Story: Kwanini Upo Single?!

Story: Kwanini Upo Single?!

Jamaaani Tereza mpole hana kiburi
Au unawajua nduguzako wagita ni viburi?!

ha ha haa!

Upole na ukorofi haijawahi kuwa sifa ya jumla! Ukiona mdau anatupia sifa hizi kama blankenti ujue ipo shida, tena shida kubwa mno.

Itoshe kusema sababu za Teresia kupigwa haziko wazi!
 
ha ha haa!

Upole na ukorofi haijawahi kuwa sifa ya jumla! Ukiona mdau anatupia sifa hizi kama blankenti ujue ipo shida, tena shida kubwa mno.

Itoshe kusema sababu za Teresia kupigwa haziko wazi!
Sheedah
 
Nipo single kwa sababu nikiwa kwenye mahusiano huwa nahisi nabanwa.... yaani niache kufanya vitu vya maana eti nichat na wewe....aaaaaaaaargggggghhhhhhh
Hahahaha
Acha ukorofi utakufa na tai shingoni shauriako
 
Kulthum mtoto wa kidigo kutokea Tanga, ana matatizo sana... tena matatizo yake yapo ukeeni...

Anasikitisha sana... though amejaribu kua mkweli... hapo hata Koku anasubiri kwanza...

Mwelu ndiyo anaonekana boya mpaka sasa...

Cc: mahondaw
 
Kulthum mtoto wa kidigo kutokea Tanga, ana matatizo sana... tena matatizo yake yapo ukeeni...

Anasikitisha sana... though amejaribu kua mkweli... hapo hata Koku anasubiri kwanza...

Mwelu ndiyo anaonekana boya mpaka sasa...

Cc: mahondaw
Hahaha ah
Yajayo yanafurahisha upo tayari? !
 
D NIPO SINGO KWASABABU NG'OMBE HAWAZEEKI MAINI



Ashakumsi matusi Kwa Mwalimu na wanafunzi wote

Wote: ahahahahaha

Kwajina naitwa Kulthum, sina kifupi wala nini, kama mnavyoniona mimi ni kibonge, mfupi, mtu wa Tanga, Mdigo Baby! Ndio je mimi mfupi wadigo sio wafupi ila mimi ni mfupi

Mfupi na kibonge, nimeishia kidato cha 4, ila sikufaulu nilipata divishen 0 lakini divishen 0 ya shule sio ya maisha

Kwa sasa nina miaka 35, sina mtoto, sijaolewa, nimejiriwa kwenye hotel moja kariakoo kwenye mapokezi. .. Mimi nipo singo Kwa sababu moja tu, kwanza staking kuolewaa, pili staki watoto, tatu nipo singo kwasababu ng'ombe(wanaume) hawazeeki Maini... kwangu mimi kuwa singo ni kama ajira... unajua kwanini?!

Kama mtu ukiwa singo unakula kila kitu na kupata kila kitu bila stress kwanini nikaolewe?!

Ndio mimi kwetu wa kwanza na wadogo zangu washaolewa kwahiyo?! Ina who?! Hai-who babu wee! Habari ndo hio

Nawashangaa hawa waliotangulia wanavyochanganyikiwa kwasababu wapo singo!

Mwana saikolijia: kwanini upo kwenye hili darasa sasa?!

Kuluthum: kusema ukweli, nimekuja Kwa ajili ya hizo safari unazosema baada zitakuwaepo, as hivi sina bwana nategemea kupata bwana kama tutasafiri, hela yangu haiendi bure, nilipolipa ada nilijua nalipa kwa ajili ya nini

Inawa watu wananisema nimepagawa na machine za kiume lakini me najiona nipo sawa, sijapagawa

Nyie hamjui tu, wanaume muwatumie mkiwa na shida tuu au mna hamu tuuu, mambo ya kujigandisha Kwa wanaume weee ndio mana mnalizwa

Mimi hakuna mwanaume ananisumbua kichwa, sina muda wa kupendaa

Mimi napendwa tu, na nikiona unanipenda sana nakuachaaa

Watu wanapenda kuniita Mdangaji, ila mimi siamini kama ni mdangaji kwasababu zifuatazo:

1. Wanaume siwafuati wananifuata wenyewee na najua jinsi ya kuwapata bila kutumia nguvu

Mfano: najua wanaume wanapopatikana, nikitaka mwanaume wa aina flani labda matajiri, naenda sehemu za matajiri tuuu, kama Masaki, Mbezi Beach, Kunduchi, Zanzibar, Arusha, Mwanza yani kwenye mahotel makubwa makubwa tu sio hotel zenu mavi mavi alafu unamlaumu Mungu hakupendi wakati wewe hujui kuzitumia hela na uchumi ambao Mungu kakupa

Disco vumbi sijui maisha basement siendi, wala mende baa siendi kwanza ukinikuta ntaumwaa bora nilale nyumbani

2. Najua kujitoa ufahamu
Nikitoka out kwenda kudanga kwanza sivai chupi, ya nini, pili lazima nivae kivazi cha kutega cha kumwita mwanaume njoo, tatu akija lazima nijinatishe nanata kiduuuuchu ili nione ana uwezo kiasi gani sio unajirahisiiiisha mpaka anakuona njaa hapanaaa


Akikubali kukaa na mimi kula na kunywa lazima alipe yeye, akishakipa labda lakini 2 au 3 maana mimi vinywaji vya pombe za mataputapu sinywi ..bili zangu zote nikiamua kutoka kima cha chini ni laki 2 au 3

Lazima uizoee baa yako na uwe na urafiki na ma baa attendant, maana wateja wengine wakorofi, akikataa kulipa bili mliotumia unaongea na baa maid anakusaidia unaondoka zako, anakamatwa yeye

Nikiona mwanaume anazuga hataki kulipa najua huyu njaa, namwita baa medi namwambia bili atalipa huyu naacha pochi hapa naenda toilet aniangalizie (ndani ya pochi naacha condom 5 na elfu 1 na kitambaa cha kujifuta jasho) akiiba pochi imekula Kwake
Pia inamrahisishia baa medi kudai hela kwa huyo bwana aliejidai kunifuata na kama ataondoka na pochi yangu ndani atakutana na condom na mazagazaga yaliosalia
3. Mapenzi hayana kinyaa
Ukishakubalu kwenda na mwanaume hotel ( sio ghetto lake wala kichumba mbuzi) ... akikwambia weka mguu pande unaweka, mguu sawa unaweka, nenda kushoto unaenda, kulia unaenda
Ukiambiwa kula koni unakula kweli kweli mpaka anapagawa
Tatizo lenu nyie maspinsta watarajiwa mkiwekwa mechini mkabinuliwa mnaanza mapozi me siwezi, me sijui, me siendi, naskia kinyaa, hiki sifanyi, hiki nafanya... unaleta mambo ya kuboa boa unamboa mtu na pombe zake anaona alale tu mwisho wa siku kesjo hakutafuti tena
Mwanaume lazima umchanganye mechini umpagawishe mpaka akiamka asbh anachokumbuka ni jana usiku
Sio unaleta ulokole ulokole Yesu kazema mkazae na kuijaza nchi, kitandani ni malazini lazima ujimwage kama shangingi mmesikia we Teresa na nyau Mwelu?!
Koku: ahahahaha watakuelewa baadae sana hao labda kama ataongea Mwalimu Mwakasege au Mchungaji wa Kanisa Lao ndio watafanya we endelea na somo hili la leo nimeliewa sana
4. Mwanaume akikuita tena nenda kwani shida nini, ukienda mara ya 2 akataka ufanye kama jana au juzi we kubali, akimaliza hapo lazima akupongeze. .. mimi mwenzenu ninaishi kwangu nimejenga kwasababu ya chiu, nimenunua magari 2 kwasababu ya chiu, nina shamba kwasababu ya chiu, kazini nimepandishwa cheo kwasababu ya chiu, chiu imenipeleka ulaya nimesafiri nchi 20 mpaka navyoongea kila nchi haijirudiii nawashangaa nyie
Walokole mnavyokalia chiu utadhani kuna medali mtapewa siku za mwisho woi!
5. Usiombe ombe wanaume hela, yani wewe ukikutana na mwanaume unamtangazia shiiidaaa utadhani umekutana na Mungu, woi!
Kwani wewe mlemavu au?! Si una ajira yako?!
Wanawake sisi tungekuwa na mindset (mtazamo) kama wangu kuwa mwanaume hata akinitumia vipi sitamwomba hela tungefika mbali
Kwanzaa wanaume hawatutumii, tunatumiana, kwani yeye raha hapati au?!
Si wote mnapata?! Sasa unalalamika nini kuwa unatumiwa vibaya na wanaume wanakuzeesha kwani ukikaa mwenyewe hautazeeka?! Tena ndio utalongoroka kwa magonjwa na siku zako za kuishi zitakuwa chache, bora ujitahidi utimize alichokisema Mungu kuwa zaeni mkaongezeke mkaijaze Dunia yaishe
Muache kusingizia wanaume kuwa wanawatumia wote mnatumika sema tu labda mnakuwa hamjapendana
Mimi siwaelewagi wale wanaosema mwanaume kanipotezea Muda, amekupotezeaje kama wewe mwenyewe haujataka kupotezewa?! Kama haukutaka kupotezewa Muda Si ungeondoka kwani alikushika?!
Mwanamke unakuwaje zoba kiasi cha kupotezewa Muda? !
Mimi sipendi watoto nahakikisha siku za hatari najituliza ndani akiniita nasema naumwa au sipokei simu, mahusiano ya kugandana na mwanaume sinaga
Mwana saikolojia: my dia Kuluthum, unaongea kama Mwanamke mwenye maumivu na alievurugwa, skia mami hakuna binadamu alieletwa duniani awe kuwa kisiwa cha watu kupita na kuondoka unauhakika haujawahi kupenda?
Kuluthum: kupenda wanapenda watoto wadogo sio mimi, kwani hamjasikia watu wanasema Wanawake ni Dunia? ! Maanake
Tumeletwa Duniani kutumiwa tu na wanaume
Mwana saikolojia: ukisema hivyo utakuwa umekosea na unajikosesha haki yako ya msingi
Kuluthum: haki za msingi zote nazipata, hizo zako ni zipi?!
Mwana saikolojia: Kuluthum mami, mapenzi sio utumwa mapenzi sio ndoo kiasi kwamba ukinge tuuu maji yawekwe yakatumiwe
wooote hapa tunawazazi waliopendana na kukubaliana wakaoana wakapata watoto tukazaliwa kwa ajili ya mapenzi ya wazazi wetu
Kuluthum: kwahiyo mwl unakata kusema watoto wote wanaozaliwa wanazaliwa kwa sababu ya baba na mama kupendana? ! Je wanaobakwa?! Watoto wanaotelekezwa?!
Mwana saikolojia: naongelea upendo unachokosa ni upendo
Kuluthum: mimi napendwa ndio Maana kila napoenda napata Bwana, sio kama hawa majinga jinga, wanapata mabwana wanaleta pozi wao wanalalamika hamna wanaume
Mwana saikolojia: wewe haupendi wewe hauna tofauti na mtu anayejiuza na sijui kwanini unajiuza kwanini usitafute mtu mkapendana mkaanzisha familia mkapata watoto mkasonga mbele kwanini unachukia sana watoto na wewe ni mzaliwa wa kwanza?! Shida ipo wapi?! Kitu gani kilikutokea mpaka haupendi watoto, ndoa, unatumiwa unaona sawa? !
Kwanini unajidharau namna hii hata thamani yako kuwa Mwanamke hauijui?!
Kila mwanadamu ana thamani, Wanawake wanaume wote wana thamani, sijaelewa kwanini umejidharau kiasi hiki
Kuluthum: love ni Bullshit hamna love Duniani... wanadamu wote nawapenda ila mpaka Sasa sijapata wa kunipenda kunifanya nitulie nianze maisha ya familia naona usanii mwingi tu mtaani
Si unaona mwalimu mwenyewe
Hawa mademu wanalia kuhusu wanaume walivyo wabaya. . Bora tu ufanye yako mengine mbele kwa mbele
Kama ulivyoniuliza kwanini nipo singo na mimi nimekujibu nipo singo kwasababu ng'ombe hazeeki maini, na ng'ombe naowapata mimi hawana stress na mimi, wananitunza, wananilisha, wananivisha, kila kitu napewa, nikisafiri haja kubwa naenda, haja ndogo naenda, hakuna nachokosa kwahiyo mimi kuwa singo hainisumbui kabisa, haya ndio maisha yangu mpaka nitakaporudisha namba kwa Muumba hata kama mtanihukumu
Mwana saikolojia: akachokaa! Akaamua kuweka pozi baadae akaendelea
Ambacho mnanishangaza wote mliosema hapo awali ni kwamba wanaume wote wabaya Je mmeshawahi kujiuliza wenyewe kama nyie mnaowashutumu wanaume kama ni wazuri?
Kama wewe ni mbaya au una tabia mbaya au unaroho mbaya kwanini upate mwanaume mzuri?!
Hamjawahi kusikia kizuri kinavuta kizuri chenzake?! Hata sikumoja Mungu hawezi kukupa Kitu tofauti na ulivyo, anakupa wa kufanana nawe
Leo ninawapa homework mkifika nyumbani andikeni kwenye makaratasi ma5 tofauti
Karatasi la:
1. Andika wanaume wooote uliowahi kuwa nao kimapenzi tangu unakua mpaka sasa ... Hata kama bwana wako alikuwa mchungaji au sheikh mimi sitahukumu
2. Andika mazuri yooote ya hao wanaume uliokutana nao
3. Andika mabaya ya hao wanaume wooote uliokuwa nao
4. Andika mazuri yako yoooote unayohisi na kujua unayo
5. Andika mabaya yoote unayohisi (unayojua) unayo
Alafu kila mtu aniletee darasa lijalo
Najua tumebakia watu 2 kujielezea na Najua wote hatutokuwa mbali na ukweli watakaouelezea lakini naomba muandike na mniwekee kwenye bahasha za A4 juu ya bahasha muandike majina yenu 3 mniletee kila mtu kwa wakati wake. .. sawa
Wote: sawa mwalimu

KWA MWENDELEZO WA SEHEMU YA PILI

BONYEZA LINK KWANINI UPO SINGO (SINGLE)? - MONEY PENNY TZ KUISOMA

aisee hiyo site mbona immekaa kizee alie itengeneza, iweke vizuri tuwe tuna soma kila siku>>>>HABARI ZERO
 
Back
Top Bottom