Mkuu ukweli no kwamba hawawezi kumwalika, mmiliki wa TV anamuunga mkono magufuri ndio maana wanajaribu kutumia fursa yoyote inayojaribu kuonesha udhaifu wa mgombea wa UKAWA. Tanzania ni nchi pekee katika ukanda wa Afrika Mashariki ambayo licha ya kufahamu ukweli Kuwa vyama vya upinzani bado vichanga nguvu nyingi imekuwa ikitumika kuvikandamiza kwa kupotosha mantiki ya uwepo wake. Mi nashangaa kivipi hivi vyama vinakuwa tishio kwa chama kilichopo madarakani miaka zaidi ya 50 mpaka baadhi ya watu kufikia kuandaa mipango ya hila dhidi yao, je wanaoandaa mipango hiyo hawatambui mchango wa vyama vya upinzani duniani kote? Na kulikuwa na haja gani ya kuruhusu mfumo wa vyama vingi kama tulikuwa bado hajutaelewa maana halisi ya msingi wake. Inashangaza kuona baadhi ya viongozi wa dini wanahusisha vyama vya upinzani na vurugu na hii inaonesha kwa nchi kama Tanzania dhana ya upinzani kueleweka bado tunasafari ndefu maana kuna watu kutokana na maslahi binafsi wanaviona ni kikwazo kwa maendeleo yao na wanatumia huu mtizamo hasi kuwa aminisha na wengine.