Star Times waache mchezo mchafu

Star Times waache mchezo mchafu

mfereji

Member
Joined
Jan 20, 2014
Posts
13
Reaction score
1
Nawashukuru Star Times kwa kujibu hoja yangu kuhusu ufanisi wa kisimbuzi chao ya tarehe 21 Februari 2014. Hii ni ishara ya uwajibikaji kwa umma. Kwa maelezo yao, channels za bure hazionekani vizuri kutokana na kukosa ushirikiano toka kwa wenye stesheni za TV husika yaani ITV, EATV, TBC, Star Tv na Channel Ten. Nawashauri Star Times wawasiliane na TCRA ili wawalazimishe wahusika kutoa ushirikiano kwani suala la kuonyesha stesheni za bure ni la KISHERIA na siyo HIARI. Sheria na Kanuni za mawasiliano ya Kielektroniki ziko wazi juu ya suala hili. Wasiingize maslahi binafsi katika suala hili ili kulazimisha watu kununua visimbuzi vyao. TCRA waingilie kati kwani ndio wasimamizi wakuu wa suala hili.
 
mdau, ukiongelea sheria, wao pia wanazijua wameshaona udhaifu wa iyo sheria ndo maana watumia fursa Kui-exploit. kuna msemo wa utamlazimisha punda kwenda kisimani lakini huwezi kumlazimisha kunywa maji.
unadhani Hao star times hawajawasiliana na TCRA? na je unadhani Hao TCRA hawajui kuna tatizo la channel za bure kusumbua kwenye visimbusi?

wakae pamoja wazungumze kila mtu ajue anafaidikaje na channel yake kuonyeshwa na visimbusi vingine.
 
Back
Top Bottom