiani nikapitia bank nijaribishe nione kama hii kadi ya kweli au feki



kuangalia Yeeeesu wangu na mariaaaa... akaunt ina milioni 80 cash, mpaka nikaogopa, hapo naangalia ilikuwa mwaka wa 95... mwaka wa 95 mtu anamiliki milion 80 niligandaaa! nikatamani nizipige zile hela nisepe akinifuata nitamwomba msamaha lakini nikakumbuka shule yangu iko ukingoni kuisha huenda akanisaidia kupata ajira sio kwa hela hizi

nikarudi nyumbani kichwa chamoto nikalala!

Jioni akaingia dogo mmoja dogo wangu sanaaa, namkubali sanaa dogo ana akili kinyama ila yeye hakufanikiwa kusoma aliingia kwenye biashara, dogo ana pesa zake ana biashara zake mtu mzuri sana,

tukaongea ongea palee nene, mambo kibao ananitania Penny ukimaliza tu shule nakuajiri kwenye kampuni zangu me namcheka wai huna hela ya kunilipa bwana acha kelele... tukaongea hapo weee akaniambia Penny tena nimekumbukaa, naomba unisaidie kitu kimoja

kuna demu nimemzimia nataka kumuwooowaa! nilikutana nae wakati na deposite hela bank, yeye alikuwa receptionist!
nikampenda ghafla mzuri sanaa!

nimemfukuzia sana lakini naona hatuelewani anasema sijui kaokoka sijui hataki kuchezewa dah ananichanganya sana....ngoja nitoe picha yake nikuonyeshe... akatoa picha akanionyeshaaa kuangalia tobaaa ndio yule yule ANITA nilipopewa na Pastor Papaaa! nikachoka ndani kwa ndani heee

yule dogo akaniambia huyu hapa Penny unahisi ataweza kunikubali? mimi sina mvuto ila nikizaa na huyu mrembo watoto watatoka vizuri sana sana... sasa unanisaidiaje? nimejaribu kila njia nimeona haiwezekani ananichomoleaaa,

Money Penny: nikajikaza nikamwuliza wewe Aloyce, huyu dada hana mtu kweli mbona mzuri sana?

Aloyce: hana bwana nimemfuatilia mpaka polisi nimemcheki ila kwao mambo safi flan hivi, babake maarufu flan hivi, huenda ndio inampa kiburi au sijui ndio huo ulokole, we nisaidie Da Penny nakuombaa! nakuachia namba yake ya simu, na anapofanya kazi adress anapoishi na majina ya marafiki zake! plz nyie wanawake mnajuana wenyewe mnavyoweza kutoana taarifa nisaidie kama ananifaa nimuwowe fasta nisije nikawahiwa!

Money Penny: nikachokaaa hii ya leo ni Mungu kanishukia au Malaika ananitafutia neema ... uuuuwi mbona sheedah

Kwani wewe Aloyce baada ya kuonana na huyu demu, ulitumia njia gani ya kumtongoza?! labda kuna sehemu unakosea nikusahihishe unajua urafiki na huyu demu bwana staki shida tayar nina shida za kunitosha,

Aloyce: akaanza kuniadithia jinsi show ilivyokuwa

TUONANE TAR 17 MARCH 2018 SAA 2 USIKU YA TZ KUJUA JINSI GANI ALOYCE ALIVYOMFUKUZIA ANITA




glass amo
 
Nawatag mapemaaa staki ubaya na mtu
Alisina Atuganile Mmari tiztizo ChamaB Mhandisi Mzalendo Mhandisi wa Umeme
Jolie Jolie juuuuuuu RED BULL Homeofservices vvm kanali mstaafu Jiwedogo Kichaafulani kichaa cha mbwa Kichaa wa YESU kichaa msafi Nalendwa Ngosha Mashine Ngosha jr Daby mbalizi1 Vladimirovich Putin vladimir fuschs Vladmir Putin kawoli Shubiri Pori Masweeter Shunie Gwallo shubbie jaji mfawidhi Jaji matundu Kyalow Tarime one Demiss NaughtyGuy Naughty girl linguistics mchecheto Karucee DJ Sepetu MIXOLOGIST mmubiayi Smart911 mahondaw Benfamous monde arabe mchumi tumbo adden Davet Ngadu01 steveachi Chris14 Kheri Hansen Dr Garangi Mtoto halali na hela Dossa2008 mtoto wa kipare dos.2020 mtoto wa mjini fix kido joanah Pyaar Kadada saasita saasita omoth Mlatinoh king witnessj Mamaa Africa kifumue Money Talk Money Box Money Stunna sab Mwakamele 16 relis MBITIYAZA Kingwenembe kingwellu Kingwe mdudu kilambimkwidu DrLove69 Mgeni wa Jiji fix kido barafuyamoto barafu finnest espy Bonny MILL8 jakitoo jakichanii Mareth joanah Dreka
John Powese shubbie kitalembwa Bujibuji Pyaar kiumbempole kiumbe kipya Chris14 Kichwa Kichafu kichwa kikubwa Kichwa Kontena Kichwa Ngumu victor moshi Msokwa1 Gyole TsafuRD ben milazo kkenzki Nokia83 sumbai Saint Ivuga SaintErick esc343 Majighu2015 jerrytz sandraeli reyzzap Katavi katavi graphics Msemaji_ Msemachochote Msema yote MsemajiUkweli msemakweli2 Tuchki sumbai chundaji everlenk Evergreen Jr everhurt dottoz kapeace Agustino87 Barn Hany tukulu Tukundane tukulilila ubhumi tukunyemamzee TUKUTUKU Tukuwoni Tuyuku mlogolaje
BIGstallion likandambwasada G7n4_inv Detective J Detective G Detective G detective mfaume keri keri Kheri Hansen KHERY 50thebe Hajar

kama sijakutag naomba unisamehe nimekuwa na marafiki wengi huku mpaka nasahau majina yenu kuwatag ila wote karibuni sana hii stori ni ya kweli ilitokea Tz na pia nimeiandika kwenye website yangu kama unataka kutangulia mbele kuisoma

naomba uwe mvumilivu kwenye kusoma na uweke umakini wa hali ya juu sana maana naenda na spidi ya 5G mieee ... mtanisamehe wale slow lena, msisahau kuuliza maswali nitawajibu kwa upendo

nipo hapa kuwasaidia na sio kumcheka wala kumsema mtu vibaya.. nafanya kwa upendo kwa wazalendo wote mliopo huku​
 
@Money Penny


Hizi kazi za hivi mwisho wake hauwaGi mzuri. Kuna mawili, Anita atahamia kwa Aloyce ama @Money Penny kuhamia kwa Mtumishi Papaa (Blesser) huyu. Ngoja tuone!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom