St Aloysius versus St Mary Goreti

St Aloysius versus St Mary Goreti

Kambaku

JF-Expert Member
Joined
Nov 12, 2011
Posts
8,709
Reaction score
32,477
Wakuu natumaini mko poa na poleni na mihangaiko.

Nina mjukuu wangu kamaliza 'la saba' mwaka huu na katika hangaika hangaika yake kafanikiwa kufaulu interview katika shule mbili, St Aloysius girls iliyoko Visiga, Kibaha Pwani na St Mary Goreti iliyoko Moshi, msaada kwa anayezijua shule hizi ki undani ipi ni bora zaidi?

Kwangu shule nzuri ni inayotoa elimu bora, yenye mazingira bora na inayofundisha maadili

Nitashukuru sana kwa ushauri
 
mpeleke mary goreti wanatoa elimu nzuri sana na mwanao lazima afaulu maana naijua hiyo shule vizuri ipo mjini moshi wana maadili mazuri sana mtoto hawezi kua mtundu
 
mpeleke kwa masister pale MARIAGORET hutajuta kuacha pale milion tatu na upuuzi kila mwaka
 
Mkuu, mimi nazijua hizo zote. Ya Moshi-Maria Goreti ni shule kongwe na bora. Aloysius ya pale Visiga Zegereni ni shule changa sana na bado haijajipambanua kitaaluma kama Goreti. Ingawa, zote ni shule zenye maadili mema ya kidini na kimaisha.
 
matokeo ya form 4 yaliyotoka jana yapo hivi:

St Aloysius imeshika nafasi ya 12 kitaifa (mwaka jana ilikuwa ya 6).

St Mary Goret imeshika nafasi ya 52 kitaifa (mwaka jana sijui)

common sense inahitajika hapo.
 
matokeo ya form 4 yaliyotoka jana yapo hivi:

St Aloysius imeshika nafasi ya 12 kitaifa (mwaka jana ilikuwa ya 6).

St Mary Goret imeshika nafasi ya 52 kitaifa (mwaka jana sijui)

common sense inahitajika hapo.
Haijalishi Mkuu, matokeo hubadilika.
 
matokeo ya form 4 yaliyotoka jana yapo hivi:

St Aloysius imeshika nafasi ya 12 kitaifa (mwaka jana ilikuwa ya 6).

St Mary Goret imeshika nafasi ya 52 kitaifa (mwaka jana sijui)

common sense inahitajika hapo.
Kwa wazazi kuna kucheza kamali kwenye haya majambo. Mimi ningechukua risk ya kumpeleka St Aloysius hata kama matokeo hubadilika. Kinidhamu sidhani kama zinapitana sana (hizi ni hisia zangu tu).
 
Naijua Maria Goreti vizuri.
Wapo vizuri.
Tatizo la sister Njau ni kuchukua wanafunzi wengi!! Kama over 140! Na ndio maana walipata div 4 chache zinawashusha. Ukiangalia matokeo ya mmoja mmoja utagundua wamefanya vizuri sana. Aloysius siifahamu.
 
Naijua Maria Goreti vizuri.
Wapo vizuri.
Tatizo la sister Njau ni kuchukua wanafunzi wengi!! Kama over 140! Na ndio maana walipata div 4 chache zinawashusha. Ukiangalia matokeo ya mmoja mmoja utagundua wamefanya vizuri sana. Aloysius siifahamu.
Ni kweli...
 
Hivi bado Sister Njau ni headmistress pale Mary G...??

Wame-drop sana sana....si kawaida...something must be done kuinusuru
Sister mtata sana...ila bado mtaani watu walikuwa wanatafuna watoto wake.
 
Back
Top Bottom