youngkato
JF-Expert Member
- Sep 3, 2014
- 3,642
- 3,660
Stick with one skill au Jifunze Multiple skills ili upate pesa.
Hii kauli inachanganya watu wengi sana wanaamini kwamba inabidi wajifunze skills nyingi sana.
Uhalisia ni unaweza ukajifunza skill moja lakini ukatumia njia tofauti kupata pesa.
Nitakuonesha how👇👇
Unaweza ukajifunza skills hata 10, ukazielewa vizuri, lakini kama hujui au hujajifunza jinsi ya kupata pesa
Kwenye hizo skills unakuwa unapoteza muda.
Nitakuonesha jinsi unavyoweza kujifunza skill moja tu na ukaitumia
Hiyo kupata pesa kuliko mwenye
Skills 10
Tutaanza mfano na skill moja kama graphics design.
Assume wewe ni graphics designer, lakini unaambiwa lazima ujifunze skills nyingi.
Ili kupata pesa haimaanishi ujifunze kila kitu.
Inatakiwa ujifunze jinsi ya kupata pesa kwenye hiyo skill.
Kwanza unatakiwa utengeneze products tofauti
Kwenye graphics design
Utakuwa na service package ya bei ndogo, bei ya kati na bei ya juu
Hizo zote ni package kwa ajili ya
Kuwatumia wateja wako DM.
Mfano hizi bundle za simu
Pili utapata pesa kwa kufundisha watu wengine
Kuna watu wengi wapo tayari kukulipa kufanya kitu ambacho unakijua.
Siku mojamoja tangaza kufundisha kwa mtu mmoja au wachache kwa gharama unayotaka wewe.
MUHIMU ujue kutengeneza kozi
Tatu utapata pesa kwa consultation.
Kila skill inaweza kutolewa kwa consultation.
Mfano wewe ni graphics designer ni rahisi sana kuchaji watu kwa ajili ya consultation kuhusu Branding kwenye biashara yao.
Consultation ni njia nyingine ya kupata pesa.
Nne utapata pesa kwa kutengeza digital products.
Digital products ni nyingi sana kama ebook, courses, templates, graphics, posters, designs etc
Hizo ni digital products unaweza kutengeneza ukawa unauza kwenye hiyo skill yako
Tano utapata pesa kwa kufanya live training:
Hizi meetup, na live classes ni njia nyingine ya kupata pesa kwenye skill yako.
Watu ukiwaonesha unachokifanya as long as kinaleta matokeo.
Watakuja tu uwafundishe
Mwisho utapata pesa kwa kufanya freelancing. Au kufanya kazi na kulipwa.
Remote work ni plan B ya kila mtu,
Kupitia freelancing platforms, social media, utapata wateja wengi sana wa kufanyia kazi.
Jitahidi tu kujulikana na watu wengi.
Unapotaka kupata pesa anza kwa kuangalia jinsi ya kutumia skills ulizonazo kabla hujakimbilia kuongeza skills nyingine.
Pia jifunze jinsi ya kutafuta wateja kupitia social media DM iko open