Mr Alpha
Senior Member
- Jul 31, 2018
- 195
- 522
Kucheza na timu zenye uwezo mkubwa na wachezaji mahiri wanaocheza Ulaya timu zenye uzoefu mkubwa na heshima kubwa kisoka Afrika na duniani inabidi uingie uwanjani kupigana jihadi kwa jasho na damu ili kupata matokeo, tumeona namna ndugu zetu Msumbiji na Angola walivyong'ang'ania vigogo tishio kabisa Misri na Algeria na kupata alama.
Vivyo hivyo Guinea haikupewa nafasi kabisa dhidi ya wababe wa kihistoria Cameroon ila jamaa wamepambana mpaka kimeeleweka. Vipi Cape Verde kuwapiga Ghana hatujapata cha kujifunza? Nadhani kama nchi tumeenda AFCON tujue tumeingia kwenye mapambano hakuna kupigwa kinyonge lazima tuingie na mikakati yetu ya iwe mvua iwe jua lazima Morocco aachie point.
Wachezaji lazima wahusiwe mchezo dhidi ya morocco sio mechi NI VITA.
Ukiingia kwenye vita kuna chaguo moja kuua au kuuawa, Morocco hawaez kukubali matokeo ya sare au kushindwa na kibonde kutoka Afrika Mashariki watatumia kila mbinu kutuadhibu hivyo lazima tuingie na mpango wa kuishangaza dunia. Tumeamua kujitoa kwenye kundi la vibonde au kichwa cha mwendawazimu tuna deni la kuithibitishia dunia kwamba kweli tumetoka huko
Kazi kwenu timu ya hamasa na benchi la ufundi taifa stars wafikishieni ujumbe huu vijana wetu, heshima ya nchi ipo mikononi mwao
Wapambane kama hawatakuja kupambana tena hakika juhudi zao zitaandikwa kwa wino wa dhahabu na kuenziwa milele katika taifa la Tanzania
Mungu ibariki Tanzania
Vivyo hivyo Guinea haikupewa nafasi kabisa dhidi ya wababe wa kihistoria Cameroon ila jamaa wamepambana mpaka kimeeleweka. Vipi Cape Verde kuwapiga Ghana hatujapata cha kujifunza? Nadhani kama nchi tumeenda AFCON tujue tumeingia kwenye mapambano hakuna kupigwa kinyonge lazima tuingie na mikakati yetu ya iwe mvua iwe jua lazima Morocco aachie point.
Wachezaji lazima wahusiwe mchezo dhidi ya morocco sio mechi NI VITA.
Ukiingia kwenye vita kuna chaguo moja kuua au kuuawa, Morocco hawaez kukubali matokeo ya sare au kushindwa na kibonde kutoka Afrika Mashariki watatumia kila mbinu kutuadhibu hivyo lazima tuingie na mpango wa kuishangaza dunia. Tumeamua kujitoa kwenye kundi la vibonde au kichwa cha mwendawazimu tuna deni la kuithibitishia dunia kwamba kweli tumetoka huko
Kazi kwenu timu ya hamasa na benchi la ufundi taifa stars wafikishieni ujumbe huu vijana wetu, heshima ya nchi ipo mikononi mwao
Wapambane kama hawatakuja kupambana tena hakika juhudi zao zitaandikwa kwa wino wa dhahabu na kuenziwa milele katika taifa la Tanzania
Mungu ibariki Tanzania