St Peters Oysterbay rekebisheni Hili

ngongoti2000

JF-Expert Member
Nov 20, 2017
2,235
2,124
Kama muumini wa kanisa katoliki pale St Peters Oysterbay na Mwananyamala kuna mapungufu ambayo(at least machache ninayoyaonaga) ningependa wahusika wayaangazie macho na wayarekebishe ikiwezekana(siyo lazima);
1. Kutokupangwa kwa viti vya ziada pale nje kabla ya Misa:-kwa kawaida karibu jumapili zote waumini huwa hawatoshi ndani ya kanisa(limeshakuwa dogo) hivyo hulazimika kukaa nje.Hali inakuwa mbaya zaidi siku za misa kubwa kama za sikukuu e.g ijumaa kuu,xmas,pasaka nk...lakini pamoja na kuwa viti vipo vya kutosha kule madarasani karibu na ukumbi wa Rugambwa, hakuna juhudi zinazozofanyikaga kuvipanga viti maeneo ambayo watakaa watu waliochelewa kabla ya misa haijaanza.Nasema hivi kwa sababu huwa kuna usumbufu mkubwa wakati misa inaendelea kuona watu wakipishana na kuburuza viti kule nje.Halafu kibaya zaidi kuna watu wengine huwa hawajui kama kuna zoezi hilo la kufuata viti hivyo wanabaki wamesimama ,hakuna mtu anayeshughulika na watu walio nje ya kanisa.Kwa mfano juzi kwenye misa ya Kipaimara na Komunyo ni misa kubwa (nilikuwa sijahudhuria siku nyingi) nilishangaa bado mchezo ni ule ule...nimefika hakuna viti kabisa nje....watu wakaanza kujaa zikaanza pilika pilika za kwenda kubeba viti ,si wazee , si vijana si watoto wote tunakimbizana na viti kama tupo shule ya msingi.....huku askofu Ruwaichi anaendelea na misa...kuna wengine tena watu wazima wallikuwa hawana habari kama kuna viti vya ziada kule madarasani hivyo wakawa wamekaa kwenye majani,mawe,vizingiti,chini nk hakuna maelekezo yeyote....sasa nikawa najiuliza , ninavyojua kila jumapili huwa kuna wasimamizi wa huduma kanisani....hili suakla la kupanga viti vya kutosha kule nje lina vikwazo gani???labda wadau mnieleweshe kama kuna masharti au ni nini?Mbona kanisa la Mwananyamala huwa tunakuta viti vya kutosha kule nje na huwa wanabadilisha idadi ya viti kulingana na ukubwa wa misa?? sijawahi kuona mtu akikosa kiti labda kama vyoote vimekwishachukuliwa na vinatumika lakini huwa vyote vinapangwa kule nje.

2.Maji ya baraka - haya huwa yanapatikana ndani tu ya kanisa. sasa kama kuna watu wengi nje manake misa ikiisha kama ukitaka uchovye maji ya baraka ambayo yapo ndani mnakutana na watu wa ndani wanatoka nje...sasa pale kuna kuwa na chaos/misuguano ambayo sioni kama ni ya lazima..waumini wengine huamua kutochovya maji ya baraka kabisa sababu ya ule msuguano wa jinsi ya kupishana .Ukilinganisha na Mwananyamala, maji ya baraka yanapatikana pia kwa watu wa nje(au siyo sahihi?)...yaani huhitaji kuingia ndani ili upate maji ya baraka.Sasa pia hapa najiuliza kama hili nalo ni kuna masharti au nini kikwazo???
Ofcourse nilishaongeaga na mzee wa kanisa mmoja pale st Peters lakini naoana labda alipitiwa au halikuwa na uzito kwake.
Nawasilisha wadau kwa ajili ya maoni, kunielimisha nk
 
Ushauri /malalamiko yako umeisha yafikisha kanisa husika? kwa kawaida mambo ya kanisani hutatuliwa kanisani, na uzuri ofisi za kanisa zinakuwa wazi jumatatu adi jumamosi,
 
Kuna ibada zaidi ya tatu, kwanini unaenda hiyo ya kujazana na msongamano?

Kuna makanisa mangapi unayoweza kwenda zaidi ya St. Peters? Yapo mengi sana.

Acha kulalamika, ukifika kama viti unaviona humo ukumbini chukua tenga kaa, wenzako nao watajiongeza.

Alafu acha kulala sana, kwanini unachelewa kanisani mpaka unakosa seat kila siku.
 
Sidhani kama huo uongozi wa kanisa upo humu ndani,

Ni vyema ukaenda siku ambazo sio za ibada,ukaonana na mhusika ukamueleza haya naamini atalishughulikia.
 
Ujumbe wako una lengo zuri sana, ;1)ungeenda pale kanisani ukamueleza paroko 2)malalamiko kama haya hujadiliwa kwenye jumuiya, unahudhuria? 3) unaweza kuwa unaenda na kiti chako 4) uwe unawahi, ibada huwa njema unapowahi 5) hamasisha upanuzi wa kanisa, inakubalika.
 
Kuna ibada zaidi ya tatu, kwanini unaenda hiyo ya kujazana na msongamano?

Kuna makanisa mangapi unayoweza kwenda zaidi ya St. Peters? Yapo mengi sana.

Acha kulalamika, ukifika kama viti unaviona humo ukumbini chukua tenga kaa, wenzako nao watajiongeza.

Alafu acha kulala sana, kwanini unachelewa kanisani mpaka unakosa seat kila siku.
kila mtu anahaki ya kutoa maoni yake acha kumpangia jinsi ya kuishi. kama hayakuhusu pita hivi
 
Kuna ibada zaidi ya tatu, kwanini unaenda hiyo ya kujazana na msongamano?

Kuna makanisa mangapi unayoweza kwenda zaidi ya St. Peters? Yapo mengi sana.

Acha kulalamika, ukifika kama viti unaviona humo ukumbini chukua tenga kaa, wenzako nao watajiongeza.

Alafu acha kulala sana, kwanini unachelewa kanisani mpaka unakosa seat kila siku.
kila mtu anahaki ya kutoa maoni yake, acha kumpangia mtu mwingine jinsi ya kuishi. kama hiyo mada haikuhusu na huna cha kushauri pita hivi
 
Ushauri /malalamiko yako umeisha yafikisha kanisa husika? kwa kawaida mambo ya kanisani hutatuliwa kanisani, na uzuri ofisi za kanisa zinakuwa wazi jumatatu adi jumamosi,
Ingekuwa hivyo basi hiI mitandao ya kijamii haina maana...kila mtu anatakiwa akalalamike kunako husika..kama huna jibu piga kimya
 
Ujumbe wako una lengo zuri sana, ;1)ungeenda pale kanisani ukamueleza paroko 2)malalamiko kama haya hujadiliwa kwenye jumuiya, unahudhuria? 3) unaweza kuwa unaenda na kiti chako 4) uwe unawahi, ibada huwa njema unapowahi 5) hamasisha upanuzi wa kanisa, inakubalika.

1&2)Paroko nitamuona saa ngapi??? mimi kwa sasa nilishahamia kwingine pale nakwenda kama mgeni tu
3|) Viti vipo siyo tatizo pale
4) Hata kama nikiwahi, mara zote kuna watu nje waliochelewa
5)Namini mipango ipo
 
Kuna ibada zaidi ya tatu, kwanini unaenda hiyo ya kujazana na msongamano?

Kuna makanisa mangapi unayoweza kwenda zaidi ya St. Peters? Yapo mengi sana.

Acha kulalamika, ukifika kama viti unaviona humo ukumbini chukua tenga kaa, wenzako nao watajiongeza.

Alafu acha kulala sana, kwanini unachelewa kanisani mpaka unakosa seat kila siku.
Hata kama siendi kusali pale bado kunahitajika utaratibu mzuri wa kuwa accomodate waliochelewa
Mbona kanisa kama Mwananyamala huwa wana utaratibu mzuri wa kuwapangia waumini viti??? Mimi nilihamakanisa la obay na sasa nasali Mwananyamala baada ya kuhama makazi ,huku naona kama jumuiya inazamu ya wiki basi jukumu la kupanga viti nk ni la jumuiya husika ndiyo maana sioni kuna shida gani
 
1&2)Paroko nitamuona saa ngapi??? mimi kwa sasa nilishahamia kwingine pale nakwenda kama mgeni tu
3|) Viti vipo siyo tatizo pale
4) Hata kama nikiwahi, mara zote kuna watu nje waliochelewa
5)Namini mipango ipo
nimependa majibu yako, ila 1&2, ungekuwa na nia ya dhati na kwa kuona kuna uhitaji huo, usingeshindwa kuupeleka pale huu ujumbe, kama uliweza kuabudu pale siku hiyo.... nia yako ni nzuri sana...ukiiufikisha pale direct nna hakika ungepata majibu yasiyo na shaka, kama no. 5- kuna mipango ipo.
 
Kama muumini wa kanisa katoliki pale St Peters Oysterbay na Mwananyamala kuna mapungufu ambayo(at least machache ninayoyaonaga) ningependa wahusika wayaangazie macho na wayarekebishe ikiwezekana(siyo lazima);
1. Kutokupangwa kwa viti vya ziada pale nje kabla ya Misa:-kwa kawaida karibu jumapili zote waumini huwa hawatoshi ndani ya kanisa(limeshakuwa dogo) hivyo hulazimika kukaa nje.Hali inakuwa mbaya zaidi siku za misa kubwa kama za sikukuu e.g ijumaa kuu,xmas,pasaka nk...lakini pamoja na kuwa viti vipo vya kutosha kule madarasani karibu na ukumbi wa Rugambwa, hakuna juhudi zinazozofanyikaga kuvipanga viti maeneo ambayo watakaa watu waliochelewa kabla ya misa haijaanza.Nasema hivi kwa sababu huwa kuna usumbufu mkubwa wakati misa inaendelea kuona watu wakipishana na kuburuza viti kule nje.Halafu kibaya zaidi kuna watu wengine huwa hawajui kama kuna zoezi hilo la kufuata viti hivyo wanabaki wamesimama ,hakuna mtu anayeshughulika na watu walio nje ya kanisa.Kwa mfano juzi kwenye misa ya Kipaimara na Komunyo ni misa kubwa (nilikuwa sijahudhuria siku nyingi) nilishangaa bado mchezo ni ule ule...nimefika hakuna viti kabisa nje....watu wakaanza kujaa zikaanza pilika pilika za kwenda kubeba viti ,si wazee , si vijana si watoto wote tunakimbizana na viti kama tupo shule ya msingi.....huku askofu Ruwaichi anaendelea na misa...kuna wengine tena watu wazima wallikuwa hawana habari kama kuna viti vya ziada kule madarasani hivyo wakawa wamekaa kwenye majani,mawe,vizingiti,chini nk hakuna maelekezo yeyote....sasa nikawa najiuliza , ninavyojua kila jumapili huwa kuna wasimamizi wa huduma kanisani....hili suakla la kupanga viti vya kutosha kule nje lina vikwazo gani???labda wadau mnieleweshe kama kuna masharti au ni nini?Mbona kanisa la Mwananyamala huwa tunakuta viti vya kutosha kule nje na huwa wanabadilisha idadi ya viti kulingana na ukubwa wa misa?? sijawahi kuona mtu akikosa kiti labda kama vyoote vimekwishachukuliwa na vinatumika lakini huwa vyote vinapangwa kule nje.

2.Maji ya baraka - haya huwa yanapatikana ndani tu ya kanisa. sasa kama kuna watu wengi nje manake misa ikiisha kama ukitaka uchovye maji ya baraka ambayo yapo ndani mnakutana na watu wa ndani wanatoka nje...sasa pale kuna kuwa na chaos/misuguano ambayo sioni kama ni ya lazima..waumini wengine huamua kutochovya maji ya baraka kabisa sababu ya ule msuguano wa jinsi ya kupishana .Ukilinganisha na Mwananyamala, maji ya baraka yanapatikana pia kwa watu wa nje(au siyo sahihi?)...yaani huhitaji kuingia ndani ili upate maji ya baraka.Sasa pia hapa najiuliza kama hili nalo ni kuna masharti au nini kikwazo???
Ofcourse nilishaongeaga na mzee wa kanisa mmoja pale st Peters lakini naoana labda alipitiwa au halikuwa na uzito kwake.
Nawasilisha wadau kwa ajili ya maoni, kunielimisha nk

Umewasilisha kwenye Jumuiya yako hoja hii au katika utaratibu wa kawaida wa Kanisa Katoliki??? Hivi kweli imefika masuala haya eti yajadiliwe humu mitandaoni???!!!
 
Wakuu huyu ndugu ametoa malalamiko ya msingi asibezwe bwana! Kama Askofu hapiti humu lakini baraza la Walei wanapita humu! Hata Mapadre huwa wanapita humu hivyo ujumbe utakuwa umefika!
 
Back
Top Bottom