Stop lines kwenye kila zebra crossing? Think again!!

Stop lines kwenye kila zebra crossing? Think again!!

Barabarani

Member
Joined
Sep 27, 2017
Posts
19
Reaction score
8
Sehemu nyingi nchini wameweka hii mistari ya “Simama” (Stop lines) kwenye kila vivuko vya watembea kwa miguu. Japokuwa lengo ni zuri, pengine wahusika hawajafikiria vizuri hasara, usumbufu na mkanganyiko unaoletwa na hii mistari. Nitatoa mifano michache tu.

1. Stop Lines peke yake bila kuwepo Stop signs, Stop Warning Sign au Stop markings.

Mstari wa Simama (Stop Line) huambatana na alama ya Simama (Stop Sign) na kazi yake ni kuashiria wapi usimamishe gari lako kabla ya kufika kwenye kivuko. Mstari mzima kabla ya kivuko cha watembea kwa miguu KIMSINGI unakutaka usimame, bila kujali kama kuna mtembea kwa miguu au la.

Tatizo ni pale unakutana na huo mstari bila hata ya kuwepo Alama ya Simama, Tahadhari au hata Mchoro wa barabarani kukuonya mapema kuwa mbele kuna kivuko cha watembea kwa miguu ambapo utalazimika kusimama. Hili ni muhimu kwani kimsingi Alama ya kivuko cha watembea kwa miguu yenyewe haimrishi mtu kusimama hivyo basi ili kuondoa kushtukiza watu ni budi pawepo alama ya tahadhari au amri kwa madereva kuwa watawajibika kusimama wakifika eneo husika. Surprises barabarani ni hatari. Ni vizuri mistari hii iambatane na alama ya Simama au neno “Stop/Simama” kwenye lami au iondolewe kabisa.

2. Hakuna mantiki ya stop lines kwenye kila kivuko cha watembea kwa miguu kwenye barabara za barabarani 30/50 speed limits.
Ukishadhibiti mwendokasi mpaka30/50 kmh unakuwa umemuongezea dereva uwezo na muda wa ku-scan njia vizuri na kuona kama kuna watumiaji wengine wa barabara. Kitaalam ukiwa unaendesha 50kmh, unakuwa na breaking distance ya mita 14-15. Maana yake ni kwamba ukiwa unaendesha 50kmh, ukianza kushika breki gari lako litatembea mita 14-15 hadi liweze kusimama kabisa. Kwa spidi ya 50, utaona kabisa kwamba dereva atakuwa na uwezo wa kuona kivuko au watembea kwa miguu mapema na kusimama kuwapisha na hasa ukizingatia kuwa kuna alama za tahadhari ya kuwepo kivuko cha watembea kwa miguu. Ni kweli pia kwamba madereva wengi hawasimami kuwapisha watu wanaojaribu kuvuka lakini ufumbuzi sio kuweka Stop lines kwenye kila kivuko au kulazimisha magari kusimama kwenye kila kivuko cha watembea kwa miguu hata kama hakuna mtu anayevuka. Pengine aidha tutumie bumps au iwe ni lazima kusimama kama tu kuna watu wanaovuka.

3. Kwenye maeneo ya makazi au miji Stop lines kwenye vivuko vya watembea kwa miguu zinaleta usumbufu usio wa lazima hasa pale unapokuta kuna vivuko kadhaa vya watembea kwa miguu vimeachana mita chache. Mfano mjini kila baada ya mita mia tano unakuta zebra crossings yenye Stop lines, ambazo kimsingi zinakutaka usimame hata bila pedestrians kuwepo. Utasimama mara ngapi bila kusababisha jam au ajali ya kugongwa na magari yanayotokea nyuma? Ni aidha hatujali muda au hatufahamu vizuri muktadha wa kutumia hizi Alama za Barabarani.

Tufikirie tena vizuri.
Barabarani.

>>>Kama unahitaji kujifunza zaidi kuhusu alama za barabarani, unaweza ku-download Application ya simu ya AlamaBarabarani Quiz - Google Play au App Store -
85c851f6e4922d6aa12dae0205ea1105.jpg
 
Kweli mkuu.

Hapo Mlandizi, Ruvu, Chalinze ni balaa. Malori yanasimama kila panapo zebra crossing regardless of uwepo wa wavukaji.

Mfano Zebra crossing ya JKT club pale, its pathetic.

Foleni yake pia ni balaa. Lori ikisimama mpaka iamke sio kazi ndogo. Nyinyi huku nyuma mshachimba dawa kabisa yeye ndio anaanza mwendo.

Ila nadhani yale yanakuwaga malori ya nchi jirani (Congo, Rwanda) since nimesikia kuwa kwao ni lazima kusimama na kuwasha hazard kwenye zebra crossing.
 
Logic ni nini kusimama tu hata kama hakuna mtu? Navyojua mimi ni unapswa kusimama hata kama kuna mtu mmoja anahitaji kuvuka...
 
Na ndiyo maana unnecessary que inazalishwa. Kwa wenzetu kuna madaraja ya Manzese,Buguruni na Furahisha kila mahali panapohitaji kuvusha watu.
Issue hapo ni gharama kubwa. Japo Botswana nasikia wamejitahidi sana
 
Ona tunavyopata tabu from jangwani to ubungo via morogoro road. Mpaka traffic police anakaa kwenye zebra crossing kuwazuia wavukaji esp maeneo ya manzese, argentina na tip top watu wako busy kuvuka muda wote kama hawana shughuli nyingine za kufanya
 
Kweli mkuu.

Hapo Mlandizi, Ruvu, Chalinze ni balaa. Malori yanasimama kila panapo zebra crossing regardless of uwepo wa wavukaji.

Mfano Zebra crossing ya JKT club pale, its pathetic.

Foleni yake pia ni balaa. Lori ikisimama mpaka iamke sio kazi ndogo. Nyinyi huku nyuma mshachimba dawa kabisa yeye ndio anaanza mwendo.

Ila nadhani yale yanakuwaga malori ya nchi jirani (Congo, Rwanda) since nimesikia kuwa kwao ni lazima kusimama na kuwasha hazard kwenye zebra crossing.



Mambo mengine yanafanyika kama vile wanaofanya walikosa kwa kuelekeza fedha iliyobaki kwenye budget ya mwaka, unaweza kusikia "fedha hii imebaki ikatumike wapi, ...hebu tafutenitafuteni maeneo kachoreni zebra ili fedha itumike" kuna baadhi ya maeneo zebra zimechorwa in less than 200 M, mfano mmojawapo ni pale Kihonda Morogoro karibu na njiapanda ya VETA, then ukishuka kidogo tu kama unaelekea mjini kama 120 M, eneo wanalochomelezea mageti kuna zebra, hii ni dalili kuwa kunakosekana kabisa creativity mfano tungeweza kufikiria kujenga madaraja ya bei nafuu hata kama ni ya kamba ngumu.
 
Foleni yake pia ni balaa. Lori ikisimama mpaka iamke sio kazi ndogo. Nyinyi huku nyuma mshachimba dawa kabisa yeye ndio anaanza mwendo.

Ila nadhani yale yanakuwaga malori ya nchi jirani (Congo, Rwanda) since nimesikia kuwa kwao ni lazima kusimama na kuwasha hazard kwenye zebra crossing.


Ungefanywa utaratibu wa ku review haya mambo nchi nzima, ikiwa ni pamoja na kuondoa matuta, tunatumia fedha nyingi sana za kigeni kununua mafuta yanayotumika excessively kwenye matuta na ununuzi wa vipuri kutokana na matuta kuharibu magari, huwa sielewi kama wanaofanya haya wanalazimishwa na wale wasiotumia barabara kusafiri au wanaoneemeka na adha hizo
 
Ungefanywa utaratibu wa ku review haya mambo nchi nzima, ikiwa ni pamoja na kuondoa matuta, tunatumia fedha nyingi sana za kigeni kununua mafuta yanayotumika excessively kwenye matuta na ununuzi wa vipuri kutokana na matuta kuharibu magari, huwa sielewi kama wanaofanya haya wanalazimishwa na wale wasiotumia barabara kusafiri au wanaoneemeka na adha hizo
Mkuu, wao wanasafiri na VX V8 za serikali wakiwekewa mafuta na serikali.

Efficiency ya Biashara hawaijui, na hawawashirikishi wadau ambao kwao barabara ni biashara.
 
Logic ni nini kusimama tu hata kama hakuna mtu? Navyojua mimi ni unapswa kusimama hata kama kuna mtu mmoja anahitaji kuvuka...
Hawa watu wetu wa usalama barabarani wana matatizo sana. Sasa kama umesimama wakati HAMNA MVUKAJI nini kitakachokuruhusu uende? Wanachanganya sheria za zebra crossing zenye traffic lights ambazo kuna taa ya kukusimamisha na kuruhusu uende.
Screenshot_2017-08-02-08-53-59.png
 
Ungefanywa utaratibu wa ku review haya mambo nchi nzima, ikiwa ni pamoja na kuondoa matuta, tunatumia fedha nyingi sana za kigeni kununua mafuta yanayotumika excessively kwenye matuta na ununuzi wa vipuri kutokana na matuta kuharibu magari, huwa sielewi kama wanaofanya haya wanalazimishwa na wale wasiotumia barabara kusafiri au wanaoneemeka na adha hizo
Wanaoweka hizo sheria hawafikirii namna hii vinginevyo tusingekuwa hapa tunajadili hii.
 
Wengine huchanganya speed humps na pedestrian crossing.. Huwa nawashangaa sana..
 
Mambo mengine yanafanyika kama vile wanaofanya walikosa kwa kuelekeza fedha iliyobaki kwenye budget ya mwaka, unaweza kusikia "fedha hii imebaki ikatumike wapi, ...hebu tafutenitafuteni maeneo kachoreni zebra ili fedha itumike" kuna baadhi ya maeneo zebra zimechorwa in less than 200 M, mfano mmojawapo ni pale Kihonda Morogoro karibu na njiapanda ya VETA, then ukishuka kidogo tu kama unaelekea mjini kama 120 M, eneo wanalochomelezea mageti kuna zebra, hii ni dalili kuwa kunakosekana kabisa creativity mfano tungeweza kufikiria kujenga madaraja ya bei nafuu hata kama ni ya kamba ngumu.

Exactly, sio kukosa creativity tu ni kukosa ufahamu pia.
 
Mimi niliona Lori limesimama hakuna MTU mvukaji,,ile linataka tutoka akatokea MTU akikimbia kuvuka zebra

Haha. Huko ni ku-risk maisha. Bora mtu aachie lori liende kwanza kama limeshafika kivukoni
 
Logic ni nini kusimama tu hata kama hakuna mtu? Navyojua mimi ni unapswa kusimama hata kama kuna mtu mmoja anahitaji kuvuka...

Hakuna logic.
Ni kwa sababu wahusika wenyewe hawafahamu sheria ya usalama barabarani vizuri
 
Hawa watu wetu wa usalama barabarani wana matatizo sana. Sasa kama umesimama wakati HAMNA MVUKAJI nini kitakachokuruhusu uende? Wanachanganya sheria za zebra crossing zenye traffic lights ambazo kuna taa ya kukusimamisha na kuruhusu uende.View attachment 656672

Exactly. Wanachanganya sheria za guarded (controlled) pedestrian crossing NA unguarded(uncontrolled) pedestrian crossing.
 
Back
Top Bottom