BIG BROTHER ALEX
JF-Expert Member
- Sep 24, 2025
- 1,293
- 2,214
Hii inshu ya El Chapo imenikumbusha kaka yangu.
Mwaka fulani maeneo fulani Kanda ya Ziwa, katika mkoa mpya fulani, kipindi hicho palikuwa bado bush sana. Kaka yangu alikuwa akijihusisha na utafsiri wa movie za kihindi, kizungu na kichina katika ukumbi mkubwa sana kwa kipindi hicho.
Kutokana na mazingira ya wakati huo, DJ alionekana kama super star mwenye ufahamu mkubwa wa mambo. Just imagine unaangalia Kuch Kuch ya Shah Rukh Khan, halafu unatafsiriwa na mtu makini. Akili inakutuma kwamba huenda DJ naye ni fundi kama Shah Rukh Khan tu.
Sasa katika wateja waliokuwa wanaingia pale ukumbini kulikuwa na dada mmoja, si jina lake halisi, aliitwa Mwaida. Huyu alikuwa pisi kwa kipindi hicho, ashikiki. Washikaji wengi walijigonga sana. Alikuwa kama Wema Sepetu wa miaka hiyo mkoani.
Sasa basi yule demu akatokea kumpenda bro kwa sababu bro alikuwa star, na yeye pia akataka kuwa na demu star. Tetesi zinadai demu ndiye aliyemtongoza bro, na bro akajaa kwa sababu demu alikuwa pisi na star hapo mkoani.
Baada ya muda, bro aliacha kazi pale na kuhamia sehemu nyingine yenye masilahi zaidi akiwa na Mwaida. Wakaanza kuishi pamoja kama mpenzi na mpenzi wake.
Siku moja akiwa ndani, alishangaa mlango unagongwa kwa fujo. Akauliza ni nini tena. Ikabidi Mwaida afungue. Mara ghafla polisi wakaingia na kuwaamuru wote waliinua mikono juu chini ya ulinzi. Bro akawa anashangaa kinachoendelea. Polisi wakadai wamekamata majambazi waliodai kuwa walikuwa wakificha silaha zao, yaani bunduki, kwa bro, hivyo walikuja kuzifuata na kumtaja bro pamoja na demu wake kama washiriki.
Bro alishangaa na kukataa, akisema hana silaha yoyote ndani ya geto lake. Lakini wale majambazi wakamwonyesha Mwaida na kusema anajua zilipo. Baada ya kofi moja tu, Mwaida alibinua kitanda, akafungua sehemu fulani na kutoa bunduki. Bro alibaki hana nguvu, hajui hata zilifika humo saa ngapi.
Hapo hapo wakawekwa chini ya ulinzi na kupewa kesi ya ujambazi yeye, demu wake na wale jamaa. Cha kushangaza, haikupita muda demu aliachiwa, huku bro na wale jamaa wakibaki wanateseka. Hawakuhukumiwa mara moja, lakini walikaa miaka jela wakisubiri hukumu.
Hawa mademu kuishi nao kunahitaji maombi sana, na kwa bahati mbaya si rahisi kupambana nao. Mara nyingi mwanaume hujikuta ameshapoteza kila kitu kabla hajagundua kilichotokea.
Mwaka fulani maeneo fulani Kanda ya Ziwa, katika mkoa mpya fulani, kipindi hicho palikuwa bado bush sana. Kaka yangu alikuwa akijihusisha na utafsiri wa movie za kihindi, kizungu na kichina katika ukumbi mkubwa sana kwa kipindi hicho.
Kutokana na mazingira ya wakati huo, DJ alionekana kama super star mwenye ufahamu mkubwa wa mambo. Just imagine unaangalia Kuch Kuch ya Shah Rukh Khan, halafu unatafsiriwa na mtu makini. Akili inakutuma kwamba huenda DJ naye ni fundi kama Shah Rukh Khan tu.
Sasa katika wateja waliokuwa wanaingia pale ukumbini kulikuwa na dada mmoja, si jina lake halisi, aliitwa Mwaida. Huyu alikuwa pisi kwa kipindi hicho, ashikiki. Washikaji wengi walijigonga sana. Alikuwa kama Wema Sepetu wa miaka hiyo mkoani.
Sasa basi yule demu akatokea kumpenda bro kwa sababu bro alikuwa star, na yeye pia akataka kuwa na demu star. Tetesi zinadai demu ndiye aliyemtongoza bro, na bro akajaa kwa sababu demu alikuwa pisi na star hapo mkoani.
Baada ya muda, bro aliacha kazi pale na kuhamia sehemu nyingine yenye masilahi zaidi akiwa na Mwaida. Wakaanza kuishi pamoja kama mpenzi na mpenzi wake.
Siku moja akiwa ndani, alishangaa mlango unagongwa kwa fujo. Akauliza ni nini tena. Ikabidi Mwaida afungue. Mara ghafla polisi wakaingia na kuwaamuru wote waliinua mikono juu chini ya ulinzi. Bro akawa anashangaa kinachoendelea. Polisi wakadai wamekamata majambazi waliodai kuwa walikuwa wakificha silaha zao, yaani bunduki, kwa bro, hivyo walikuja kuzifuata na kumtaja bro pamoja na demu wake kama washiriki.
Bro alishangaa na kukataa, akisema hana silaha yoyote ndani ya geto lake. Lakini wale majambazi wakamwonyesha Mwaida na kusema anajua zilipo. Baada ya kofi moja tu, Mwaida alibinua kitanda, akafungua sehemu fulani na kutoa bunduki. Bro alibaki hana nguvu, hajui hata zilifika humo saa ngapi.
Hapo hapo wakawekwa chini ya ulinzi na kupewa kesi ya ujambazi yeye, demu wake na wale jamaa. Cha kushangaza, haikupita muda demu aliachiwa, huku bro na wale jamaa wakibaki wanateseka. Hawakuhukumiwa mara moja, lakini walikaa miaka jela wakisubiri hukumu.
Hawa mademu kuishi nao kunahitaji maombi sana, na kwa bahati mbaya si rahisi kupambana nao. Mara nyingi mwanaume hujikuta ameshapoteza kila kitu kabla hajagundua kilichotokea.